JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Top Stories. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Top Stories. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 2 Julai 2025

REA YASAMBAZA MITUNGI, MAJIKO YA GESI KWA WATUMISHI 461 WA MAGEREZA MKOA WA MARA


Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa mitungi hiyo iliyoanza kugaiwa katika Gereza la Wilaya Musoma leo Julai 02, 2025, Mjumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Lucas Malunde amesema kuwa mradi huo umelenga kuwafikia watumishi wa magereza 15,126 wote nchini.

Amesema kuwa, Wakala wa Nishati Vijijini uliingia makubaliano na Jeshi la Magereza Septemba 13, 2024 uliolenga kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa Magereza yote nchini.

Mkataba huo wenye gharama ya Shilingi Bilioni 35.23 umelenga kuwezesha ujenzi wa miundombinu ya gesi asilia, ujenzi wa miundombinu ya biogas, ujenzi wa miundombinu LPG, usambazaji wa mitungi ya gesi pamoja na majiko ya sahani mbili kwa watumishi wa magereza, usambazaji wa mkaa mbadala, ununuzi wa mashine za kutengenezea mkaa mbadala na kuwajengea uwezo watumishi wa magereza kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia.

“Serikali kupitia REA imeweza kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya nishati safi ya kupikia na sasa Magereza yote Tanzania Bara yanatumia nishati safi ya kupikia. Hii ni hatua kubwa sana katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Na leo tunaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kugawa bila gharama yoyote mitungi hii ya Kilogramu 15 na majiko ya sahani mbili kwa watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara. Mkawe mabalozi wazuri wa nishati safi ya kupikia,” amesema Mjumbe huyo wa Bodi.

Awali, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mara, ACP. Hospitius Mendi amesema kuwa tangu kuanza kutumia nishati safi ya kupikia, Magereza wameokoa muda waliokuwa wanatumia kutafuta kuni pamoja na gharama za kusafirisha kuni.

Kwa upande wake Kaimu Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Wawekezaji Miradi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Emmanuel Yesaya ametoa rai kwa watumishi wa jeshi la magereza wote nchini kutunza miundombinu ya nishati safi ya kupikia iliyofungwa katika magereza pamoja na kuwa mabalozi wa nishati safi ya kupikia.

ETDCO YAONYESHA UTEKELEZAJI WA MRADI YA UMEME SABASABA

Mhandisi Mkuu wa Kampuni ya Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO) Mustapha Himba (kulia) akitoa ufafanuzi wa utekelezaji wa miradi ya umeme kwa wananachi waliotembelea leo julai 2, 2025 katika banda la Kampuni hiyo katika  Maonesho  ya 49 ya Kimataifa ya Biashara sabasaba  katika Viwanja vya  Julius Nyerere, Dar es Salaam Afisa Uhusiano wa Kampuni ya ETDCO Bi. Samia Chande (kulia) akitoa maelezo ya utekelezaji wa miradi ya umeme kwa mwananachi aliyetembelea leo julai 2, 2025 katika banda la Kampuni hiyo katika  Maonesho  ya 49 ya Kimataifa ya Biashara sabasaba  katika Viwanja vya  Julius Nyerere, Dar es Salaam .

Wafanyakazi wa Kampuni ya ETDCO wakiwa katika picha ya pamoja kwenye banda la kampuni hiyo,  maonesho ya sabasaba.

..........

Wananchi wamehimizwa kutembelea banda la Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO), katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba, ili kuona namna Serikali ilivyowekeza katika kuboresha miundombinu ya umeme kwa lengo la kuhakikisha Watanzania wanapata umeme wa uhakika kwa maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza leo Julai 2, 2025, jijini Dar es Salaam katika Viwanja vya Maonesho ya Julius Nyerere, Mhandisi Mkuu wa Kampuni ya ETDCO, Mustapha Himba, amesema kuwa katika utekelezaji wa miradi ya umeme nchini, wamefanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati kwa mafanikio makubwa, hali ambayo imeleta tija kwa jamii.

Mhandisi Himba amesema kuwa mojawapo ya miradi waliyotekeleza ni mradi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Mtwara hadi Maumbika yenye kilovolti 132, ikiwa na urefu wa kilomita 80, pamoja na mradi mwingine kutoka Tabora hadi Urambo wenye kilovolti 132 na urefu wa kilometa 115.

Aidha, ameeleza kuwa kuna mradi mwingine wa kutoka Tabora hadi Katavi wenye kilovolti 132, ambao umewezesha wananchi wa mkoa huo kupata huduma ya umeme wa uhakika.

"Tunawakaribisha wananchi wote kutembelea banda letu la ETDCO lililopo ndani ya banda la TANESCO. Lengo ni kuwaonesha wadau namna kampuni yetu inavyotekeleza majukumu yake kwa weledi mkubwa ili kuisaidia Serikali katika kuboresha huduma ya umeme," amesema Mhandisi Himba.

Ameongeza kuwa kampuni hiyo imefanikiwa kujenga miradi ya REA katika mikoa mbalimbali ikiwemo Mwanza, Arusha, Katavi, Mbeya, Geita, pamoja na Kigoma.

Amefafanua kuwa hadi sasa, katika utekelezaji wa miradi hiyo, wamejenga njia za usafirishaji umeme zenye kilovolti 132 kwa urefu wa kilomita 578, na usambazaji wa kilovolti 33/11 kwa urefu wa kilomita 4,483.

Aidha, wamefanya ukarabati wa miundombinu ya umeme yenye urefu wa kilomita 534, na kufanikiwa kuunganisha umeme katika vijiji 291 na vitongoji 105.

Kwa upande wao, baadhi ya wananchi waliotembelea banda la ETDCO, akiwemo Bi. Fatuma Yusuph, wameipongeza kampuni hiyo kwa kutekeleza miradi hiyo kwa wakati, huku wakitoa wito kwa Serikali kuendelea kuboresha miundombinu ya umeme ili kuchochea shughuli mbalimbali za kiuchumi.

WATUMISHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS WAHIMIZWA USHIRIKIANO NA WIZARA ZA KISEKTA

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akifungua kikao kazi cha kimkakati na Menejimenti na watumishi wa Ofisi hiyo leo Jumatano (Julai 2, 2025) jijini Dodoma kilicholenga kujadili vipaumbele vya mpango kazi wa utekelezaji wa shughuli na majukumu ya Ofisi hiyo katika mwaka 2025/2026.

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamuwa Rais, Prof. Peter Msoffe akizungumza wakati wa kikao kazi cha kimkakati na Menejimenti na watumishi wa Ofisi hiyo leo Jumatano (Julai 2, 2025) jijini Dodoma kilicholenga kujadili vipaumbele vya mpango kazi wa utekelezaji wa shughuli na majukumu ya Ofisi hiyo katika mwaka 2025/2026.

Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (NCMC) Prof. Eliakim Zahabu akiwa katika kikao kazi cha kimkakati na Menejimenti na watumishi wa Ofisi hiyo leo Jumatano (Julai 2, 2025) jijini Dodoma kilicholenga kujadili vipaumbele vya mpango kazi wa utekelezaji wa shughuli na majukumu ya Ofisi hiyo katika mwaka 2025/2026. 

Sehemu ya Watendaji wa Ofiisi ya Makamu wa Rais wakifuatilia kikao kazi cha kimkakati kilichofanyika leo Jumatano (Julai 2, 2025) jijini Dodoma kilicholenga kujadili vipaumbele vya mpango kazi wa utekelezaji wa shughuli na majukumu ya Ofisi hiyo katika mwaka 2025/2026.

...................... 

Watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais wamehimizwa kuimarisha ushirikiano na mahusiano na Wizara, Taasisi na Idara za kisekta ili kuwezesha kuimarika kwa Muungano na usimamizi endelevu wa sekta ya hifadhi ya mazingira nchini. 

