Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Marekani kutuma ndege na meli za kivita huku Iran ikitishia Israel

 


Marekani itapeleka meli na ndege za kivita za ziada Mashariki ya Kati ili kusaidia kuilinda Israel dhidi ya mashambulizi ya Iran na washirika wake, Pentagon imesema

Mvutano bado unaendelea katika eneo hilo kuhusu mauaji ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh nchini Iran na kamanda mkuu wa kundi la wanamgambo wa Lebanon Hezbollah.

Vikosi vya ulinzi wa makombora viliwekwa kwenye hali ya utayari wa kutumwa, Pentagon ilisema, na kuongeza kuwa kujitolea kwake kuilinda Israel ni jambo "lisiloweza kubadilishwa".

Kiongozi wa Iran Ayatollah Khamenei ameapa "adhabu kali" dhidi ya Israel kwa mauaji ya Haniyeh, na kutangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

Kiongozi huyo wa Hamas aliuawa mjini Tehran siku ya Jumatano.

Iran na washirika wake huko Gaza walilaumu Israel kwa shambulio hilo, ambayo haijazungumzia lolote.

Haniyeh mwenye umri wa miaka 62, alichukuliwa kuwa kiongozi mkuu wa Hamas na alikuwa na jukumu muhimu katika mazungumzo yaliyolenga kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano katika vita vya Gaza.

Kifo chake kilitokea saa chache tu baada ya Israel kudai kuwa imemuua Fuad Shukr, kamanda mkuu wa kijeshi wa Hezbollah, nchini Lebanon.


Post a Comment

0 Comments