JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumamosi, 14 Juni 2025

RAIS SAMIA NA RAIS WA BENKI YA AFRIKA AfDB WAKAGUA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE MSALATO

Muonekano wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato Jijini Dodoma tarehe 14 Juni, 2025. ujenzi wa Kiwanja hicho cha Msalato unahusisha njia ya kuruka na kutua ndege (runway) jengo la abiria, jengo la kuongozea ndege pamoja na Miundombinu mengine.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Nala Jijini Dodoma mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato pamoja na ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje ya Jiji la Dodoma yenye urefu wa km (112.3) tarehe 14 Juni, 2025.

Matukio mbalimbali kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Nala Jijini Dodoma tarehe 14 Juni, 2025.

DC MSANDO AONGOZA MAADHIMISHO SIKU YA MAZINGIRA MKOA WA DAR,ASISITIZA NISHATI SAFI

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es salaam Albert Msando akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya mazingira kimkoa ambayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Makuburi kwenye Wilaya hiyo Leo tar 14/6/2025.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo Jaffary Juma Nyaigesha akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya mazingira kimkoa ambayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Makuburi Ubungo Leo tar 14/6/2025 jijini Dar es salaam.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Songoro Mnyonge akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya mazingira kimkoa ambayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Makuburi Ubungo Leo tar 14/6/2025 jijini Dar es salaam.

...........................

NA MUSSA KHALID 

Serikali imeendelea kuweka msisitizo wa kupunguza athari za uharibifu wa mazingira kwa kupunguza matumizi ya nishati ya kuni na mkaa kwa shughuli za kupikia ili kuepukana na changamoto ya uharibifu wa mazingira.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Albert Msando alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam katika maadhimisho ya Siku ya mazingira kimkoa ambayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Makuburi kwenye Wilaya hiyo,yakienda sambamba na kauli mbiu ya "Mazingira yetu na Tanzania Ijayo,tuwajibike sasa dhibiti matumizi ya Plastiki"

DC Msando amesema kuwa kauli mbiu hiyo inatoa chajizo la kila mwananchi kuhakikisha anahifadhi mazingira ikiwemo kuhamasisha na kuielimisha jamii kuhusu umuhimu wa mazingira kwa kudhibiti matumizi ya plastika.

"Nitoe wito kwa vyombo vya Habari,taaisisi zote za serikali na zisizoza serikali pamoja na wadau mbalimbali kushirikiana katika kutoa elimu kwa jamii ili kupunguza uharibifu wa mazingira nchini Kwa kudhibiti matumizi ya Plastiki"amesema DC Msando

Aidha amesema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila ameziagiza Halmashauri zote katika Mkoa huo kuendeleza juhudi za ukusanyaji wa taka ngumu na laini ili kudumisha usafi wa mazingira kwenye maeneo yao.

Pia amewaagiza wakandarasi wote waliopewa kazi ya kukusanya taka kwenye Mkoa huo kuhakikisha wanatimiza wajibu wao wa kimkataba Kwa ufanisi.

Awali wakizungumza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinonondoni Songoro Mnyonge amesema wataendelea kutoa elimu ikiwemo kuhamasisha matumizi ya nishati safi huku Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo Jaffary Juma Nyaigesha akisisitiza kuthaminiwa Kwa watu wanaofanya shughuli za kuokota na kukusanya taka katika maeneo mbalimbali.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Bonde la Wamiruvu Mkoa wa Dar es salaam Bi Diana Kimbute amesema mazingira yanapotunzwa ndivyo pia vyanzo vya Maji vinatunzwa.

Katika Maadhimisho yao yamezikutanisha kwa pamoja Halmashauri za Mkoa wa Dar es salaam ambapo pia wameshiri wadau kutoka Taasisi mbalimbali wa mazingira ikiwemo Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ya HUDEFO,Taasisi zinazojihusisha na masuala ya nishati,wanafunzi na wazalishaji wa mitungo ya gesi


MAGAZETI YA TZ LEO JMOSI JUNI 14,2025

 

Listen Mkisi Radio