Monday, April 14, 2025
TUTAENDELEA KUDHIBITI UHALIFU WA KIFEDHA-MAJALIWA
TPDC, ZPDC ZAENDELEA KUSHIRIKIANA UENDELEZAJI SEKTA YA GESI NCHINI
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) mwezi Februari, 2022 liliingia makubaliano ya ushirikiano na Shirika la Maendeleo ya Petroli Zanzibar (ZPDC) ambapo kupitia ushirikiano huo masuala mbalimbali yamekuwa yakifanyika kuiendeleza Sekta ikiwemo kubadilishana ujuzi na utaalam.
Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Aprili 14, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Kwahani, Mhe. Khamis Yussuf Mussa Mkenge aliyeuliza ni lini Serikali itainufaisha Zanzibar katika matumizi ya Nishati ya Gesi ili iweze kutumika katika magari.
"Mheshimiwa Spika katika ushirikiano huu suala la kupeleka gesi Zanzibar ni mojawapo ya agenda kuu. Pande zote mbili bado zinaangalia namna bora ya kufikisha gesi asilia Zanzibar ili iweze kupatikana kwa bei nafuu kwa watumiaji.". Amesema Mhe. Kapinga
Saturday, April 12, 2025
BALOZI NCHIMBI ASAINI KANUNI ZA MAADILI YA UCHAGUZI MKUU 2025
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ameshiriki katika utiaji saini wa Kanuni za Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025. Shughuli hiyo imefanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), ikitanguliwa na mjadala wa Makatibu Wakuu wa Vyama vya Siasa vyote vyenye usajili wa kudumu, waliohudhuria na kuridhia kanuni hizo, leo Jumamosi, tarehe 12 Aprili 2025.
Watumishi Watakiwa Kuzingatia Taratibu za Ununuzi Ili Kuepusha Mianya ya Rushwa
Na Mwandishi Wetu
TABORA
Watumishi kutoka Taasisi mbalimbali wametakiwa kuzingatia taratibu za manunuzi ili kuepusha mianya ya Rushwa na kuendelea kujenga uchumi wa nchi imara kwa manufaa ya taifa.
Hayo yanesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Paul Matiko Chacha wakati akifunga mafunzo ya kujengea uwezo watumishi kutoka taasisi mbalimbali kuhusu matumizi ya Mfumo wa NeST ambayo yamefanyika kuanzia Aprili 07 hadi 11, 2025 katika ukumbi wa Mwanakiyungi Mkoani Tabora.
Mhe. Paul amesema mafunzo hayo yamekuwa ya kipekee kwa sababu yamejikita katika moduli mpya na muhimu kwa maboresho ya michakato ya ununuzi wa umma nchini ambapo Mfumo wa NeST unaendelea kuboresha uwazi, uwajibikaji, na ufanisi katika matumizi ya fedha za umma.
“Sasa ndugu zangu mara nyingi tunasikia mfumo unachelewesha lakini mimi nasema mifumo haicheleweshi, mifumo hii imekuja kwaajili ya kurahisisha kazi zetu sasa ninyi wataalamu wetu mpo hivyo muikotroo na kwa bahati nzuri mifumo hii inaindeshwa na wewe hivyo tujitahidi kuwa waadilifu ili tuache kusingizia mfumo”alisema Mkuu wa Mkoa.
Aidha, kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhandisi Deusdetith Katwale amesema mafunzo hayo ni muuendelezo wa jitihada za serikali katika kuhakikisha changamoto za ununuzi ndani ya taifa ziwe zinashughulikiwa kimifumo ili kuendana na teknolojia inayozidi kushika kasi nchini.
“Sasa hivi serikali inashika kasi kwenye mambo ya kidijitali ambapo zamani tulikuwa tunasema serikali inawasiliana kwa makaratasi tu lakini sasa hivi serikali tunawasiliana kidijitali kwa hiyo ni mwendelezo wa kuhakikisha inakuwa na mifumo imara ya mawasiliano hivyo ni imani yangu kwamba mafunzo yaliyofanyika hapa yataendelea kuleta chachu na kupunguza mianya ya rushwa katika Serikali yetu” aliongeza Mkuu wa Wilaya.
Naye, Mkurugenzi wa Idara ya Kujenga Uwezo na Huduma za Ushauri kutoka PPRA Makao Makuu, Bi. Winfrida Samba amesema, lengo kuu la mafunzo hayo ni kupata elimu kuhusu Mfumo wa NeST na katika mfumo huo kuna moduli mbalimbali na nyingine ni moduli ni mpya ambazo zilizopelekea kufanya mafunzo hayo.
“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa katika Mfumo wetu wa NeST tuna moduli mbalimbali ikiwemo usajili ambayo inahusika na wazabuni pamoja na taasisi nunuzi, moduli nyingine ni “Etendering” ambayo inahusika na uchakataji wa zabuni pia tuna moduli ya “E-contract Management” ambayo nayo inahusika na usimamizi na utekelezaji wa Mikataba, tuna “Epayment”ambayo inahusika na masuala ya malipo lakini pia tuna moduli ndogo ambazo hizi ndizo washiriki wamejifunza zaidi” alisema Mkurugenzi Samba.
Mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa serikali kuhusu Mfumo wa NeST yameanza tarehe 7 hadi 11 Aprili, 2025 katika ukumbi wa Mwanakiyungi Mkoani Tabora.
