Na Mwandishi wetu
Dar es salam.
Waziri wa Uchukuzi Prof Makame Mbarawa amezungumza na Naibu Waziri wa Biashara wa China Mhe Tang Wenhong Jijini Dar es Salaam ambapo Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na China katika sekta ya usafirishaji na biashara, hasa kupitia maboresho ya miundombinu ya bandari, Reli ya TAZARA na Ujenzi wa Reli ya kisasa ya SGR
Kupitia Mkutano huo viongozi hao wamewejadili mikakati ya kuharakisha utiaji saini wa Mikataba ya miradi ya maboresho na ukarabati wa Reli ya TAZARA, kuongeza matumizi ya bandari yetu katika kusafirisha shehena, ambapo Naibu Waziri wa Biashara wa China amesisitiza dhamira ya serikali yao kuendelea kuwekeza nchini Tanzania, huku akieleza kuwa maendeleo yaliyofanyika kwenye bandari, Ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR unaoendelea, na ukarabati wa reli ya TAZARA utakaofanyika vitakuwa kichocheo kikubwa cha biashara na mahusiano ya kiuchumi baina ya nchi hizo mbili.
Hata hivyo Prof.Mbarawa ameeleza kuwa ushirikiano uliopo baina ya Nchi hizi mbili ni muhimu kwa uchumi wa Taifa na unafungua fursa zaidi kwa wafanyabiashara wa ndani na wa kanda nzima ya Afrika Mashariki.
Aidha Mkutano huo unaenda kuimarisha zaidi urafiki na ushirikiano wa kimaendeleo.
Vilevile Mkutano huo umehudhuriwa na baadhi ya Viongozi na watumishi kutoka TPA,TAZARA, na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki