JSON Variables

Thursday, May 8, 2025

TANAPA YAENDESHA MAFUNZO YA USIMAMIZI WA VIATARISHI


Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limefanikiwa kuendesha mafunzo muhimu ya Usimamizi wa Viatarishi kwa Wakuu wa Kanda, Wasimamizi wa Ofisi Viunganishi, Maafisa wa Hifadhi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi.


Mafunzo hayo, yaliyofanyika katika ofisi ya Kiunganishi ya TANAPA, Dodoma kuanzia Mei 5 hadi 9, 2025, yamelenga kuimarisha ufanisi katika usimamizi wa viatarishi kwa kutoa ujuzi na mbinu bora za kutambua, kudhibiti, na kuripoti viatarishi katika ngazi zote za Shirika.


Akizungumza katika katika hafla ya ufunguzi wa mafunzo haya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Godwell Meng’ataki ambaye pia ni Mkuu wa Kanda ya Kusini alieleza kuwa Semina hii elekezi inalenga kuimarisha ujuzi, uelewa wa pamoja na mbinu bora za kusimamia vihatarishi jambo ambalo ni msingi wa Utawala Bora na uwajibikaji wa TANAPA.


“Mafunzo haya ni sehemu ya juhudi za TANAPA, katika kuhakikisha kuwa utawala bora na uwajibikaji unazingatiwa katika usimamizi wa Hifadhi za Taifa, hivyo kuimarisha Uhifadhi na Utalii endelevu nchini ni matarajio yangu kuwa tukirejea katika maeneo yetu ya kazi tutakuwa na nguvu mpya ya kuhakikisha viatarishi vinatambuliwa, mikakati ya kuvithibiti inatekelezwa ipasavyo, na taarifa sahihi zinaandaliwa kwa wakati katika ngazi zote za shirika.” alisema Kamishna Meng’ataki


Semina hii elekezi, iliongozwa na wataalamu kutoka Wizara ya Fedha wakiongozwa na Msaidizi Mkaguzi Mkuu wa ndani Bw. Abrahamu Elisamia Msechu, ambaye aliendesha mafunzo katika kuimarisha utekelezaji wa Usimamizi wa Viatarishi, huku Dkt. Bernard Mnzava kutoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) akitoa mafunzo ya kina kuhusu mbinu bora za usimamizi wa viatarishi ili kufikia malengo.


Sambamba na hayo, mafunzo ya vitendo yalifanyika kupitia Mfumo wa Usimamizi wa Viatarishi wa TANAPA, Risk Information Management System (RIMS), ambapo Maafisa wa kutoka kitengo cha TEHAMA walionyesha namna bora ya matumizi ya  mfumo huo katika usimamizi wa viatarishi.

0 comments:

Post a Comment