JESSICA MSHAMA MGENI RASMI KATIKA KONGAMANO LA BINTI NA DKT. SAMIA.

 

Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa UVCCM Taifa, Ndugu *Jessica Mshama*, atakuwa mgeni rasmi katika *Kongamano Maalum la Mabinti na Dkt. Samia* litakalofanyika   tarehe 1 Mei 2025 katika ukumbi wa Kibo Garden. Kongamano hili limeandaliwa na *UVCCM UDSM MLIMANI* kwa lengo la kuwaunganisha vijana wa elimu ya juu na kuwawezesha kubadilishana mawazo, kuongeza uelewa wa masuala ya uongozi n.k. kama ilivyo elezwa hapo juu.


🇹🇿 Ndugu *Jessica Mshama* anatarajiwa kutoa hotuba ya kuhamasisha, kuelimisha  mabinti na vijana wote wa UDSM kushiriki kikamilifu katika kuchangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla. Kongamano hili litakuwa jukwaa muhimu kwa vijana wasomi wa kike na wa kiume kujifunza na kupata mwanga kuhusu nafasi ya vijana katika siasa na Uongozi  hasa kupitia dira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, *Dkt. Samia Suluhu Hassan*. 


 "KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE" 

Post a Comment

Previous Post Next Post