Rai hiyo imetolewa leo Jumatano (Julai 2, 2025) jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Mhandisi Cyprian Luhemeja wakati akifungua kikao kazi cha kimkakati kinacholenga kujadili vipaumbele vya mpango kazi wa utekelezaji wa shughuli na majukumu ya Ofisi hiyo katika mwaka wa fedha 2025/26.

Mhandisi Luhemeja amesema kikao hicho ni mkakati maalum wa Ofisi hiyo katika kujiwekea malengo mahsusi ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na hivyo kuwashirikisha watumishi wa kutambua wajibu na majukumu waliyonayo ili kufikia malengo.

Amebainisha kuwa katika mwaka wa Fedha 2025/2026 vipaumbele vya ofisi hiyo ni kuhakikisha inapatia majibu hoja mbalimbali kuhusu masuala ya Muungano na Mazingira kupitia ushirikiano na wadau wa kimkakati ikiwemo Wizara, Taasisi na Idara za kisekta.

“Ni wajibu wetu kuhakikisha tunaimarisha uratibu na ushirikiano na Wizara, Idara na Taasisi zote za kisekta ili kuhakikisha tunatambulika vyema….kwa mfano masuala ya uchumi wa buluu kunahitajika usimamizi na uratibu wetu wa karibu ili kuweza kutekeleza kwa pamoja na wizara nyingine,” amesema Mhandisi Luhemeja.

Mhandisi Luhemaja amesema mazingira ni sekta mtambuka inayogusa wadau wote wa kimkakati zikiwemo Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Mashirika na Taasisi za umma, hivyo ofisi hiyo ina wajibu wa kusimamia uratibu wa miongozo mahsusi ya masuala ya uhifadhi wa mazingira nchini.

Amesema kuwa ili kufikia malengo ya uratibu wa masuala ya mazingira nchini, ofisi hiyo imechukua hatua mahsusi ikiwemo kuunda madawati maalum ya uratibu wa masuala ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira katika mashirika na taasisi za umma pamoja na mamlaka za serikali za mitaa nchini.

“Kuna zaidi ya mashirika na taasisi za umma 302 ambazo zina idara ya mazingira…tumeanza kushirikiana katika kuhimiza masuala ya uhifadhi wa mazingira kwa kutumia fursa zilizopo…ushirikiano huu na wadau ni muhimu katika kuchagiza agenda ya mazingira nchini” amesema Luhemeja.

Kuhusu maudhui ya mpango kazi uliondaliwa kwa mwaka 2025/26, Mhandisi Luhemeja, amesema vipaumbele na mwelekeo wake umejikita katika kuleta matokeo tarajiwa kuhusu utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo katika kufikia malengo yaliyowekwa.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Peter Msoffe amesema watendaji na watumishi wa ofisi hiyo wapo tayari katika kutekeleza maelekezo yaliyotolewa kupitia kikao hicho ili kubadilisha mfumo wa utendaji kazi wenye kuleta matokeo chanya kwa umma.

Kikao hicho cha siku 03 kitahusisha mawasilisho ya mada mbalimbali za masuala ya Muungano na Mazingira sambamba na kujadili Mpango wa tathimini na ufuatiliaji wa shughuli na majukumu ya ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26.

  

ASANTENI WANA RUANGWA -MAJALIWA

..............

WAZIRI MKUU, na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa leo Julai 2, 2025 ametangaza rasmi kutokugombea tena ubunge wa jimbo la Ruangwa baada ya kulitumikia jimbo hilo kwa miaka 15.

Akizungumza na wajumbe wa kamati ya Siasa ya Mkoa na Wilaya ya Ruangwa Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi kwa kumuunga mkono wakati wote ambao amekuwa mbunge wa jimbo hilo.

