JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumatano, 9 Julai 2025

MAITI YA BINADAMU YATUMIKA KATIKA USAFIRISHAJI WA DAWA ZA KULEVYA

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini –DCEA akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo Julai 9,2025
......................

NA MUSSA KHALID

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini –DCEA inandelea kuwadhibiti baadhi ya wahalifu wa Dawa za kulevya ambao wameanza kutumia maiti za Binadamu kubeba dawa hizo maarufu kwa jina la begi ili kukosemsha uhalifu huo.

Kamishna Jenerali wa Mamlaka hiyo Aretas Lyimo amebainisha hayo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wanahabari akitoa taarifa ya operesheni waliyoifanya kwa kipindi cha mwezi Mei hadi Julai mwaka huu.

Kamishna Jenerali Lyimo amesema wamebaini kumekuwa na matukio ya raia wa kigeni kuwatumia watanzania kusafirisha na kusambaza dawa za kulevya kwa kutumia njia hizo hivyo amewasisitiza wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari wanapotumwa au kupokea mizigo.

‘Mara niyingi huanzisha mahusiano ya kirafiki na kisha kuwahusisha katika biashara hii haramu kwa kutumia kampuni zao na vyombo vyao vya usafiri hususani bodaboda,bajaji,Tax na wasambazaji wa vifurushi’amesema Kamisha Lyimo

Aidha Kamishna Jenerali Lyimo amesema katika operesheni hizo pia wamekamata dawa za kulevya jumla ya Kilogram 37,197.142 na watuhumiwa 64 waliohusishwa na dawa hizo.

Amesema kuwa Dawa hizo zinajumuisha kilogram 11,031.42 za dawa mpya za kulevya aina ya Mitragyna Speciosa,bangi kilogram 24,873.56,mirungi kg 1,274.47,skanka kg 13.42,heroin kg 2.21 na methamphetamine gramu 1.42.

Ameendelea kueleza kuwa katia ukamataji huo umehusisha dawa tiba zenye asili ya kulevya aina ya ketamine kilogramu 1.92,Fluni-trazepam vidonge 1000,lita 6 za kemikali bashirifu aina ya hydrochloric acid na uteketezaji wa ekari 1,045.5 za mashamba ya bangi.

Kamishna Lyimo amesema katika mkoa wa Dar es salaam eneo la Sinza waliwakamata watu wawili wamiliki wa kiwanda bubu kinachotengeneza biskuti zinazochanganywa na bangi kisha kuzisambaza katika mikoa ya Dar es salaam,Mwanza,Lindi na Mtwara amba pia wakati huohuo mkoani Lindi alikamatwa mfanyabiashara wa madini akisambamba biskuti zilizochanganywa na bangi.

‘Vilevile kwa upande wa dawa za kulevya za mashambani zilikamatwa jumla ya Kilogram 26,191.45 za bangi,mirungi,skanka na kuteketeza akari 1,045.5 za mashamba ya bangi katika mikoa ya Ruvuma,Mbeya,Mara,Kagera,Dodoma,Tabora,Morogoro na Arusha. 

Hata hivyo Mamlaka hiyo imetoa tahadhari kwa mtu yeyote atakayeendelea kujihudisha na biashara,usambazaji na uzalishaji wa Dawa za Kulevya kuwa watachukuliwa hatua kali za kisheria pindi atakapobainika.

0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio