JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Top Stories. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Top Stories. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 30 Juni 2025

MAKAMU WA RAIS AKISHIRIKI UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA UFADHILI WA MAENDELEO NCHINI HISPANIA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na  na Viongozi mbalimbali kabla ya kuanza kwa  Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Ufadhili wa Maendeleo (FfD4) unaofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Fibes Jijini Sevilla nchini Hispania. Tarehe 30 Juni 2025.

MKINGA ACHUKUA FOMU KUOMBA UBUNGE LUDEWA

Mtia nia James Innocent Mkinga (kulia), Mtaalamu mbobezi katika Fani ya Teknojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) akichukua fomu yake kuomba kuteuliwa kugombea jimbo hilo.

 

James Innocent Mkinga, Mtaalamu mbobezi katika Fani ya Teknojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

JOTO la Siasa katika Jimbo la Uchaguzi la Ludewa limezidi kupanda kufuatia kuendelea kujitokeza kwa watia nia mbalimbali wanaoashiria kuwepo kwa mchuano mkali jimboni humo. 

Jumapili Juni 29 2025, Mtia nia James Innocent Mkinga, Mtaalamu mbobezi katika Fani ya Teknojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Kada CCM na mwana harakati wa Maendeleo ya Vijana amejitokeza kwa mara ya pili kuchukua Fomu ili kushiriki katika mchakato wa kupata nafasi ya kupeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa Mbunge wa Jimbo hilo.

BIASHARA YA KABONI NYENZO MUHIMU KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mha. Hamad Yussuf Masauni akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Juni 30, 2025 mara baada ya kupokea Taarifa ya Tathmini ya Mwenendo wa Biashara ya Kaboni kutoka kwa Kamati ya Biashara ya kaboni.

.......................

Mwandishi Wetu Dar es Salaam

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mha. Hamad Yussuf Masauni amesema Biashara ya Kaboni ni miongoni mwa nyenzo muhimu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambapo nchi, taasisi, kampuni na wananchi wanaweza kushiriki katika jitihada za Kitaifa na Kimataifa za kupunguza gesijoto duniani. 

Waziri Masauni amesema hayo jijini Dar es Salaam Juni 30, 2025 mara baada ya kupokea Taarifa ya Tathmini ya Mwenendo wa Biashara ya Kaboni kutoka kwa Kamati ambapo amesema Tanzania imeimarisha usimamizi wake kwa kuanzisha Kanuni za mwaka 2022 na marekebisho yake ya mwaka 2023, pamoja na Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).

Amesema NCMC ina jukumu la kusajili miradi, kuwezesha ufuatiliaji, uthibitishaji wa gesijoto, utoaji wa elimu na uhamasishaji wa wadau. Tangu kuanza kutumika kwa kanuni, jumla ya miradi 73 ambayo miradi 69 ipo katika hatua mbalimbali za usajili na miradi 4 ipo katika hatua ya utekelezaji.

Ameongeza kwa upande wa Zanzibar imeanza kupokea maombi ya miradi ya kaboni kufuatia kupitishwa kwa Kanuni za Udhibiti na Usimamizi wa Biashara ya Kaboni za mwaka 2025. Kufikia Mei 2025, kampuni nne (4) zilionesha nia ya kutekeleza miradi hiyo, ambapo mbili (2) kati yao zimewasilisha maandiko dhana.

“Kamati hii ilipewa jukumu la kufanya tathmini na kutoa mapendekezo ya kuongeza ufanisi wa uendeshaji wa biashara ya Kaboni nchini, lengo kuu ni kufanya tathmini ya hali ya sasa ya biashara ya kaboni nchini Tanzania na kutoa mapendekezo kwa serikali kuhusu njia bora za kuimarisha mifumo na mwenendo wa biashara ya kaboni Tanzania Bara na Zanzibar.

Amesema katika kuimarisha uelewa na ushirikishwaji wa wadau katika Biashara ya Kaboni, Serikali kwa kushirikiana na wadau imeendelea kutoa elimu kwa Umma ili kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu biiashara hiyo.

Amesema Kamati imependekezwa kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu Biashara ya Kaboni, kuandaa miongozo ya mafunzo kwa wadau wa ngazi zote, pamoja na kuanzishwa majukwaa ya wadau la majadiliano katika ngazi mbalimbali.