"Imefika wakati kwa mshikamano tulioujenga  sasa ni wakati wa kutoa fursa kwa Wana-Ruangwa wengine wapenda maendeleo waweze kuunganisha nguvu hizi ili Kauli mbiu yetu ya Ruangwa kwa maendeleo inawezekana iweze kusonga mbele zaidi."

Aidha, ametoa wito wajumbe wa kamati ya siasa ya Wilaya kuwapa ushirikiano wagombea wote wenye nia ya kugombea ubunge wa jimbo hilo.

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amewasihi Wana-Ruangwa kuendelea kushikamana na itakapofika siku ya uchaguzi waweze kuchagua wagombea wote watakaowakilisha chama cha Mapinduzi kwenye uchaguzi huo. 

"viongozi wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mgombea Mwenza Dkt. Nchimbi watakapokuja tujitokeze kwa wingi kwenye mikutano tusikilize sera, lakini siku ya kupiga kura tuwapigie kura nyingi za kutosha."

Aidha, amemshukuru Rais Dkt. Samia  Viongozi wakuu wa chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kumuamini na kumpa fursa ya kuwatumikia wana Ruangwa.

Mheshimwa Majaliwa alichaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Ruangwa mwaka 2010 na amehudumu kwa kipindi cha miaka 15.

Jumatatu, 30 Juni 2025

MAKAMU WA RAIS AKISHIRIKI UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA UFADHILI WA MAENDELEO NCHINI HISPANIA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na  na Viongozi mbalimbali kabla ya kuanza kwa  Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Ufadhili wa Maendeleo (FfD4) unaofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Fibes Jijini Sevilla nchini Hispania. Tarehe 30 Juni 2025.

MKINGA ACHUKUA FOMU KUOMBA UBUNGE LUDEWA

Mtia nia James Innocent Mkinga (kulia), Mtaalamu mbobezi katika Fani ya Teknojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) akichukua fomu yake kuomba kuteuliwa kugombea jimbo hilo.

 

James Innocent Mkinga, Mtaalamu mbobezi katika Fani ya Teknojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

JOTO la Siasa katika Jimbo la Uchaguzi la Ludewa limezidi kupanda kufuatia kuendelea kujitokeza kwa watia nia mbalimbali wanaoashiria kuwepo kwa mchuano mkali jimboni humo. 

Jumapili Juni 29 2025, Mtia nia James Innocent Mkinga, Mtaalamu mbobezi katika Fani ya Teknojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Kada CCM na mwana harakati wa Maendeleo ya Vijana amejitokeza kwa mara ya pili kuchukua Fomu ili kushiriki katika mchakato wa kupata nafasi ya kupeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa Mbunge wa Jimbo hilo.

BIASHARA YA KABONI NYENZO MUHIMU KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mha. Hamad Yussuf Masauni akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Juni 30, 2025 mara baada ya kupokea Taarifa ya Tathmini ya Mwenendo wa Biashara ya Kaboni kutoka kwa Kamati ya Biashara ya kaboni.

.......................

Mwandishi Wetu Dar es Salaam

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mha. Hamad Yussuf Masauni amesema Biashara ya Kaboni ni miongoni mwa nyenzo muhimu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambapo nchi, taasisi, kampuni na wananchi wanaweza kushiriki katika jitihada za Kitaifa na Kimataifa za kupunguza gesijoto duniani. 

Waziri Masauni amesema hayo jijini Dar es Salaam Juni 30, 2025 mara baada ya kupokea Taarifa ya Tathmini ya Mwenendo wa Biashara ya Kaboni kutoka kwa Kamati ambapo amesema Tanzania imeimarisha usimamizi wake kwa kuanzisha Kanuni za mwaka 2022 na marekebisho yake ya mwaka 2023, pamoja na Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).

Amesema NCMC ina jukumu la kusajili miradi, kuwezesha ufuatiliaji, uthibitishaji wa gesijoto, utoaji wa elimu na uhamasishaji wa wadau. Tangu kuanza kutumika kwa kanuni, jumla ya miradi 73 ambayo miradi 69 ipo katika hatua mbalimbali za usajili na miradi 4 ipo katika hatua ya utekelezaji.

