Shirikisho la mpira wa miguu Afrika ( CAF) wamefungia uwanja wa Benjamin Mkapa kutokana na kukosa ubora eneo la kuchezea ( Pitch ) huku wakieleza kuwa yanahitajika maboresho yafanywe haraka ili kuepusha uwanja huo kufungwa kwa muda mrefu.
Klabu ya Simba Sc ambayo ilipanga kucheza mchezo wake wa robo fainali kombe la Shirikisho dhidi ya Al Masri April 9 mwaka huu hivyo kuepuka usumbufu Shirikisho la mpira wa miguu TFF limetakiwa kutuma jina la uwanja mbadala utakaotumiwa na klabu ya Simba kufikia Machi 14 .
CAF imepanga kufanya ukaguzi wa uwanja wa Benjamin Mkapa ifikapo machi 20 ili kuona kama maboresho yamefanyika ili kuona kama unafaa kutumika au uendelee kufungiwa.
Mbali na mashindano hayo uwanja Benjamin Mkapa pia umepangwa kutumika kwenye mashindano ya fainali za CHAN yatakayofanyika Agosti 2025.
0 Comments