JSON Variables

Tuesday, April 15, 2025

UTATUZI MIGOGORO KWA NJIA MBADALA WA MAHAKAMA UNAWEZEKANA-NCC

Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu, Dk Fauz Twaib akizungumza wakati wa mafunzo ya kuhusu utatuzi migogoro kwa njia mbadala wa mahakama yaliyoandaliwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) ambayo yamefanyika kwa siku tatu jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, anayehusika na sehemu ya mikataba, majadiliano na utawala, Mkadiriaji Majenzi Elias Kisamo akijibu maswali tatizi yaliyoulizwa na washiriki wa mafunzo utatuzi migogoro kwa njia mbadala wa mahakama yaliyoandaliwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) ambayo yamefanyika kwa siku tatu jijini Dar es salaam.

Mhandisi wa kujitegemea, Julius Mamiro akifundisha washiriki wa mafunzo mbinu ya utatuzi migogoro kwa njia mbadala wa mahakama ambayo  yaliyoandaliwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) ambayo yamefanyika kwa siku tatu jijini Dar es salaam.

Baadhi ya washiriki wa wa mafunzo ya kuhusu utatuzi migogoro kwa njia mbadala wa mahakama yaliyoandaliwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) ambayo yamefanyika kwa siku tatu jijini Dar es salaam.

Picha ya pamoja wakufunzi na washiriki wa wa mafunzo ya kuhusu utatuzi migogoro kwa njia mbadala wa mahakama yaliyoandaliwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) ambayo yamefanyika kwa siku tatu jijini Dar es salaam.

........................

Na Mwandishi wetu

-Yaelimisha namna ya kuitatua bila kujeruhi upande wowote 

BARAZA la Taifa la Ujenzi (NCC) limesema usuluhishi wa migogoro ya kibiashara, madai ya kimkataba na mingine iliyopo na inayojitokeza kwenye sekta ya Ujenzi, unawezekana bila wahusika wa migogoro hiyo kupelekana mahakamani.

Hali hiyo, kwa mujibu wa wataalamu wa masuala hayo ya usuluhishi na utatuzi wa migogoro wanaotoa mafunzo kuhusu eneo hilo, chini ya uratibu wa NCC, inasaidia si tu kuokoa muda na kuacha wahusika wakiwa na amani, bali inapunguza mirundikano ya kesi mahakamani.

Akizingumza Dar es Salaam hivi karibuni wakati mafunzo hayo yaliyoandaliwa na NCC yakiendelea, Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu, Dk Fauz Twaib ambaye ni miongoni mwa wafundisha njia hizo, alisema: "Kinachotakiwa ni wasuluhishi kuzingatia maadili, sheria na taratibu za usuluhishi". 

Alisema njia zaidi ya nne za kusuluhisha migogoro mbali na kushitakiana mahakamani, zinafundishwa na kuwawezesha waliopata mafunzo hayo kuamua kwa weledi ipi inafaa kulingana na mazingira na hali halisi ya mgogoro husika.

Kwa mujibu wa Dk Twaib, Kwa kutumia njia hizo mbadala, hakuna upande unaojeruhiwa, kwa sababu pande zote zinahusika katika hatua zote muhimu za usuluhishi, ikiwemo kuchagua nani ahusike kuwasuluhisha.

"Ikiwa hakuna mazingira yoyote ya tamaa inayoweza kusababisha upendeleo, mfano rushwa au chochote kile kitakachofanya usuluhishi uegemee upande mmoja, mlolongo wa kisuluhishi hautokei, hivyo kuokoa muda na gharama.

Kwa upande wake, Mhandisi wa kujitegemea, Julius Mamiro anayefundisha mbinu hizo, hususan majadiliano ya kisuluhishi ya madai ya kimkataba ya ujenzi alisema, maadili mazuri yanafanikisha usuluhishi.

Alisema, jambo kubwa wanalolisisitiza ni wataalamu wa masuala yote yanayoweza kuhusika kwenye migogoro, iwe ya sekta ya ujenzi au ya kibiashara nje ya sekta ya ujenzi au ya kimkataba kwenye sekta yoyote, wawe na elimu ya namna ya kuitatua migogoro yao bila kupelekana mahakamani, kisha watekeleze mbinu walizofundishwa kwa kuzingatia maadili.

Kwa maelezo yake, kujua kusuluhisha au kutatua mgogoro halafu ukauharibu utatuzi kwa kutoruhusu haki au kwa kupendelea, hata kama umefunzwa vipi, unabaki kuwa kikwazo cha usuluhishi. 

"NCC inatekeleza jukumu la kuhakikisha elimu hiyo inawafikia watu wengi, kwa faida ya wanaoipata, wateja wao, familia zao na Taifa kwa ujumla.

Alisema, kutokana na umuhimu huo, anawashauri Watanzania kuchangamkia mafunzo hayo pindi wanaoipata fursa hiyo nyakati zote yanapotangazwa.

Katika mafunzo hayo yaliyotolewa kwa siku tatu, washiriki walifanya mazoezi ya usuluhishi kwa vitendo na kisha kutahiniwa kwa mtihani wa kuandika, lengo likiwa kupima uelewa wao kuhusu maarifa waliyapata kwenye mafunzo hayo.

Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, anayehusika na sehemu ya mikataba, majadiliano na utawala, Mkadiriaji Majenzi Elias Kisamo, pamoja na kufundisha, alijibu maswali tatizi yaliyoulizwa na washiriki wa mafunzo hayo, hivyo kuongeza uelewa wao juu ya walichojifunza.

Kisamo alisema," Ukitaka usuluhishi uende sawa, epuka njia za mkato. Hakuna shortcuts, iwe katika majadiliano au kwenye utatuzi mwingine, epuka 'shortcuts'...

Monday, April 14, 2025

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAZIDI KUJIIMARISHA KATIKA MIPANGO NA SERA.

 

...................

Na Sixmund Begashe - Singida

Wataalam wa Sera na Mipango Wizara ya Maliasili na Utalii wameendelea na kikao kazi Mkoani Singida kwa lengo la kupata uwelewa wa pamoja wa namna bora zaidi ya utekelezaji wa mpango wa shughuli mbalimbali za Uhifadhi na Utalii kwa mwaka 2025/2026

Akizungumza kwenye kikao kazi hicho, Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Bw. Abdullah Mvungi licha ya kuwapongeza wataalam hao kwa michango mizuri, amewasisitiza kuendeleza umakini katika mapitio na maboresho ya mipango hiyo ili iweze kuleta tija zaidi kipindi cha utekelezaji wake.

Bw. Mvungi ameeleza kuwa, wataalam hao kutoka Idara na Taasisi mbalimbali za Wizara hiyo wamekuwa ni chachu kubwa ya Maendeleo endelevu ya Uhifadhi na sekta ya Utalii kutokana na umahiri wao katika sera na Mipango inayotekelezeka katika Wizara hiyo yenye mchango mkubwa katika pato la taifa.

   

TUTAENDELEA KUDHIBITI UHALIFU WA KIFEDHA-MAJALIWA

................ 

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Tanzania itaendelea kushiriki na kutimiza matakwa ya kimataifa katika kupambana na kudhibiti uhalifu wa kifedha.
 
Amesema kuwa Tanzania inatambua changamato za uhalifu wa kifedha na imejidhatiti katika kudhibiti hali hiyo kwa viwango vya kimataifa vilivyopo.
 
Amesema hayo leo Jumatatu (Aprili 14, 2025) wakati Ufunguzi wa Mkutano kati ya Ujumbe wa Tanzania na Kikosi Kazi cha Kimataifa cha Kudhibiti Fedha Haramu, kwenye ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
 
Amesema kuwa kufuatia tathmini zilizofanywa na taasisi za Kuthibiti Uhalifu wa Kifedha Kusini Mashariki mwa Afrika mwaka 2021 na Kikosi cha Kimataifa cha Ushirikiano na Tathmini ya mwaka 2022, Tanzania imeimarisha mifumo ya kupambana na fedha haramu ikiwemo kujengea uwezo wa rasilimali watu na vifaa taasisi zinazohusika katika mapambano hayo.
 
Waziri Mkuu ameyataja maeneo yaliyofanyiwa kazi kuwa ni mabadiliko ya sheria na sera, matumizi ya takwimu na teknolojia, kuimarisha sekta nyumba na ardhi, kuwajengea uwezo wadau na kuimarisha usimamizi wa Taasisi za za kifedha.
 
