.……....
Na Sixmund Begashe - Singida
Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii Leo tarehe 1 Mei 2025, wameungana na wafanyakazi wote Duniani kwenye Maadhimisho Siku ya wafanyakazi Duniani MEI MOSI ambayo kitaifa yamefanyika mkoani Singida huku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa Mgeni rasmi.
Maadhimisho hayo yalipambwa na matembezi mbele ya jukwa kuu mapoja na burudani mbalimbali ambapo Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii walinog'esha maadhimisho hayo kwa Mavazi rasmi na mabango yaliyobeba ujumbe wa kutangaza vivutio vya Utanii na kuhamasisha Uhifadhi.
Tags
Top Stories