TAARIFA zilizotufikia kutoka vyanzo vya uhakika zimedokeza kuwa aliyekuwa afisa habari wa Yanga SC Ally Shaban Kamwe Ameandika barua kwa uongozi wa Yanga SC Kujiuzulu nafasi yake ya idara ya Habari na mawasiliano baada ya kuitumikia nafasi hiyo toka Septemba 25 mwaka 2022 Hadi leo alipojiuzulu Rasmi .
Kupitia page yake ya Instagram Ally Kamwe mwenyewe ameandika hivi .
"Mtumbuizaji mzuri anatakiwa kujua ni wakati gani wa kuondoka Jukwaani..
Maneno ya hekima kutoka katika kinywa cha Patrick Loch Otieno Lumumba;
Na ni Hekima hii, inanituma mbele yenu Wananchi, Mashabiki na Wanachama wa Klabu yetu pendwa, kuwaambia kuwa, Ni wakati sasa wa kijana wenu kuondoka Jukwaani.
Nimesimama Miaka miwili juu ya hili Jukwaa, Tumeimba, Tumecheza, Tumefurahi na Alhamdulillah Tumeshinda pamoja kila pambano Lililokuja mbele yetu.
Muda wangu umemalizika na Asanteni sana.
Tutaonana tena Wakati mwingine nikiwa na kitu kizuri cha kuwaonyesha Juu ya Jukwaa.
0 Comments