Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete leo Alhamisi amefanya mazungumzo na Ujumbe wa Kiwanda cha Kutengeneza Cement Cha Dongote kutokea Mtwara walipokuja kumtembea Ofisini Dodoma wakiongozwa na Meneja wa Kiwanda hicho Nchini Bwana Adeyemi Fajobi.
Mazungumzo yao yamejikita zaidi kuzungumzia maeneo yenye changamoto na utatuzi wake. Pia Serikali kuwakumbusha umuhimu wa kiwanda hicho kwa Watanzania haswa ajira na kukuza uchumi wa miji ikianza na Mkoa wa Mtwara.
Kwa upande wake Bwana Adeyemi amemsisitizia Waziri kuendelea kufanya kazi kutatua changamoto zinazotoka mahala pa kazi na kuiomba Serikali kuendelea kushirikiana nao huku Waziri Kikwete akimuahidi kuwa serikali itaendelea kufanya kazi nao kwa pamoja kustawisha kiwanda kicho kikubwa kwa ustawi wa uchumi wa Tanzania.
#KaziInaendelea #DangoteCement
0 comments:
Post a Comment