JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Top Stories. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Top Stories. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 10 Julai 2025

WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA NISHATI SAFI


Charles Barnabas Kiongozi wa Ubia na Uhusiani wa Mradi wa masuala ya Nishati wa Services Modern Energy Cooking ambao unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (UKAD) kupitia ubalozi wa Uingereza Tanzania aki akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es salaam leo tar 10 July 2025.

Mwakilishi wa Kampuni inayojishughulisha na matumizi ya nishati safi majiko ya kutumia umeme SESCOM Shabani Selemani  akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es salaam leo tar 10 July 2025

...................

NA MUSSA KHALID

Watanzania wametakiwa kuepukana na matumizi ya kuni na mkaa badala yake watumie nishati safi ili kuendana na adhma ya serikali ya awamu ya sita ya mapambano ya mabadiliko ya tabia nchi.   

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na Charles Barnabas Kiongozi wa Ubia na Uhusiani wa Mradi wa masuala ya Nishati wa Services Modern Energy Cooking ambao unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (UKAD) kupitia ubalozi wa Uingereza Tanzania wakati wakifanya mradi wa Pikasmati katika eneo la Mwenge.

Amesema kuwa wanafanya kampeni ya mradi wa Pikasmati lengo lake ni kuongeza uelewa kwa wananchi kutumia matumizi ya nishati safi kwa kupika kwa umeme ili kuendana na dhamira ya serikali ya matumizi ya nishati safi.

“Tunawapa elimu wananchi watambue kwamba kupika kwa umeme sio gharama kubwa kwani kuna majiko ambayo ni fanisi kwa ajili ya matumizi hayo na elimu hii ndio imekuwa ikifanya watu waweze kutambua matumizi sahihi ya nishati safi ya kupikia’amesema Charles

Kwa upande wake Mwakilishi wa Kampuni inayojishughulisha na matumizi ya nishati safi majiko ya kutumia umeme SESCOM Shabani Selemani amesema matumizi yake yanasaidia kuonda  gharama na kupunguza uharibifu wa mazingira.

Nao baadhi ya wananchi Anamery George kutoka Kigamboni Twangoma na Oliver  John Mkazi wa Ubungo wameelezea umuhimu wa matumizi ya  nishati safi ya kupikia inasaidia katika utunzaji wa mazingira lakini pia inatunza muda sambamba na kuokoa gharama.

 Imeelezwa kuwa Kampeni hiyo ya Pikasmati ni ya Kitaifa ambayo inajumuisha maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Zanzibar ambapo itafanyika mpaka mwezi wa 12 mwaka huu ili watanzania wafahamu kuwa kupikia kwa umeme ni nafuu.

 

TFRA YAANZISHA MAABARA YA UPIMAJI WA UDONGO NA UBORA WA MBOLEA

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibi wa Mbolea Tanzania –(TFRA) Joel Laurent  akimsikiliza Afisa Udhibiti ubora Mwandamizi kutoka katika Mamlaka hiyo  Azizi Mtambo alipotembelea banda la Mamlaka hiyo katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya biashara 'Sabasaba' yanayoendelea jijini Dar es salaam leo tar 10/7/2025.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibi wa Mbolea Tanzania –(TFRA) Joel Laurent (kushoto) akimsikiliza Meneja wa Uhusiano, Mawasiliano na Elimu kwa Umma wa TFRA, Bi. Matilda Kasanga (kulia) alipotembelea banda la Mamlaka hiyo katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya biashara 'Sabasaba' yanayoendelea jijini Dar es salaam leo tar 10/7/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibi wa Mbolea Tanzania –(TFRA) Joel Laurent akimsikiliza Afisa kutoka TARI alipotembelea Banda la Taasisi hiyo katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya biashara 'Sabasaba' yanayoendelea jijini Dar es salaam leo tar 10/7/2025

.............................

NA MUSSA KHALID

Mamlaka ya Udhibi wa Mbolea Tanzania –TFRA imewasisitiza watanzania kutumia fursa ya uwepo wa maabara ya kisasa iliyoanzishwa na Mamlaka hiyo ili kujua afya ya udongo na ubora wa mbolea kuwa katika kiwango sahihi.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA Joel Laurent wakati alipotembelea banda la Mamlaka hiyo katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya biashara 'Sabasaba' yanayoendelea jijini Dar es salaam ambapo amesema ni vyema wakaondoa wasiwasi kwani maabara hiyo inakwenda kuwasaidia katika shughuli zao za kilimo

Mkurugenzi huyo amesema kuwa lengo lao ni kuonyesha fursa zilizopo katika mnyororo wa thamani katika mbolea lakini pia kuwaelimisha watanzani namna ya kutumia matumizi sahihi ya mbolea.

