HUDUMA YA MAJI DAR NA PWANI YAENDELEA KUIMARIKA

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu DAWASA, Mhandisi Mkama Bwire akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo Machi 7,2025
..............

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imesema hali ya upatikanaji huduma ndani ya eneo lake la kihuduma katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani ipo vizur na inaendelea kuimarika kupitia vyanzo vya uzalishaji wa maji vya Ruvu Juu na Ruvu Chini.


Akiongea na Waandishi wa Habari, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu DAWASA, Mhandisi Mkama Bwire Amesema kuwa vyanzo vya uzalishaji maji katika mitambo ya Ruvu Juu na Ruvu Chini inapokea maji ya kutosha na hali ya maji katika Mtoni Ruvu iko katika hali nzuri ya uzalishaji ukiacha changamoto ndogo iliyojitokeza katika Mtambo wa Uzalishaji Maji wa Ruvu Juu ambayo imeshatatuliwa na uzalishaji unaendelea vizuri.

Mhandisi Bwire ameongeza kuwa kazi inayoendelea kwa sasa ni kuhakikisha Maji yanayozalishwa yanasukumwa nakusambaza kwa Wananchi.

"Mamlaka inaendelea na taratibu za manunuzi ya Pampu mpya 12 za kufunga kwenye Mitambo ya uzalishaji maji ili kuboresha na kuongeza kiwango cha uzalishaji maji ili kuhudumia wananchi wengi zaidi," amesema Mhandisi Bwire

Amebainisha kuwa kwa maeneo yaliyokuwa na changamoto ya huduma ikiwemo Kinyerezi, Makabe, Mshikamano na Machimbo kazi ya usambazaji maji kwa sasa inaendelea vizuri na huduma inaendelea kuimarika.

mussa khalidi

I am ,Journalist, Presenter Radio & TV, Producer, Video editor, Graphics Designer, Layout Newspaper designer,Contact: +255 659 669 902 Email: mussakhalid70@yahoo.com or muxabhai200@gmail.com

Post a Comment

Previous Post Next Post