Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Ukraine yaelezea wasiwasi kuhusu nyambizi za Urusi katika Bahari Nyeusi

 

Nyambizi tatu za Urusi ziko katika Bahari Nyeusi, vikosi vya ulinzi vya Ukraine vinaendelea kufuatilia hali ilivyo, msemaji wa Jeshi la Wanamaji la Ukraine Dmitry Pletenchuk amesema.

"Hali bado haijabadilika - kuna nyambizi tatu huko sasa. Haya ni kama mafunzo ya kijeshi, lakini hata hivyo, mazoezi huishia mara kwa mara kwa ufyatuaji wa risasi.

Kwa hivyo, kila wakati mtu anapaswa kutarajia hatari kutokana na vitengo hivi na tunatarajia hilo," Pletenchuk alinukuliwa akisema na shirika la habari la Ukraine -Ukrayinska Pravda.

Hapo awali, Pletenchuk aliripoti kwamba jeshi la wanamaji la Urusi liliweka manowari tatu, ambazo hutumika kusafirisha makombora ya cruise, ndani ya bahari , na alizungumzia kuhusu mabadiliko ya mbinu za Urusi katika Bahari Nyeusi na Azov.

Urusi haijatoa taarifa zozote kuhusu ripoti za nyambizi zake katika Bahari Nyeusi.

Tangu 2022, jeshi la Ukraine limeshambulia zaidi ya meli 20 za Urusi na meli za msaada. Kati ya meli hizo angalau saba ziliharibiwa.

Post a Comment

0 Comments