JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Top Stories. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Top Stories. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 21 Juni 2025

MADEREVA WAJA NA "TUNAKWENDA NA SAMIA 2025"

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Patrobas Katambi akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam  Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Patrobas Katambi akikabidhiwa Tuzo ya Rais Samia Suluhu Hassan kutoka Kwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Madereva wa masafa marefu na ya kati Tanzania Hassan Dede katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es salaam Albert Msando akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam  Mwenyekiti wa Taasisi ya Madereva wa masafa marefu na ya kati Tanzania Hassan Dede akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam  Mrakibu wa Polisi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Tanzania -Mussa Manyama akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam  Mr Chuki Shaban,Mwenyekiti wa wamiliki wa Malori (TAMSTOA) akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam.(PICHA ZOTE NA MUSSA KHALID)

Baadhi ya Madereva walioshiriki katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam 

.....................

NA MUSSA KHALID 
Serikali imeendelea kuwasisitiza madereva wa masafa marefu nchini  kudumisha amani ulinzi na usalama wa vyombo, ikiwemo kutiii Sheria na taratibu za kimamlaka na usimamizi ili kuonyesha uzalendo kwa Taifa.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Patrobas Katambi ametoa wito huo leo wakati akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam yenye kauli mbiu isemayo "madereva tunakwenda na Samia 2025".

Aidha Naibu Waziri Katambi amewapongeza madereva hao kwa kuandaa kongamano hilo lenye dhamira ya kuipongeza serikali katika kazi kubwa iliyofanywa nchini.
Katika hatua nyingine Naibu Waziri Katambi amesema kuwa serikali inaendelea kusisitiza utoaji wa mikataba kwa madereva ili kuonyesha makubaliano kati ya mmiliki wa chombo na madereva.

"Ni muhimu sana kutoa mikataba kwa sababu inaonyesha haki ya wajibu kwa Mmiliki wa chombo na Dereva lakini usalama wa chombo ni kupitia mkataba"amesema Naibu Waziri Katambi

Awali akizungumza Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Albert Msando amesema kuwa watahakikisha wanaendeleza ushirikiano na madereva wote wanaofanya shughuli zao kwani Ubungo imekuwa ni lango la kwenda katika maeneo mbalimbali nchini 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Madereva wa masafa marefu na ya kati Tanzania Hassan Dede ametumia fursa hiyo kusema madereva wanakiu kubwa kuona mambo yanabadilika.

Naye Mrakibu wa Polisi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Tanzania -Mussa Manyama amesema wao kama wasimamizi wa sheria wanawakumbusha madereva kuendelea kutii Sheria za usalama barabarani ili kuepukana na ajali.
Amewataka kuondoka na kuendesha magari Kwa mwendo wa masi kwani imekuwa ni chanzo kikubwa cha ajali barabarani
Mr. Chuki Shaban ni Mwenyekiti wa wamiliki wa Malori (TAMSTOA) amesema ni vyema wamiliki wote wa Malori kuingia kwenye Vyama ili kuweza kutambulika Kwa haraka.

NAIBU WAZIRI -UTUMISHI ATEMBELEA BANDA LA NCC

Naibu Waziri Deus Sangu wa UTUMISHI akionesha kitu katika moja ya machapisho ya NCC ambapo alishauri ifanyike kazi ya ziada kuhakikisha taarifa za NCC zinaifikia jamii yote ya Watanzania na si wakandarasi pekee au wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi tu.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mhe. Deus Sangu, akisikiliza maelezo ya NCC baada ya kutia sahihi kwenye kitabu cha wageni cha taasisi hiyo.

...............

Naibu Waziri-UTUMISHI atembelea banda la NCC

• Aipongeza kwa mchango wake katika kukuza sekta ya ujenzi

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu, ametembelea banda la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) na kuelezwa masuala mbalimbali yanayohusu Baraza hilo.

Mhe. Sangu ameelezwa majukumu yanayotekelezwa na NCC, huduma zinazotolewa na Baraza hilo, pamoja na mafanikio yanayoendelea kupatikana kwa kutolewa huduma hizo, ambapo alipongeza jitihada zinazofanywa na kusema kuwa ofisi yake itatoa ushirikiano, pindi itakapohitajika kutoa msaada wa kiutumishi.

