JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumapili, 18 Mei 2025

ZIARA YA KUSHTUKIZA VIWANDANI YAFANYWA NA KAMISHNA MKUU WA TRA


Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuph Juma Mwenda amefanya ziara ya kushitukiza kwenye baadhi ya Viwanda vilivyopo wilayani Mkuranga mkoani Pwani na kubaini kuwepo kwa ukwepaji mkubwa wa Kodi.unaofanywa na wamiliki wa Viwanda hivyo.


Jana Mei 17, 2025 akiwa katika kiwanda cha kuzalisha viatu vya Plastiki maarufu kama Yeboyebo cha DOLIN Investment Company Ltd na Kiwanda cha nondo cha Fujian Hexingwang lndustry Tanzania Ltd vyote vikiwa vinamilikiwa na wageni, CG Mwenda amesema TRA itafanya uchunguzi wa kiwango Cha Kodi kilichokwepwa ambacho kitalipwa sambamba na Riba pamoja na adhabu.


Kamishna Mkuu Mwenda amesema walipata taarifa kutoka kwa wasamalia wema pamoja na Watumishi wa TRA kwenda kujiridhisha kuhusu kuwepo ukwepaji Kodi na alipofika amebaini kuwepo kwa hali hiyo hivyo Kodi yote ambayo haijalipwa, itapaswa kulipwa na Riba pamoja na adhabu.


“Watumishi wa TRA watakuwepo kwenye hivi Viwanda kwa mwezi mmoja kufanya uchambuzi na ufuatiliaji ili kupata thamani halisi ya Kodi ambayo inapaswa kulipwa” amesema Mwenda huku akiwapongeza wamiliki wa Viwanda kwa kufanya Uwekezaji mkubwa na kuwaajiri Watanzania.


Hata hivyo Kamishna Mkuu Mwenda amewaonya wote wenye tabia ya kukwepa Kodi kujisalimisha maana ukwepaji wa Kodi una athari kubwa na mwisho wa siku ni lazima ilipwe, hivyo amesema Kukwepa Kodi kwa sasa ni kuchelewesha kuilipa tu.

 

0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio