*Wito:*
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, ameombwa na wananchi wa baadhi za kata aungane nao kwenye ujenzi wa sekondari ya pili na ya tatu ya kata zao - Mbunge amekubali.
*Takwimu:*
Jumla ya Sekondari Jimboni mwetu:
(i) Sekondari 26 za Kata/Serikali
(ii) Sekondari 2 za Madhehebu ya Dini
(iii) Sekondari mpya 3 zinazojengwa kwa nguvu za wanavijiji na viongozi wao: Kisiwani Rukuba (Kata ya Etaro, sekondari ya pili), Kijijini Nyasaungu (Kata ya Ifulifu, sekondari ya pili) na Kijijini Muhoji (Kata ya Bugwema, sekondari ya pili - Serikali imeanza kuchangia).
Sekondari hizi 3 zitafunguliwa Januari 2025
(iv) Sekondari mpya 3 zinajengwa kwa kutumia fedha nyingi za Serikali: Kijijini Butata (Kata ya Bukima, sekondari ya pili), Kijijini Kasoma (Kata ya Nyamrandirira, sekondari ya tatu) na Kijijini Kurwaki (Kata ya Mugango, sekondari ya pili)
Sekondari hizi 3 zitafunguliwa Januari 2025
Jimbo letu lina Kata 21 zenye Vijiji 68 (jumla ya Vitongoji ni 374)
*Ratiba ya Mikutano ya Hadhara na Harambee za ujenzi wa sekondari mpya:*
Jumanne, 13.8.2024
Saa 4 Asubuhi: Kijijini Kataryo, Kata ya Tegeruka (sekondari ya pili)
Saa 9 Alasiri: Kijijini Mmahare, Kata ya Etaro (sekondari ya tatu)
Jumatano, 14.8.2024
Saa 4 Asubuhi: Kijijini Chitare, Kata ya Makojo (sekondari ya pili)
Saa 9 Alasiri: Kijijini Kiriba, Kata ya Kiriba (sekondari ya tatu)
Alhamisi, 15.8.2024
Saa 4 Asubuhi: kazi maalumu
Saa 9 Alasiri: Kijijini Nyambono, Kata ya Nyambono (sekondari ya pili)
Ratiba ya Vijiji vya Butata (Kata ya Bukima), Kasoma (Kata ya Nyamrandirira) na Kurwaki (Kata ya Mugango) itatolewa baadae.
*KARIBUNI TUCHANGIE UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWETU*
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
P. O. Box 6
Musoma
Tarehe:
Ijumaa, 9.8.2024
0 Comments