UCHAGUZI SI MBWEMBWE NA MATUSI NI MAANDALIZI YA USHINDI -MBETO

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar 


Chama Cha Mapinduzi kimesema ACT wapande au washuke  ikiwa kisiwani  Pemba au Unguja  kijue  kitapigwa kumbo la aina yake mwaka huu na kishindo cha ushindi  wa Rais Dk Hussein Ali Mwinyi .


CCM kimewahakikishia wananchi  wa Pemba kuwa  mgombea urais wa ACT  Wazalendo Othman Masoud Othman  hana ubavu wa kumshinda kiongozi aliyeiletea Mageuzi ya kimaendeleo  Zanzibar. 


Hayo yameelezwa na Katibu  wa Kamati  Maalum ya NEC Zanzibar, Idara  ya Itikadi ,Uenezi na Mafunzo , Khamis Mbeto Khamis, aliyesema nguvu  ya umma ndio itakayomrudisha tena Rais Dk Mwinyi  madarakani. 


Mbeto  alisema  uchaguzi  wowote ili chama cha siasa kiweze kushinda ni  mpango wa maandalizi na mikakati  kabambe si mbwembwe, fedhuli wala mikogo.


Alisema CCM kinaamini  kazi kubwa ya mikakati ya kimageuzi kuelekea maendeleo ya kweli  Zanziabr, imefanywa na Rais Dk Mwinyi kwa jinsi anavyoendelea kuitumikia Zanzibar .


"ACT  kiseme na kuonyesha kimefanya nini katika kuwatumikia wananchi .Kiache kulitaja jina la Hayati  Maalim  Seif Sharif  Hamad kama mtaji  wa kupata  kura. CCM kimetenda na yaliofanyika yanaonekana kwa macho " Alisema Mbeto. 


Akijibu madai yaliotolewa na Makamu Mwenyekiti wa ACT Ismail Jussa Ladhu akiwa jimbo la Mtambwe, aliyedai  ACT  kitashinda Uchaguzi  ,ajiandae kushuhudia kikipeperushwa na kimbunga Hidaya .


"Jussa ndiye mgombanishi mkubwa baina ya  viongozi  wenzake na Hayati Maalim  Seif .Wewe Jussa ni  kirusi hatari na mchafuzi wa mahusiano toka mkiwa  CUF na sasa amkiwa ACT "Alisema Mbeto. 


Aidha Katibu  huyo Mwenezi alimtaka Jussa  asimame kama Mwanasiasa mwenye uwezo wa kujieleza na kushawishi wananchi kwa  sera za chama chake na kuacha kukitumia  jina la Maalim seif  kwani sio sera  wala maendeleo. 


"CCM haina kabrasha la  makubaliano  yoyote yaliofanyika kati ya Rais  Dk Mwinyi na  Maalim   Seif.  Kama Jussa ana ushahidi huo auonyeshe na kutaja yalioazimiwa ,  lini na wapi yalikofanyika "Alieleza


Hivyo basi, Mbeto alimtaka Makamu huyo Mwenyekiti ACT  ,aache kubwabwaja  hovyo kwa maneno  ya kutunga na kutamka maneno ya kipuuzi na yenye ujinga mwingi. 


"Jussa  huna siri zozote unazozijua  za Maalim  Seif katika siasa za Zanzibar bali wewe  ni mzandiki na mzushi baada ya Maalim Seif kufariki na kuzikwa kwa heshima  zote " Alisema


Mbeto aliwataja baadhi ya wanasiasa ndani ya ACT ambao walikuwa karibu na Maalim Seif ni kina Hamad  Rashid Mohamed na Juma Duni Haji  lakini si yeye mtoto  wa watu" Alisisitiza Mbeto

Post a Comment

Previous Post Next Post