Akizungumza baada ya kusikia maelezo hayo, Mhe. Naibu Waziri alisema, NCC ina umuhimu mkubwa kwa taifa, kutokana na majukumu inayoyatekeleza, ikiwemo kuratibu usuluhishi wa migogoro inayohusu sekta ya ujenzi, pamoja na kutoa elimu ya mbinu mbadala za kutatua migogoro kwa wadau wa sekta hiyo na nyingine.

“Awali palikuwa na migogoro mingi katika sekta ya ujenzi nchini, lakini sasa inazidi kupungua...

 Tunaamini NCC ina mchango mkubwa katika kuipunguza kwa namna yoyote ile inayofanya ikiwemo kutoa mafunzo ya usuluhishi tofauti na mahakama. Tunatambua hili na tunapongeza jitihada hizi,”Naibu Waziri Sangu amesema. 

Ameongeza kuwa, uwepo wa NCC umeleta uwiano wa mambo mengi katika sekta ya ujenzi nchini.

Aidha, kuhusu ushiriki wa NCC kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma Naibu Waziri Sangu ameitaka taasisi hiyo izidishe ushiriki wake kwenye matukio mengi zaidi, kama ilivyo shikiri kwenye Wiki ya Utumishi wa umma. Amesema lengo ni kuhakikisha Watanzania wanaifahamu vizuri zaidi taasisi hiyo, hivyo kuitumia.

Amesema, majukumu ya NCC ni makubwa na ya msingi yanayopaswa kutangazwa zaidi, ili yajulikane kwa jamii yote na wala si kwa makandarasi au wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi pekee.

“Tumefurahia maandalizi ya banda lenu na ushiriki wenu katika wiki hii muhimu. NCC imeonesha utayari wa kuhudumia wananchi hivyo, Ofisi ya Rais-UTUMISHI inaahidi kuwaunga mkono,” 

Banda la NCC limetembelewa na viongozi mbalimbali kwa siku tofauti, akiwemo Naibu Waziri huyo, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais (UTUMISHI) Bw.Juma Mkomi, pamoja na Mkurugenzi wa ofisi hiyo, Bw. Benard Makhanda, Mkurugenzi Msaidizi wa UTUMISHI, Bw. Jafari Maganga na wengine wenye nyadhifa tofauti, walioambatana nao.

Alhamisi, 19 Juni 2025

RAIS DKT. SAMIA AMEDHAMIRIA KUIENDELEZA SEKTA YA MADINI-MAJALIWA

...................

 

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa uzinduzi wa kiwanda cha kwanza cha kisasa cha kuchenjua shaba ni ishara ya dhamira ya dhati ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuisimamia na kuendeleza sekta ya madini.

 

Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa kiwanda hicho chenye uwezo wa kuchenjua tani 31,200 za mashapo ya shaba kwa mwezi kitaleta manufaa kwa Wana-chunya na Taifa kwa ujumla.

 

Amesema hayo jana (Jumatano Juni 18, 2025) alipomuwakilisha Rais Dkt. Samia katika uzinduzi wa kiwanda cha Mineral Access Systems Tanzania Ltd (MAST), kilichopo katika kata ya Mbugani, Chunya mkoani Mbeya.

 

“Uthubutu na ubunifu wa Rais wetu Dkt. Samia ndio uliochagiza kwa kiasi kikubwa maendeleo katika Sekta ya Madini, wawekezaji hawa wamekuja kwasababu ya mazingira mazuri ya uwekezaji”.

 

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa Wizara ya Madini na Taasisi mbalimbali nchini ziendelee kusimamia wawekezaji ili wanapofanya shughuli zao wazingatie Sheria, Kanuni na Taratibu za nchi ikiwemo kulipa kodi stahiki, kutunza mazingira katika maeneo wanapofanya shughuli zao. “Hakikisheni pia wanzingatia Usalama wa wafanyakazi na raia wanaozunguka maeneo ya uwekezaji”.

 

“Ninyi pia wamiliki wa viwanda na wawekezaji wote hakikisheni mnaendesha shughuli zenu kwa kuzingatia matakwa ya sheria na hasa kwenye utunzaji wa mazingira mkishirikiana na halmashauri wenyeji, kijiji na Wilaya”.

 

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wawekezaji kuweka kipaumbele cha ajira kwa wakazi wanaozunguka maeneo ya uwekezaji ikiwemo za kitaalamu na hata ambazo sio za kitaalamu.

 

 “Ametuambia mkurugenzi mtendaji ameanza na vijana takribani 200 lakini wapo pia ambao wanakuja kila siku na tunaamini atapanua wigo kuajiri, tunataka kuona vijana wa Chunya wakifanya kazi hapa”.

