BASHUNGWA APONGEZA JESHI LA POLISI, KWA KUMKAMATA MTUHUMIWA WA VITISHO DHIDI YA PADRI KITIMA.

::::::::::

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, amelipongeza Jeshi la Polisi kwa juhudi zake katika kufuatilia na kuchukua hatua dhidi ya matukio mbalimbali ya kihalifu, ikiwemo tukio la kukamatwa na kuhojiwa kwa mtu anayetuhumiwa kutoa ujumbe wa vitisho kabla ya shambulio dhidi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Dkt. Charles Kitima.

Bashungwa alitoa pongezi hizo leo, Mei 5, 2025, mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Jumanne Muliro, kuhusu hatua zinazochukuliwa na Jeshi hilo kufuatia matukio mbalimbali ya kihalifu.

“Nimepata taarifa za kukamatwa na kuhojiwa kwa aliyetoa vitisho kabla ya tukio la kushambiliwa la Padri Kitima. Nalipongeza Jeshi la Polisi kwa jitihada  mbalimbali zinazoendelea za ufutiliaji wa matukio mbalimbali yaliyotokea” amesema Waziri Bashungwa.

Aidha, Waziri Bashungwa amelielekeza Jeshi la Polisi kuendelea na msako dhidi ya washukiwa wa matukio yote ya kihalifu na kuhakikisha wanachukuliwa hatua kali za kisheria kwa haraka.

mussa khalidi

I am ,Journalist, Presenter Radio & TV, Producer, Video editor, Graphics Designer, Layout Newspaper designer,Contact: +255 659 669 902 Email: mussakhalid70@yahoo.com or muxabhai200@gmail.com

Post a Comment

Previous Post Next Post