Kwa upande wake, Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa Tanzania baada ya kupokea mpango kazi kutoka Kikosi Kazi cha Kimataifa cha Kupambana na Fedha Haramu ilifanya maamuzi ya ngazi ya juu ya kuimarisha usimamizi uhalifu wa kifedha nchini hali ambayo imeonesha mafanikio makubwa

 

TPDC, ZPDC ZAENDELEA KUSHIRIKIANA UENDELEZAJI SEKTA YA GESI NCHINI

.................

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) mwezi Februari, 2022 liliingia makubaliano ya ushirikiano na Shirika la Maendeleo ya Petroli Zanzibar (ZPDC) ambapo kupitia ushirikiano huo masuala mbalimbali yamekuwa yakifanyika kuiendeleza Sekta  ikiwemo kubadilishana ujuzi na utaalam.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Aprili 14, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Kwahani, Mhe. Khamis Yussuf Mussa Mkenge aliyeuliza ni lini Serikali  itainufaisha Zanzibar katika matumizi ya Nishati ya Gesi ili iweze kutumika katika magari.

"Mheshimiwa Spika katika ushirikiano huu suala la kupeleka gesi Zanzibar ni mojawapo ya agenda kuu. Pande zote mbili bado zinaangalia namna bora ya kufikisha gesi asilia Zanzibar ili iweze kupatikana kwa bei nafuu kwa watumiaji.". Amesema Mhe. Kapinga 

Saturday, April 12, 2025

BALOZI NCHIMBI ASAINI KANUNI ZA MAADILI YA UCHAGUZI MKUU 2025

******

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ameshiriki katika utiaji saini wa Kanuni za Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025. Shughuli hiyo imefanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), ikitanguliwa na mjadala wa Makatibu Wakuu wa Vyama vya Siasa vyote vyenye usajili wa kudumu, waliohudhuria na kuridhia kanuni hizo, leo Jumamosi, tarehe 12 Aprili 2025.







 

Watumishi Watakiwa Kuzingatia Taratibu za Ununuzi Ili Kuepusha Mianya ya Rushwa

 


Na Mwandishi Wetu

TABORA


Watumishi kutoka Taasisi mbalimbali wametakiwa kuzingatia taratibu za manunuzi ili kuepusha mianya ya Rushwa na  kuendelea kujenga uchumi wa nchi imara kwa manufaa ya taifa.


Hayo yanesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Paul Matiko Chacha wakati akifunga mafunzo ya kujengea uwezo watumishi kutoka taasisi mbalimbali kuhusu matumizi ya Mfumo wa NeST     ambayo yamefanyika kuanzia Aprili 07 hadi 11, 2025 katika ukumbi wa Mwanakiyungi Mkoani Tabora.

Mhe. Paul amesema mafunzo hayo yamekuwa ya kipekee kwa sababu yamejikita katika moduli mpya na muhimu kwa maboresho ya michakato ya ununuzi wa umma nchini ambapo Mfumo wa NeST unaendelea kuboresha uwazi, uwajibikaji, na ufanisi katika matumizi ya fedha za umma.


“Sasa ndugu zangu mara nyingi tunasikia mfumo unachelewesha lakini mimi nasema mifumo haicheleweshi, mifumo hii imekuja kwaajili ya kurahisisha kazi zetu sasa ninyi wataalamu wetu mpo hivyo muikotroo na kwa bahati nzuri  mifumo hii inaindeshwa na wewe hivyo tujitahidi kuwa waadilifu ili tuache kusingizia mfumo”alisema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhandisi Deusdetith Katwale amesema mafunzo hayo  ni muuendelezo wa jitihada za serikali katika kuhakikisha changamoto za ununuzi ndani ya taifa ziwe zinashughulikiwa kimifumo ili kuendana na teknolojia inayozidi kushika kasi nchini.


“Sasa hivi serikali inashika kasi kwenye mambo ya kidijitali ambapo zamani tulikuwa tunasema serikali inawasiliana kwa makaratasi tu lakini sasa hivi serikali tunawasiliana kidijitali kwa hiyo ni mwendelezo wa kuhakikisha inakuwa na mifumo imara ya mawasiliano hivyo ni imani yangu kwamba mafunzo yaliyofanyika hapa yataendelea kuleta chachu na kupunguza mianya ya rushwa katika Serikali yetu” aliongeza Mkuu wa Wilaya.

