"ACT BILA KULITAJA JINA LA MAALIM SEIF HAKUNA JIPYA KWA WAZANZIBARI" ASEMA MBETO

 

Na Mwandishi  wetu,Micheweni 


Chama Cha Mapinduzi kimesema  Viongozi  wa   ACT  Wazalendo bila   kulitaja jina la Marehemu   Maalim  Seif Sharif Hamad, hawana uwezo wa kukubalika katika jamii na kupata viti  vya  udiwani ,uwakilishi ubunge na kuongeza kura za urais. 


Kimesisitiza kuwa ndio maana hueneza na kuhubiri    Siasa za utengano , shari au kukimbilia kukosoa  mfumo  wa  Muungano wa serikali  mbili si sahihi ili wapatwe kusikilizwa 


Katibu wa Kamati Maalum  ya NEC  Zanzibar  Idara  ya itikadi  ,Uenezi na Mafunzo,  Khamisi  Mbeto  Khamis, ameeleza hayo akiwa katika ziara ya kizazi huko  Micheweni Mkoa wa Kaskazini  Pemba



Akizungumza na wanachama wa  CCM  Wilaya  hiyo , Mbeto  alisema kisiasa ACT  Wazalendo  kimeshakwama, hakina maneno ya kuwashawishi wananchi ili kiweze kukubalila  na kuchagulika katika  uchaguzi mkuu wa oktoba  Mwaka huu.


Mbeto  alisema baada ya chama hicho  kukosa sera zenye matumaini kwa wananchi,  kinga yao kuu ni  kulitumia jina la Maalim  Seif, kuhubiri Siasa za fitna ,majungu na ubaguzi  au kuzungumzia muundo wa Muungano .


"Juussa na viongozi  wenzake  hawana uwezo  wa kuwaeleza lolote wazanzibari wakasilizwa na kufahamika.Wana dosari  na shutuma  katika  jamii zisizowapa heshima.Baada ya kujua  wana udhaifu huo   jina la Maalim  Seif kwao huwa ngao  yao  "Alisema Mbeto 


Aidha  alisema iwapo kungekuwa na tija ya  kuzungumzia kasoro za  chaguzi zilizopita CCM kingezungumzia chaguzi za  mwaka  1957, '61 na '63,  lakini  hakioninkama kuna  umiumu  wowote.


Alisema ACT  kinapozungumzia chaguzi  za  mwaka 1995 hadi 2015 ni katika  kuiaminisha jamii katika uongo wao wa kudai kuwa hakuna  ambao CCM kilishinda kama kinavyojidanganya. .


"Kuzungumzia Uchaguzi uliopita  ni   kutonesha vidonda vilivyoanza kupona .CCM na ACT vyote havitakiwi  kuzumgumzia  chaguzi zilizopita.Kufanya hivyo  ni kupoteza wakati  bure. Ni  sawa na kufufua makaburi ya  wafu  "Alieleza 


Alisema kwa vyovyote itakavyokuwa ,  Zanzibar  haiwezi kujitoa katika  Muungano wa serikali  mbili ili mataifa  ya Tanganyika na zanzibar yawe na mamlaka kamili kama ilivyokuwa kabla ya Aprili 26  mwaka 1964.


"Serikali ya Rais Dk   Hussein Ali Mwinyi ina cha kuwaonyesha wananchi kwa  iliofanyika miaka mitano  iliopita .Yaliofanyika yanaonekana na kila mzanzibari .Rais Dk Mwinyi hana kazi ngumu Oktoba  mwaka huu" Alisema Mbeto.


Hata hivyo, Katibu  huyo Mwenezi  aliwataka wananchi wa mkoa wa  Kaskazini  Unguja kutazama mema waliofanyiwa na serikali ya awamu ya nane  Zanzibar na manufaa walioyapata.

Post a Comment

Previous Post Next Post