Sayari hii iliyo nje ya Mfumo wa Jua ilikuwa tayari inajulikana kwa hali ya hewa yake mbaya ya jua kali. Lakini sifa yake nyingine iliyogundulika hivi karibuni, ni kutoa harufu mbaya kama mayai yaliyooza.
Wanasayansi katika Chuo Kikuu cha John Hopkins nchini Marekani walitumia taarifa kutoka Darubini ya Anga ya juu ya James Webb ili kuchunguza sayari inayojulikana kama HD 189733 b, yenye ukubwa wa Jupiter.
Angahewa ya sayari hii ina hidrojeni sulfidi, molekuli ambayo husababisha harufu kali kwa mayai yaliyooza na gesi tumboni kwa binaadamu.
"Ikiwa pua yako inaweza kuishi kwenye nyuzi joto 1,000 ° C, anga yake inanuka kama mayai yaliyooza," anasema Dk. Guangwei Fu, mwanaastrofizikia wa Johns Hopkins ambaye aliongoza utafiti huo.
HD 189733 b ni miaka 64 tu ya mwanga kutoka duniani na ndiyo sayari ya karibu zaidi ambayo wanaanga wanaweza kuiona wakipita mbele ya nyota yake.
“Wanasayansi wanafanya uchunguzi wa sayari hiyo tangu ilipogunduliwa mwaka 2005,” anasema Dkt. Fu.
Sayari hiyo iko karibu mara 13 karibu na nyota yake, kuliko Mercury ilivyo karibu na Jua na inachukua takribani siku mbili tu za dunia kukamilisha mzunguko mmoja.
Ina joto kali la takribani nyuzi joto 1,000 °C, fuwele zinazong’aa na upepo wa zaidi ya kilomita 8,000 kwa saa.
Kutoka BBC
0 Comments