Ameongeza kwa upande wa Zanzibar imeanza kupokea maombi ya miradi ya kaboni kufuatia kupitishwa kwa Kanuni za Udhibiti na Usimamizi wa Biashara ya Kaboni za mwaka 2025. Kufikia Mei 2025, kampuni nne (4) zilionesha nia ya kutekeleza miradi hiyo, ambapo mbili (2) kati yao zimewasilisha maandiko dhana.

“Kamati hii ilipewa jukumu la kufanya tathmini na kutoa mapendekezo ya kuongeza ufanisi wa uendeshaji wa biashara ya Kaboni nchini, lengo kuu ni kufanya tathmini ya hali ya sasa ya biashara ya kaboni nchini Tanzania na kutoa mapendekezo kwa serikali kuhusu njia bora za kuimarisha mifumo na mwenendo wa biashara ya kaboni Tanzania Bara na Zanzibar.

Amesema katika kuimarisha uelewa na ushirikishwaji wa wadau katika Biashara ya Kaboni, Serikali kwa kushirikiana na wadau imeendelea kutoa elimu kwa Umma ili kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu biiashara hiyo.

Amesema Kamati imependekezwa kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu Biashara ya Kaboni, kuandaa miongozo ya mafunzo kwa wadau wa ngazi zote, pamoja na kuanzishwa majukwaa ya wadau la majadiliano katika ngazi mbalimbali.

Utekelezaji wa Biashara ya Kaboni nchini utaimarika kwa kufanya mapitio ya kanuni na miongozo ya biashara ya Kaboni, kuboresha rejesta ya Taifa ya Kaboni, kuweka mkakati mahususi wa utoaji wa elimu kwa umma, kuboresha mifumo ya usimamizi na utunzaji wa takwimu na kuhamasisha ushirikishwaji wa wadau ikiwemo sekta binafsi.

Ameongeza kwa upande wa Miradi ya kimkakati kunufaika na Biashara ya Kaboni, Tathmini inaonesha kuwa Tanzania ina nafasi kubwa ya kunufaika na Biashara ya Kaboni kupitia utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika sekta mbalimbali, ikiwemo reli ya kisasa ya umeme (SGR), Mabasi yaendayo haraka (Dar es Salaam Rapid Transit - DART), uzalishaji wa umeme, gesi asilia, misitu, kilimo, majengo, elimu, madini, udhibiti wa taka na uchumi wa buluu.  

Jumapili, 29 Juni 2025

ETDCO YANG'ARA TUZO SEKTA YA UJENZI

Mwakilishi wa Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya ETDCO, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa kampuni hiyo, Mhandisi Dismas (wa pili kutoka kushoto), akipokea Tuzo ya Heshima ya Sekta ya Ujenzi kutoka kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Gaudence Mmassy. Tuzo hizo zimeandaliwa na Construction Times Gala and Award 2025 kwa lengo la kutambua mchango wa kamapuni mbalimbali zilizofanyika 28 Juni 2025, jijini Dar es Salaam. Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Gaudence Mmassy akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa makampuni mbalimbali baada ya kutoa tuzo. 

 ..............

 Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO) imefanikiwa kupata Tuzo ya heshima ya Mkandarasi Bora wa Ujenzi na Miundombinu ya Umeme pamoja na uendeshaji wa kampuni kutoka Construction Times Gala and Award 2025 zilizofanyika 28 Juni 2025, jijini Dar es Salaam. 

 Katika tuzo hizo, Kaimu Meneja Mkuu wa ETDCO, CPA Sadock Mugendi, pia ametunukiwa Tuzo ya Uongozi Bora katika Uendeshaji wa Kampuni, ikiwa ni kutambua mchango wake katika kusimamia kwa mafanikio miradi.

 Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) wakati wa hafla ya kukabidhi tuzo hizo, iliyokwenda sambamba na uzinduzi wa Jarida la Ujenzi, Afisa Uwekezaji Mwandamizi wa TIC, Bw. Gaudence Nicholaus Mmassy, amepongeza washindi wote kwa mchango wao mkubwa katika maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini. 

 Akizungumza wakati kupokea tuzo hizo Kwa niaba ya Kaimu Meneja Mkuu wa ETDCO, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Kampuni ya ETDCO, Mhandisi Dismas Masawe, amesema kuwa tuzo hizo ni uthibitisho wa kutambuliwa kwa mchango mkubwa wa kampuni katika ujenzi wa miundombinu ya umeme nchini kwa kuonesha dira ya maendeleo wanayoifuata katika utekelezaji wa majukumu yao. 

 “Siri ya mafanikio haya ni usimamizi thabiti kutoka kwa menejimenti ya Kampuni, pamoja na kujitolea kwa dhati kwa wafanyakazi wetu, na utekelezaji wa miradi kwa weledi wa hali ya juu.” amesema Mhandisi Masawe. 

 Katika tuzo hizo za heshima zilizotolewa na Construction Times, jumla ya makampuni nane yalitunukiwa tuzo hizo za heshima, huku ETDCO ikijivunia kuondoka na tuzo mbili kubwa kutokana na utendaji wake bora, hasa katika usimamizi wa miradi na uendeshaji wa kampuni.


TUWE NA MAONO YA KUIONA KESHO YETU – DKT. BITEKO


................


📌Ni katika Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kuwa na maono ya kuweza kuona mbali hali itakayowasaidia  katika utendaji wa kazi na kupata suluhisho ya changamoto zinazoweza kutokea kabla ya changamoto hizo kutokea.

Dkt. Biteko ameyasema hayo leo Julai 28,2025 katika viwanja vya Jamhuri  Jijini Dodoma, wakati akizungumza na watumishi wa wizara na Taasisi zake wakati wa kufunga Bonanza la michezo mbalimbali lililohusisha Wizara ya Nishati na Taasisi zake.








 

Ijumaa, 27 Juni 2025

DKT BITEKO MGENI RASMI NISHATI BONANZA 2025


.........................

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dkt Doto Biteko anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake litakalofanyika jumamosi Juni 28, 2025 jijini Dodoma.

Akizungumzia maandalizi ya Bonanza hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja amesema kuwa, Nishati Bonanza litafanyika kwenye Viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma na kushirikisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na wadau kutoka Wizara nyingine.

‘’ Nipende kuchukua fursa hii kuzikaribisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati kushiriki kikamilifu bonanza ambalo linaleta fursa ya kufahamiana na kubadilishana mawazo baada ya muda wa kazi pamoja na kufanya mazoezi ili kujenga afya." Amesema Mbuja

Ameongeza kuwa, kwa mwaka huu Nishati Bonanza linaongozwa na kauli mbiu ya "Michezo kwa Afya bora, Shiriki uchaguzi 2025 ikiwa na lengo pia la kuhamasisha wafanyakazi na wananchi kwa ujumla kutumia haki yao ya kikatiba kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 .

Amesema maandalizi yote yameshakamilika na timu zitakazoshiriki michezo mbalimbali zimeshawasili Dodoma kushiriki bonanza hilo litakaloshirikisha watu takribani 1000.

Ametaja michezo itakayoshindaniwa kuwa ni ni pamoja na Mpira wa miguu, Mpira wa Pete, Mpira wa Wavu, Mpira wa Kikapu, Kuvuta Kamba, pamoja na michezo ya jadi kama vile bao na drafti, pia kufukuza kuku.

Taasisi zitakazoshiriki Bonanza hilo la Nishati ni pamoja na TANESCO, REA, TPDC, PURA, EWURA, TGDC, ETDCO, TCPM, TANOIL, GASCO, PBPA.

Hili ni Bonanza la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Doto Biteko mwaka jana.









Listen Mkisi Radio