Alisema mradi huo, utawezesha ng'ombe wa maziwa kufungwa vifaa vya kisasa aina ya smaXtec bolus itakayosaidia mfugaji kufuatilia kwa karibu tabia za ng'ombe wake kupitia mfumo uliounganishwa na simu ya kiganjani ikiwemo kujua kiwango cha chakula au maji ambacho amekula au kunywa kwa siku.

Lakini pia atatoa maziwa kwa kiasi gani kulingana na uzalishaji huku kifaa cha Ceres tag ambacho ni mfano wa hereni kitatumika kwa kumvalisha sikuoni ng'ombe mmoja katika kundi la ng'ombe wafugwao katika jamii za kimaasai.

Mradi wa Tathimini ya Ufanisi wa za Kisasa za Ufugaji unashirikisha Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Chuo Kikuu cha Florida cha Nchini Marekani MAP Scientific Services (Ceres Tag), SmaXtec (Bolus Monitoring System) kwa ufadhili wa Bill and Melinda Gates Foundation.