PROF. MBARAWA AKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA BIASHARA WA CHINA.

 

Na Mwandishi wetu

Dar es salam.

Waziri wa Uchukuzi  Prof Makame Mbarawa  amezungumza  na Naibu Waziri wa Biashara wa China Mhe Tang Wenhong   Jijini Dar es Salaam ambapo   Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na China katika sekta ya usafirishaji na biashara, hasa kupitia maboresho ya miundombinu ya bandari, Reli ya TAZARA na  Ujenzi wa Reli ya kisasa ya SGR

Kupitia Mkutano huo viongozi  hao  wamewejadili   mikakati ya kuharakisha utiaji saini wa Mikataba ya miradi ya maboresho na ukarabati wa Reli ya TAZARA, kuongeza matumizi ya bandari yetu katika kusafirisha shehena, ambapo Naibu Waziri wa Biashara wa China amesisitiza dhamira ya serikali yao kuendelea kuwekeza nchini Tanzania, huku akieleza kuwa maendeleo yaliyofanyika  kwenye bandari, Ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR unaoendelea, na ukarabati wa reli ya TAZARA utakaofanyika vitakuwa kichocheo kikubwa cha biashara na mahusiano ya kiuchumi baina ya nchi hizo mbili.

Hata hivyo   Prof.Mbarawa   ameeleza kuwa ushirikiano uliopo baina ya Nchi hizi mbili ni muhimu kwa uchumi wa Taifa na unafungua fursa zaidi kwa wafanyabiashara wa ndani na wa kanda nzima ya Afrika Mashariki. 

Aidha  Mkutano huo  unaenda  kuimarisha zaidi urafiki na ushirikiano wa kimaendeleo.

Vilevile  Mkutano huo umehudhuriwa  na baadhi ya Viongozi na watumishi kutoka TPA,TAZARA, na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Post a Comment

Previous Post Next Post