Amesema mpaka kufika mwaka 2030 matumizi ya mbolea yatakuwa mara mbili ya kiwango cha sasa hivyo wameendelea kuyashawishi makampuni mbalimbali yaweze kuzalisha.

‘Mipango yetu ni kuendelea kuwa na mbolea sahihi kwa matumizi sahihi kwa wakulima wetu ambapo inatokana na wizara ya Kilimo kuendelea kupima afya ya udongo nchi nzima hivyo tunahitaji wenzetu wanaozalisha waweze kuagiza mbole ambazo zinaendana na afya ya udongo ili kuongeza tija’amesema Laurent

Aidha Laurent amesema kuwa Mamlaka hiyo imeanzisha mfumo wa kielekroniki ili wakulima waweze kujisajili jambo litakalosaidia wapate manufaa ya mbolea kwa bei himilivu.

Mkurugenzi huyo wa TFRA pia amesema kwa mwaka huu wameandaa mpango maalum wa kuongeza  uzalishaji wa mbolea kwa viwanda vya ndani kwa ajili ya wakulima ili ziweze kupatikana mapema,kwa urahisi na bei nafuu zaidi.

      

Jumatano, 9 Julai 2025

RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE ASHIRIKI MKUTANO WA JARIDA LA UONGOZI LA AFRIKA

Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ameshiriki katika Mkutano Mkuu wa Afrika ulioandaliwa na Jarida la Uongozi la Afrika (African Leadership Magazine) na Taasisi ya Uongozi wa Afrika (African Leadership Organization) jijini London, Uingereza. 

Mkutano huo unazungumzia masuala mbalimbali ya Afrika, ikiwemo Uongozi, Uwekezaji na Ushindani wa Kimaendeleo kwa kauli mbiu ya: “Powering Leadership, Investment and Competitiveness”.

Awali, Mheshimiwa Rais Mstaafu ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Washauri ya African Leadership Organization (ALO), aliongoza vikao vya Bodi hiyo ambayo inaangazia masuala mbalimbali ya maendeleo ya Afrika kijamanii na kiuchumi. 

Bodi hiyo ina wajumbe kutoka nchi mbalimbali duniani, akiwemo Mhe. Dkt. Jewel Howard Taylor, Makamu wa Rais Mstaafu wa Liberia; Prof. Tahir Akhtar, Mkurugenzi wa Kampuni ya Adam Global Holdings UK/UAE; Dkt. Victor Oladukon, kutoka Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB); Dkt. Christian Lindfeld, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Africa Ventures Advisory - Germany; Jenerali William Kip Ward, Kamanda Mkuu Mstaafu wa Kamandi ya Jeshi la Marekani barani Afrika; Mhe. Nomvula Makonyane, Makamu Katibu Mkuu wa ANC - Afrika Kusini; na Dkt. Ken Giami, Mtendaji Mkuu wa African Leadership Organization (ALO). 

MAITI YA BINADAMU YATUMIKA KATIKA USAFIRISHAJI WA DAWA ZA KULEVYA

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini –DCEA akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo Julai 9,2025
......................

NA MUSSA KHALID

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini –DCEA inandelea kuwadhibiti baadhi ya wahalifu wa Dawa za kulevya ambao wameanza kutumia maiti za Binadamu kubeba dawa hizo maarufu kwa jina la begi ili kukosemsha uhalifu huo.

Kamishna Jenerali wa Mamlaka hiyo Aretas Lyimo amebainisha hayo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wanahabari akitoa taarifa ya operesheni waliyoifanya kwa kipindi cha mwezi Mei hadi Julai mwaka huu.

Kamishna Jenerali Lyimo amesema wamebaini kumekuwa na matukio ya raia wa kigeni kuwatumia watanzania kusafirisha na kusambaza dawa za kulevya kwa kutumia njia hizo hivyo amewasisitiza wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari wanapotumwa au kupokea mizigo.

‘Mara niyingi huanzisha mahusiano ya kirafiki na kisha kuwahusisha katika biashara hii haramu kwa kutumia kampuni zao na vyombo vyao vya usafiri hususani bodaboda,bajaji,Tax na wasambazaji wa vifurushi’amesema Kamisha Lyimo

Aidha Kamishna Jenerali Lyimo amesema katika operesheni hizo pia wamekamata dawa za kulevya jumla ya Kilogram 37,197.142 na watuhumiwa 64 waliohusishwa na dawa hizo.

Amesema kuwa Dawa hizo zinajumuisha kilogram 11,031.42 za dawa mpya za kulevya aina ya Mitragyna Speciosa,bangi kilogram 24,873.56,mirungi kg 1,274.47,skanka kg 13.42,heroin kg 2.21 na methamphetamine gramu 1.42.

