JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumamosi, 21 Juni 2025

MADEREVA WAJA NA "TUNAKWENDA NA SAMIA 2025"

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Patrobas Katambi akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam  Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Patrobas Katambi akikabidhiwa Tuzo ya Rais Samia Suluhu Hassan kutoka Kwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Madereva wa masafa marefu na ya kati Tanzania Hassan Dede katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es salaam Albert Msando akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam  Mwenyekiti wa Taasisi ya Madereva wa masafa marefu na ya kati Tanzania Hassan Dede akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam  Mrakibu wa Polisi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Tanzania -Mussa Manyama akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam  Mr Chuki Shaban,Mwenyekiti wa wamiliki wa Malori (TAMSTOA) akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam.(PICHA ZOTE NA MUSSA KHALID)

Baadhi ya Madereva walioshiriki katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika Leo Tar 21/6/2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam 

.....................

NA MUSSA KHALID 
Serikali imeendelea kuwasisitiza madereva wa masafa marefu nchini  kudumisha amani ulinzi na usalama wa vyombo, ikiwemo kutiii Sheria na taratibu za kimamlaka na usimamizi ili kuonyesha uzalendo kwa Taifa.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Patrobas Katambi ametoa wito huo leo wakati akizungumza katika kongamano la Kitaifa la madereva wa malori na mabasi na masafa marefu na kati ambalo limefanyika katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam yenye kauli mbiu isemayo "madereva tunakwenda na Samia 2025".

Aidha Naibu Waziri Katambi amewapongeza madereva hao kwa kuandaa kongamano hilo lenye dhamira ya kuipongeza serikali katika kazi kubwa iliyofanywa nchini.
Katika hatua nyingine Naibu Waziri Katambi amesema kuwa serikali inaendelea kusisitiza utoaji wa mikataba kwa madereva ili kuonyesha makubaliano kati ya mmiliki wa chombo na madereva.

"Ni muhimu sana kutoa mikataba kwa sababu inaonyesha haki ya wajibu kwa Mmiliki wa chombo na Dereva lakini usalama wa chombo ni kupitia mkataba"amesema Naibu Waziri Katambi

Awali akizungumza Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Albert Msando amesema kuwa watahakikisha wanaendeleza ushirikiano na madereva wote wanaofanya shughuli zao kwani Ubungo imekuwa ni lango la kwenda katika maeneo mbalimbali nchini 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Madereva wa masafa marefu na ya kati Tanzania Hassan Dede ametumia fursa hiyo kusema madereva wanakiu kubwa kuona mambo yanabadilika.

Naye Mrakibu wa Polisi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Tanzania -Mussa Manyama amesema wao kama wasimamizi wa sheria wanawakumbusha madereva kuendelea kutii Sheria za usalama barabarani ili kuepukana na ajali.
Amewataka kuondoka na kuendesha magari Kwa mwendo wa masi kwani imekuwa ni chanzo kikubwa cha ajali barabarani
Mr. Chuki Shaban ni Mwenyekiti wa wamiliki wa Malori (TAMSTOA) amesema ni vyema wamiliki wote wa Malori kuingia kwenye Vyama ili kuweza kutambulika Kwa haraka.

0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio