Header Ads Widget

Responsive Advertisement

MIKUTANO YA HADHARA NA HARAMBEE ZA UJENZI WA SEKONDARI MPYA MUSOMA VIJIJINI

 


*Wito:*

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, ameombwa na wananchi wa baadhi za kata aungane nao kwenye ujenzi wa sekondari ya pili na ya tatu ya kata zao - Mbunge amekubali.


*Takwimu:*

Jumla ya Sekondari Jimboni mwetu:

(i) Sekondari 26 za Kata/Serikali 

(ii) Sekondari 2 za Madhehebu ya Dini


(iii) Sekondari mpya 3 zinazojengwa kwa nguvu za wanavijiji na viongozi wao: Kisiwani Rukuba (Kata ya Etaro, sekondari ya pili), Kijijini Nyasaungu (Kata ya Ifulifu, sekondari ya pili) na Kijijini Muhoji (Kata ya Bugwema, sekondari ya pili - Serikali imeanza kuchangia). 


Sekondari hizi 3 zitafunguliwa Januari 2025


(iv) Sekondari mpya 3 zinajengwa kwa kutumia fedha nyingi za Serikali: Kijijini Butata (Kata ya Bukima, sekondari ya pili), Kijijini Kasoma (Kata ya Nyamrandirira, sekondari ya tatu) na Kijijini Kurwaki (Kata ya Mugango, sekondari ya pili)


Sekondari hizi 3 zitafunguliwa Januari 2025


Jimbo letu lina Kata 21 zenye Vijiji 68 (jumla ya Vitongoji ni 374)


*Ratiba ya Mikutano ya Hadhara na Harambee za ujenzi wa sekondari mpya:*


Jumanne, 13.8.2024

Saa 4 Asubuhi: Kijijini Kataryo, Kata ya Tegeruka (sekondari ya pili)


Saa 9 Alasiri: Kijijini Mmahare, Kata ya Etaro (sekondari ya tatu)


Jumatano, 14.8.2024

Saa 4 Asubuhi: Kijijini Chitare, Kata ya Makojo (sekondari ya pili)


Saa 9 Alasiri: Kijijini Kiriba, Kata ya Kiriba (sekondari ya tatu)


Alhamisi, 15.8.2024

Saa 4 Asubuhi: kazi maalumu


Saa 9 Alasiri: Kijijini Nyambono, Kata ya Nyambono (sekondari ya pili)


Ratiba ya Vijiji vya Butata (Kata ya Bukima), Kasoma (Kata ya Nyamrandirira) na Kurwaki (Kata ya Mugango) itatolewa baadae.


*KARIBUNI TUCHANGIE UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWETU*


Ofisi ya Mbunge 

Jimbo la Musoma Vijijini 

www.musomavijijini.or.tz 


P. O. Box 6

Musoma 

Tarehe:

Ijumaa, 9.8.2024

Post a Comment

0 Comments