Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 50 amekamilisha mpango wa miezi miwili wa upandikizaji wa kila wiki wa kinyesi katika Chuo Kikuu cha Birmingham kwa matumaini ya kudhibiti dalili za ugonjwa sugu wa ini unaoitwa, sclerosing cholangitis (PSC).
"Sio tu kipande cha kinyesi," anacheka wakati anaelezea mchakato wa upandikizaji. "Kinatengenezwa, kinapitia mchakato katika maabara."
Kwa sasa hakuna tiba ya ugonjwa adimu wa Dallaway, isipokuwa upandikizaji wa ini kwa mgonjwa. Ugonjwa huu unaathiri kati ya watu sita na saba katika kila watu 100,000 nchini Uingereza na hupunguza umri wa kuishi kwa miaka 17 hadi 20.
Dallaway aligunduliwa kuwa na ugonjwa huo miaka minane iliyopita, alipokuwa na umri wa miaka 42.
"Nilikuwa na wasiwasi sana, na wasiwasi sana juu ya siku zijazo," anakumbuka. "
0 Comments