Utekelezaji wa Biashara ya Kaboni nchini utaimarika kwa kufanya mapitio ya kanuni na miongozo ya biashara ya Kaboni, kuboresha rejesta ya Taifa ya Kaboni, kuweka mkakati mahususi wa utoaji wa elimu kwa umma, kuboresha mifumo ya usimamizi na utunzaji wa takwimu na kuhamasisha ushirikishwaji wa wadau ikiwemo sekta binafsi.

Ameongeza kwa upande wa Miradi ya kimkakati kunufaika na Biashara ya Kaboni, Tathmini inaonesha kuwa Tanzania ina nafasi kubwa ya kunufaika na Biashara ya Kaboni kupitia utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika sekta mbalimbali, ikiwemo reli ya kisasa ya umeme (SGR), Mabasi yaendayo haraka (Dar es Salaam Rapid Transit - DART), uzalishaji wa umeme, gesi asilia, misitu, kilimo, majengo, elimu, madini, udhibiti wa taka na uchumi wa buluu.  

Jumapili, 29 Juni 2025

ETDCO YANG'ARA TUZO SEKTA YA UJENZI

Mwakilishi wa Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya ETDCO, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa kampuni hiyo, Mhandisi Dismas (wa pili kutoka kushoto), akipokea Tuzo ya Heshima ya Sekta ya Ujenzi kutoka kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Gaudence Mmassy. Tuzo hizo zimeandaliwa na Construction Times Gala and Award 2025 kwa lengo la kutambua mchango wa kamapuni mbalimbali zilizofanyika 28 Juni 2025, jijini Dar es Salaam. Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Gaudence Mmassy akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa makampuni mbalimbali baada ya kutoa tuzo. 

 ..............

 Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO) imefanikiwa kupata Tuzo ya heshima ya Mkandarasi Bora wa Ujenzi na Miundombinu ya Umeme pamoja na uendeshaji wa kampuni kutoka Construction Times Gala and Award 2025 zilizofanyika 28 Juni 2025, jijini Dar es Salaam. 

 Katika tuzo hizo, Kaimu Meneja Mkuu wa ETDCO, CPA Sadock Mugendi, pia ametunukiwa Tuzo ya Uongozi Bora katika Uendeshaji wa Kampuni, ikiwa ni kutambua mchango wake katika kusimamia kwa mafanikio miradi.

 Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) wakati wa hafla ya kukabidhi tuzo hizo, iliyokwenda sambamba na uzinduzi wa Jarida la Ujenzi, Afisa Uwekezaji Mwandamizi wa TIC, Bw. Gaudence Nicholaus Mmassy, amepongeza washindi wote kwa mchango wao mkubwa katika maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini. 

 Akizungumza wakati kupokea tuzo hizo Kwa niaba ya Kaimu Meneja Mkuu wa ETDCO, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Kampuni ya ETDCO, Mhandisi Dismas Masawe, amesema kuwa tuzo hizo ni uthibitisho wa kutambuliwa kwa mchango mkubwa wa kampuni katika ujenzi wa miundombinu ya umeme nchini kwa kuonesha dira ya maendeleo wanayoifuata katika utekelezaji wa majukumu yao. 

 “Siri ya mafanikio haya ni usimamizi thabiti kutoka kwa menejimenti ya Kampuni, pamoja na kujitolea kwa dhati kwa wafanyakazi wetu, na utekelezaji wa miradi kwa weledi wa hali ya juu.” amesema Mhandisi Masawe. 

 Katika tuzo hizo za heshima zilizotolewa na Construction Times, jumla ya makampuni nane yalitunukiwa tuzo hizo za heshima, huku ETDCO ikijivunia kuondoka na tuzo mbili kubwa kutokana na utendaji wake bora, hasa katika usimamizi wa miradi na uendeshaji wa kampuni.


TUWE NA MAONO YA KUIONA KESHO YETU – DKT. BITEKO


................


📌Ni katika Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kuwa na maono ya kuweza kuona mbali hali itakayowasaidia  katika utendaji wa kazi na kupata suluhisho ya changamoto zinazoweza kutokea kabla ya changamoto hizo kutokea.

Dkt. Biteko ameyasema hayo leo Julai 28,2025 katika viwanja vya Jamhuri  Jijini Dodoma, wakati akizungumza na watumishi wa wizara na Taasisi zake wakati wa kufunga Bonanza la michezo mbalimbali lililohusisha Wizara ya Nishati na Taasisi zake.








 

Listen Mkisi Radio