UZUSHI NA UONGO KUHUSU MACHINJIO YA VINGUNGUTI UFAFANUZI WATOLEWA NA MEYA KUMBILAMOTO

 

Meya Kumbilamoto  akizungumza na Viongozi wa Wafanyabiashara wa Machinjio ya Vingunguti  ,kikao hiki kilikuwa cha kufafanua Uvumi na Uzushi  Uongo   ulioleta hofu na Taharuki   kwa wachinjaji na wafanyabiashara wa machinjio ya Vingunguti 


Uvumi huo ni kuwa eti Machinjio ya Vingunguti imeuzwa kwa Mwekezaji  na wafanyabiashara wataondolewa  kuchinja mle ndani  watapelekwa  Pugu  ktk ufafanuzi wake Mh Meya ni kuwataka wafanyabiashara kupuuza Mbuli Kumlomo za walimwengu  waendelee na biashara zao km kawaida huku serikali ya Mh 

Rais Dkt Samia ikiendelea kulinda ajira zao na kuboresha biashara zao , wenyeji wa Dar wa Salaam Mtakumbuka kulikuwa na uvumi miaka ya 1990 pale kituo cha polisi buguruni Mtu kageuka CHATU kumbe ni uzushi 


Upatapo taarifa hii mjulishe na mwenzio  kupuuza upuzi huu Safari ya kuifanya Vingunguti kuwa Mji unaovutia kama Istanbul  au Brunei  inaendelea tutaendelea kuwapiga Spana  Mbuli Kumlomo wote 

Kazi    Utu   Tunasongambele mimi Mtumishi wenu Kumbilamoto  .

Post a Comment

Previous Post Next Post