Friday, April 11, 2025
KAPINGA ASEMA KIPAUMBELE CHA SERIKALI NI KUFIKISHA UMEME KWENYE TAASISI ZOTE
SERIKALI INAENDELEA NA UKARABATI WA MIUNDOMBINU YA UMEME – KAPINGA
Thursday, April 10, 2025
NCC YAFUNZA MBINU KUPUNGUZA GHARAMA ZA UJENZI
..........................
Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) limeendelea kuimarisha uwezo wa wataalamu wa sekta ya ujenzi nchini kwa kutoa mafunzo yatakayowawezesha kutekeleza miradi kwa ufanisi, kupunguza gharama zisizotarajiwa, na kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango vilivyokusudiwa.
Kupitia mafunzo hayo, NCC imelenga kuwajengea uwezo waajiri, wakandarasi na washauri elekezi kusimamia mabadiliko ya kazi, madai na migogoro kwa njia inayozuia upotevu wa muda, fedha, na rasilimali nyingine hali inayopunguza gharama kwenye miradi ya ujenzi.
Kwa mujibu wa wataalamu wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), miradi ya ujenzi huathiriwa na mabadiliko ya kazi, ucheleweshaji wa kushughulikia madai, na migogoro, ambavyo kwa pamoja husababisha ongezeko la gharama, muda wa mradi na hata kushusha viwango vya ubora.
Akizungumza katika mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Arusha, Mhandisi Tumaini Lemunge kutoka NCC amesema, lengo lao ni kuona miradi ya ujenzi inatekelezwa kwa gharama zilizopangwa na kwa ubora unaokubalika.
“Kupitia mafunzo haya, washiriki wamepata mbinu za kupunguza mabadiliko yasiyo ya lazima, kushughulikia madai mapema, na kutatua migogoro kwa mujibu wa mikataba” amesema Mhandisi Tumaini
Aidha Wadau mbalimbali wa sekta ya ujenzi waliopata nafasi ya kushiriki wameeleza namna mafunzo hayo yatawasaidia kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Mhandisi Lyda Osena kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) amesema “Mafunzo haya yameniongezea uwezo wa kutambua, kuepusha na kusimamia migogoro na madai kwa njia ya kisheria, vilevile yatanisaidia kutekeleza miradi kwa ufanisi zaidi, ndani ya muda, bajeti na ubora uliokusudiwa.”
Mkadiriaji Majenzi kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi amesema kuwa amepata uelewa mpya kuhusu umuhimu wa mabadiliko katika mikataba ya ujenzi hivyo anafahamu kuwa mabadiliko hayawezi kuepukwa lakini yanahitaji usimamizi makini ili kuepusha gharama zisizokuwa za lazima.
Kwa upande wake, Mwanasheria Elizabeth Kimako kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) amesema, Mwanasheria anaposhiriki katika mchakato wa ujenzi anatakiwa kuelewa kwa kina masuala ya kimkataba.
Amesema kuwa mafunzo hayo yamempa uelewa wa kusaidia taasisi yake kuendesha miradi mbalimbali kwa kwa ufanisi mzuri.


Wednesday, April 9, 2025
MNRT SPORTS CLUB YATINGA KAMBINI KWA KISHINDO.

..,............
Na Sixmund Begashe - Dodoma
Club ya michezo ya Wizara ya Maliasili na Utalii ijulikanayo kama "MNRT SPORTS CLUB" imeanza kwa kishindo mazoezi ya kujifua tayari kwa kukabiliana na timu yeyote itakayo kutana nayo kwenye michezo ya Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Dunia (MEI MOSI) inayotarajiwa kurindima Mkoani Singida hivi karibu.
Akizungumzia uwepo wa Kambi hiyo Jijini Dodoma, Mwenyekiti Msaidizi wa Club hiyo yenye wachezaji wenye uwezo mkubwa Bi ,Sharifa Dunia Salum amesema mwaka huu wamejipanga vyema katika kuhakikisha wanaibuka na ushindi mnono katika kila mchezo.
"Wachezaji wetu wote wako imara na wanahari kubwa ya kuhakikisha Wizara yetu ya Maliasili na Utalii inaibuka kidedea katika michezo yote, hatutakuwa na huruma na timu yeyote itakayokuja mbeleyetu tutaiadhibu vikali" Alisema Bi. Salum
Aidha Bi. Salum ameushukuru Uongozi wa Wizara chini ya Waziri Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, kwa kuiwezesha Club hiyo kuingia kambini na kwenda kushiriki mashinda hayo muhimu kwa ustawi wa Wafanyakazi na Taifa kwa ujumla.
"Tunaushukuru sana uongozi wa Wizara yetu, umetupa heshma kubwa na sisi tunaahudi tutailinda heshma hii kwa kutoka na ushindi wa kishindo katika michezo yote na kurejea na Makombe" Alisisitiza Bi. Salum
Club hiyo maarufu ya michezo, imekuwa ikifanya vyema kila mwaka katika michezo yake mbalimbali dhidi ya wapizao wao ambao ni timu za Wizara mbalimbali hapa nchini, na sasa inakwenda tena kuzitunishia misuli timu hizo kwenye michezo ya Mei Mosi 2025.