 

Naye, Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa amesema kuwa ujenzi wa kiwanda hicho ni sehemu ya utekelezaji wa sera na sheria ya madini inayotaka kuhakikisha madini ya Tanzania yanachimbwa, yanachakatwa na yanaongezwa hapa hapa nchini kabla ya kuuzwa nje ili kupanua wigo wa fursa za kiuchumi.

 

Ameongeza kuwa kiwanda cha MAST ni moja kati ya viwanda tisa vilivyowekwa kwenye mpango wa kujengwa kwa ajili ya kuongeza thamani ya madini kabla ya kuuzwa nje. “Kiwanda hiki bado hawajafikia hatua ya kutengeneza bidhaa za mwisho lakini ndio mpango wao, watatengeneza mpaka chuma za kutengenezea waya za umeme na nyama zilizopo kwenye magari”.

 

Juhudi hizi ni sehemu ya mpango wa taifa wa kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uchakataji wa madini barani Afrika, na kuongeza uwezo wa kuuza bidhaa zilizoongezwa thamani badala ya malighafi.

 

Kwa upande wake Rais na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya MAST Dkt. Glendon Archer amesema kuwa ujenzi wa kiwanda hicho ni mwanzo wa uchimbaji n uendelezaji wa sekta ya madini nchini Tanzania na kwamba kampuni hiyo inampango wa kujenga viwanda vingine Dodoma na Arusha.

 

“Tutaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania, Viongozi wa Serikali wametupa ushirikiano mkubwa sana na ndio maana tumefika hapa leo”.

 

Kiwanda hicho ni matokeo ya uwekezaji wa zaidi ya dola za marekani milioni 10.

 

(Mwisho)

 

Jumanne, 17 Juni 2025

SIMBACHAWENE AIPA TANO MALIASILI

 .................

Na Sixmund Begashe - Dodoma

Wizara ya Maliasili na Utalii imepongezwa kwa kazi kubwa ya Uhifadhi wa Maliasili nchini na kukuza Utalii hali inayochangia kwa kiasi kukubwa kwenye pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Pongezi hizo zimetolewa na Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mbunge), Jijini Dodoma, alipotembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kwenye maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali Park.

Mhe. Simbachawene amesema kazi inayofanywa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii inapaswa kuungwa mkono na kila mmoja ili urithi adhimu wa Maliasili nchini uendele kunufaisha kizazi kilichopo na kinachokuja.

Aidha licha ya kuipongeza Wizara hiyo kwa ushiriki katika maonesho hayo makubwa, Mhe. Simbachawene, amewasisitiza watumishi hao kuhakikisha wanaitumia vyema wiki ya maonesho hayo katika kuwahudumia wananchi watakaotembelea banda hilo.

Naye Mwenyekiti wa Maonesho ya Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Nassoro Wawa, ametoa wito kwa wananchi kutembelea banda hilo ili kujipatia huduma mbalimbali zinazotolewa na Wizara kupitia Idara na Taasisi zake katika kipindi chote cha maonesho hayo.

Jumatatu, 16 Juni 2025

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA


........................

📌 Wizara ya Nishati na TAMISEMI zaendelea kushirikiana kuhakikisha  Shule mpya zinafungwa mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema gharama ya kujaza gesi kwenye mitungi (LPG) ni himilivu ikiwa ni jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ili kuwezesha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Juni 16, 2025 katika ziara ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Simiyu  wakati wa kuzindua Shule Maalum ya Sayansi ya Wasichana ya Simiyu ambayo imefungwa miundombinu ya nishati safi ya kupikia. 

“Mheshimiwa Rais ulituelekeza Taasisi ambazo zinahudumia watu zaidi ya mia moja tuzifungie miundombinu ya nishati safi ya kupikia, Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na TAMISEMI tunatekeleza agizo hilo kwa kuzifungia mifumo ya nishati safi shule mpya ambazo zinajengwa." Amesema Kapinga

Ameeleza kuwa,  uwezo wa shule hiyo ni wanafunzi 800 na mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia iliyofungwa ina uwezo wa kuhudumia wanafunzi 800.

Ameongeza kuwa, kwa idadi hiyo ya wanafunzi 800  mtungi wa gesi katika Shule ya Wasichana Simiyu utakuwa ukijazwa kila  baada ya miezi miwili.


Listen Mkisi Radio