Ameendelea kueleza kuwa katia ukamataji huo umehusisha dawa tiba zenye asili ya kulevya aina ya ketamine kilogramu 1.92,Fluni-trazepam vidonge 1000,lita 6 za kemikali bashirifu aina ya hydrochloric acid na uteketezaji wa ekari 1,045.5 za mashamba ya bangi.

Kamishna Lyimo amesema katika mkoa wa Dar es salaam eneo la Sinza waliwakamata watu wawili wamiliki wa kiwanda bubu kinachotengeneza biskuti zinazochanganywa na bangi kisha kuzisambaza katika mikoa ya Dar es salaam,Mwanza,Lindi na Mtwara amba pia wakati huohuo mkoani Lindi alikamatwa mfanyabiashara wa madini akisambamba biskuti zilizochanganywa na bangi.

‘Vilevile kwa upande wa dawa za kulevya za mashambani zilikamatwa jumla ya Kilogram 26,191.45 za bangi,mirungi,skanka na kuteketeza akari 1,045.5 za mashamba ya bangi katika mikoa ya Ruvuma,Mbeya,Mara,Kagera,Dodoma,Tabora,Morogoro na Arusha. 

Hata hivyo Mamlaka hiyo imetoa tahadhari kwa mtu yeyote atakayeendelea kujihudisha na biashara,usambazaji na uzalishaji wa Dawa za Kulevya kuwa watachukuliwa hatua kali za kisheria pindi atakapobainika.

Jumanne, 8 Julai 2025

TANZANIA KOREA KUFANYA MRADI WA UPANUZI WA MFUMO WA GOTHOMIS

lNa Angela Msimbira, Seoul, Korea 

Serikali ya Korea Kusini kupitia shirika la KOICA imeandaa Mkutano wa Kimataifa kubadilishana uzoefu kwenye kuboresha mifumo ya usimamizi wa huduma za afya kwa kutumia teknolojia ya kisasa. 

Mkutano huu umehusisha watalaam kutoka Tanzania na Korea ikiwa ni sehemu ya ushirikiano wa Mradi wa Kupanua matumizi ya Mfumo wa GOTHOMIS unaotelekelezwa Mkoani Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya ujumbe wa Tanzania, Mkurugenzi Msaidizi - (Huduma za Lishe) Bw. Lutifrid Nnally, amesema ushiriki wa Tanzania unalenga kujifunza uzoefu wa Korea kwenye matumizi ya mifumo ya kidijitali katika huduma za afya.

Tanzania inatarajia kutumia uzoefu huo kufanya maboresho ya GOTHOMIS, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa, na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa kutumia teknolojia kama telemedicine, akili bandia (AI) na mifumo ya taarifa za kiafya.

Ushiriki huu ni hatua muhimu katika mageuzi ya sekta ya afya, hasa kwa maeneo ya vijijini, ili kuhakikisha huduma bora, za haraka na kwa gharama nafuu zinawafikia wananchi wote 

RAIS SAMIA APOKEA TUZO YA POWER OF 100 WOMEN AWARD KUTOKA ACCESS BANK GROUP

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Tuzo Maalum ya ‘Power of 100 Women Award mara baada ya kukabidhiwa Ikulu Jijini Dar es Salaam 08 Julai, 2025.

ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Access Tanzania Ndugu Protase Ishengoma pamoja na ujumbe aliombatana nao Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Julai, 2025.

Jumatatu, 7 Julai 2025

BALOZI HAMAD AKUTANA NA RAIS WA BUNGE LA MSUMBIJI

 Mhe. Balozi Hamad Khamis Hamad amekutana na Mhe. Margarida Adamugu Talapa, Rais wa Bunge la Jamhuri ya Msumbiji kwenye Ofisi za Bunge hilo Leo Jijini Maputo   Julai 07, 2025;

Wakati wa mkutano huo, Mhe. Talapa alimpongeza Mhe. Balozi Hamad kwa kuteuliwa kuiwakilisha Tanzania nchini Msumbiji na kumhakikishia kila aina ya ushirikiano katika kutekeleza majukumu yake. Aidha, alieleza kutambua ushirikiano na msaada wa Tanzania tokea wakati wa mapambano ya kutafuta Uhuru wa Msumbiji na jitihada zinazoendelea za kutafuta amani Kaskazini mwa Msumbiji.

Kwa upande wake, Mhe. Balozi Hamad alimshukuru Mhe. Talapa kwa kukubali kukutana naye na alimhakikishia kila aina ya ushirikiano kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kidugu na historia baina ya Tanzania na Msumbiji. Aidha, alishauri kuhusu umuhimu wa Mabunge ya nchi hizi mbili kuendeleza ushirikiano hasa baada ya Tanzania kumaliza Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba, 2025.