Naye, Mkurugenzi wa Idara ya Kujenga Uwezo na Huduma za Ushauri kutoka PPRA Makao Makuu, Bi. Winfrida Samba amesema, lengo kuu la mafunzo hayo ni kupata elimu kuhusu Mfumo wa  NeST na katika mfumo huo kuna moduli mbalimbali na nyingine ni moduli ni mpya ambazo  zilizopelekea kufanya mafunzo hayo. 


“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa katika Mfumo wetu wa NeST tuna moduli mbalimbali ikiwemo usajili  ambayo inahusika na wazabuni pamoja na taasisi nunuzi, moduli nyingine ni “Etendering” ambayo inahusika na uchakataji wa zabuni  pia tuna moduli ya “E-contract Management” ambayo nayo inahusika na usimamizi na utekelezaji  wa Mikataba, tuna “Epayment”ambayo inahusika na masuala ya malipo lakini pia tuna moduli ndogo ambazo hizi ndizo washiriki wamejifunza zaidi” alisema Mkurugenzi Samba.

Mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa serikali  kuhusu Mfumo wa NeST yameanza tarehe 7 hadi 11 Aprili, 2025 katika ukumbi wa Mwanakiyungi Mkoani Tabora.

Friday, April 11, 2025

KAPINGA ASEMA KIPAUMBELE CHA SERIKALI NI KUFIKISHA UMEME KWENYE TAASISI ZOTE


.............................

📌 Taasisi 1,272 zaunganishwa na umeme  Lindi

📌  Maeneo ya pembezoni mwa miji kuendelea kuguswa na miradi ya umeme

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema kipaumbele cha Serikali ni kuhakikisha Taasisi zote zinazotoa huduma za kijamii, kiuchumi na kidini zinafikiwa na nishati ya umeme wakati wa utekelezaji wa miradi ya umeme Vijijini.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Aprili 11, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Maimuna Pathan aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itakamilisha kupeleka umeme kwenye Shule na Taasisi zote zikiwepo za dini katika Mkoa wa Lindi.

"Hadi kufikia mwezi Machi 2025, jumla ya Taasisi  1,272 zimeunganishiwa umeme katika Mkoa wa Lindi zikijumuisha: Zahanati 259; Vituo vya Afya 42; Hospitali 9; Shule za Msingi 554; Shule za Sekondari 151; na Taasisi za Dini 257 (Misikiti 142 na Makanisa 115). ". Amesema Mhe. Kapinga

Ameeleza kuwa, kupitia miradi inayoendelea kutekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Taasisi 27 zinatarajiwa kupatiwa umeme mkoani humo.. 

Akijibu swali la Mbunge wa Mbogwe, Mhe. Nicodemas Maganga aliyeuliza kuhusu Makanisa na Misikiti Mbogwe kutokuwa na umeme na mpango gani Serikali inao kuzipelekea Taasisi hizo umeme, Mhe. Kapinga amesema Taasisi hizo zitafikiwa na huduma ya umeme kupitia miradi ya Vitongoji inayoendelea katika Jimbo la Mbogwe, 

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Dkt. Christina Mzava kwa niaba ya Mbunge wa Kishapu, Mhe. Boniphace Butondo aliyetaka kujua ni ipi kauli ya Serikali juu ya Kata ambazo hazijaunganishiwa umeme Kahama na Shinyanga, Mhe. Kapinga amesema Serikali ina mikakati ya kuweka miradi ya umeme pembezoni mwa miji ili wananchi waunganishiwe umeme kwa bei rahisi.

Awali, akijibu swali la msingi la Mbunge wa Kishapu, Mhe. Boniphace Butondo juu ya lini vijiji 42 vilivyobaki vya Wilaya ya Kishapu vitapatiwa umeme, Mhe. Kapinga amesema Jimbo la Kishapu lina jumla ya vijiji 117 ambapo hadi kufikia tarehe 30 Machi, 2025 vijiji vyote 117 sawa na asilimia 100 vilikuwa vimekwisha unganishwa na huduma ya umeme kupitia miradi mbalimbali iliyotekelezwa na Serikali.

Akijibu swali la Mbunge wa Tarime Vijijini, Mhe. Mwita Waitara aliyetaka kufahamu wananchi wa Nywamwaga, Sirari na Nyamongo ni lini wataanza kuunganisha umeme kwa bei ya shilingi elfu 27, Mhe. Kapinga amesema maeneo ya Vijijini yanaunganishwa na umeme kwa shilingi elfu 27 na kwa yale ya pembezoni ipo miradi mingine ya pembezoni mwa mji.