JSON Variables

Wednesday, July 10, 2024

VIDEO: Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Tanzania sekta ya sukari ni kipaumbele

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Tanzania sekta ya sukari ni kipaumbele katika kilimo kwa kuwa viwanda vya sukari ni vitovu vya kilimo na uchumi. 

 

Rais Dkt.Mwinyi aliyasema hayo alipofungua mkutano wa wazalishaji sukari wa nchi za SADC katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip  iliopo uwanja wa ndege Zanzibar.

 

Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa Tanzania imeweka mazingira wezeshi ya uwekezaji katika kilimo cha Miwa na uzalishaji sukari. 

 

Rais Dkt.Mwinyi ametoa rai kwa nchi za SADC kutumia fursa zilizopo kwa kuweka mazingira bora zaidi ya uwekezaji ili kukuza uzalishaji wa Sukari. 

 

Kwa upande mwingine Rais Dkt.Mwinyi ametoa wito kwa washiriki wa mkutano huo wa siku moja kuwekeza kikamilifu katika teknolojia za kisasa na mbinu za kilimo za kisasa zinazoongeza tija ili kuboresha mavuno ya miwa na uzalishaji sukari Afrika.

 

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha wazalishaji wa sukari Tanzania Seif Ali  Seif amesema mkutano huo utawasaida kuwa na sera a pamoja za kufikia malengo na kutatua changamoto mbalimbali.

Waziri wa Viwanda na Biashara Selemani Jaffo amesema serikali itaendelea kuwalinda wazalishaji wa sukari ili kuongeza uzalishaji wa sukari.

Akimkarishisha rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi kufungua mkutano huo,waziri wa biashara na maendeleo ya viwanda Omar Said Shaaban amesema kwa Zanzibar bado wanafasi kubwa ya kuwakaribisha wawekezaji ili kuongeza mnyororo wa thamani.

 

Ni  mkutano wa Wazalishaji wa sukari wa nchi za sadec ambao pamoja na mambo mengine unajadili  masuala muhimu ya Sekta ya Sukari hususan, changamoto  katika Sekta na namna ya kuzipatia ufumbuzi wake, mkutano  huo umefunguliwa na rais wa Zanzibar dkt Hussein ali mwinyi ambae amesema mkutano ho utasaidia kuimarisha mazingira wezeshi kwa maendeleo endelevu ya sekta ya sukari katika nchi wanachama wa SADC.

 

0 comments:

Post a Comment