Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama barabarani Tanzania DCP. Ramadhani Ng'anzi amesema tatizo la ajali za barabarani bado ni kubwa hivyo Jeshi la Polisi Kikosi cha usalama barabarani linafanya kila jitihada ili kuhakisha ajali zinatomezwa ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua madereva wasio tii sheria.
Kamanda Ng'anzi ameyasema hayo leo Julai 10, 2024 Jijjni Dar es salaam wakati akiwakabidhi vyeti na zawadi askari 5 wa kikosi hicho waliofanya kazi vizuri zaidi mwaka 2023/2024.
"Tunajua janga la ajali za barabarani hapa nchini bado ni kubwa na linatutesa lakini jitihada zinazofanyika, tunaamini ipo siku ile ndoto yetu ya Tanzania bila ajali kwa mwaka inawezekana" Alisema DCP Ng'anzi
0 Comments