Mwisho, alieleza kwamba Tanzania itaendelea kushirikiana Serikali na Wananchi wa Msumbiji katika maeneo mbalimbali hususan utunzaji wa amani Kaskazini mwa nchi hiyo ambapo Majeshi ya Tanzania yanaendelea kusaidia kwenye mapambano dhidi ya vikundi vya kigaidi.

Imetolewa na Ubalozi wa Tanzania - Maputo. 

LUHEMEJA AWATAKA WATANZANIA KUTOA UZITO NA MSISITIZO UHIFADHI NA USIMAMIZI WA MAZINGIRA


..............

WATANZANIA wamehimizwa kulipa uzito na msisitizo suala la uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini kwani ni agenda muhimu ya kimaendeleo kwa binadamu.

Hayo yamesemwa leo Jumapili (Julai 6, 2025) Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja wakati akizindua Siku ya Mazingira iliyoadhimishwa katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF).

Luhemeja amesema  Dunia inakabiliwa na changamoto za kimazingira zikiwemo ukataji miti, upotevu wa viumbehai, kupanda kwa joto, hivyo jitihada za pamoja baina ya Serikali, Asasi zisizo za Serikali, sekta binafsi na wananchi zinahitajika katika kukabiliana na hali hiyo.

”Natoa rai kwa Watanzania kudumisha utamaduni wa kutunza mazingira kwa kuepuka kutupa taka na kukata miti hovyo. Aidha, tuendeleze utamaduni wa kupanda miti na kupunguza matumizi ya kuni na mkaa kwa kutumia nishati safi ya kupikia” amesema Mhandisi Luhemeja.

Ameongeza kuwa Tanzania imebarikiwa urithi mkubwa wa rasilimali asilia na vivutio vya kipekee vinavyotambulika kitaifa na kimataifa ikiwemo misitu, ukanda wa bahari, uchumi wa bahari, eneo la misitu ya mikoko, hivyo endapo mazingira yataendelea kuharibiwa rasilimali hizo hazitakuwa salama.

Mhandisi Luhemeja awataka wananchi na  wadau kupunguza matumizi ya plastiki kwa kutumia falsafa ya ”Punguza, Tumia Tena na Rejeleza” ambapo kwa mujibu wa tafiti zimebainisha kuwa taka za plastiki huchukua miaka 400 mpaka 1,000 kuoza ardhini na hivyo kuleta athari hasi kwa afya ya binadamu, mazingira na uchumi.

Ameeleza kuwa katika kukabiliana na changamoto za mazingira,  Serikali kwa kushirikiana na wadau imefanya jitihada mbalimbali  ikiwa ni pamoja na kuandaa na kutekeleza Sera ya Taifa ya Mazingira, Mkakati wa Taifa wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mchango wa Taifa wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Maafa.

Ameeleza kuwa zaidi ya asilimia 90 ya kaya nchini bado zinaendelea kutegemea kuni na mkaa kama chanzo kikuu cha nishati ya kupikia, hivyo Serikali imezindua Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034) unaolenga kuhakikisha kuwa asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.

“Mkakati huu unaonesha dhamira ya kweli ya kumkomboa Mtanzania dhidi ya athari za nishati chafu, hasa wanawake ambao ndio wahanga wakubwa. Hili si suala la majiko au mafuta tu, bali linagusa afya, heshima, fursa na haki ya kuishi katika mazingira bora” amesema Mhandisi Luhemeja.

Awali Mkurugenzi wa Usimamizi wa Biashara wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), Bi. Lulu Mkudde amesema tukio la uzinduzi wa Siku ya Mazingira ni la kwanza kufanyika tangu shughuli na huduma za maenesho hayo kuanza nchini.

Amesema kuwa TANTRADE itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais katika masuala ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini hususani kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia na upandaji miti.

“Tunatambua suala la uhifadhi wa mazingira kwa sasa limekuwa ni fursa ikiwemo biashara ya kaboni ambayo imeendelea kunufaisha jamii ya Watanzania. Tutaendelea kuunga mkono juhudi hizi kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya jamii yetu” amesema Mkudde.

MWISHO

  

MAADHIMISHO YA SIKU YA KISWAHILI DUNIANI YAFANYIKA OSAKA JAPAN

Matukio mbalimbali katika picha wakati wa maadhimisho ya kilele cha siku ya Kiswahili duniani, tarehe 7, Julai, 2025. Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika eneo la Yumeshima; jijini Osaka, nchini Japan, yamekuwa sehemu ya maonesho ya biashara ya dunia (Expo 2025, Japan) yanaondelea nchini Japan.

Ikumbukwe kuwa maadhimisho ya siku ya Kiswahili kikanda (Afrika Mashariki) yanafanyika nchini Rwanda na kwa Tanzania, maadhimisho hayo yanafany9ika visiwani Zanzibar.  

Listen Mkisi Radio