JSON Variables

Thursday, April 17, 2025

KUELEKEA MAADHIMISHO MALIKALE,MAKUMBUSHO YABAINISHA MAFANIKIO YAKE

Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga wakati akizungumza ofisini kwake jijini Dar es salaam akielezea katika kuelekea maadhimisho ya siku ya Siku ya Kimataifa ya Malikale ambayo hufanyika tar 18 April ya kila mwaka.

........................

NA MUSSA KHALID

Taasisi ya Makumbusho ya Taifa la Tanzania imeisisitiza jamii kuendelea kushiriki kikamilifu katika kuhifadhi malikale zilizopo nchini ili kuepukana na madhara yanayosababishwa na majanga na migogoro katika sekta hiyo.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga wakati akizungumzia kuhusu  kuelekeza maadhimisho ya siku ya Siku ya Kimataifa ya Malikale ambayo hufanyika tar 18 April ya kila mwaka.

Dkt Lwoga amesema kuwa lengo la kufanyika maadhimisho hayo ni kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa malikale katika maisha yao sambamba na kushiriki katika uhifadhi wa malikale kwa faida ya jamii hiyo.

‘Kwa mwaka huu 2025 maadhimisho haya kauli mbiu kubwa ni kuangazia madhara ya majanga na migogoro katika maeneo ya Malikale lakini pia kutafakari miaka sitini ya utekelezaji wa baraza la kimataifa la Malikale katika kutatua migogoro ya malikale na kushughulikia majanga yanayoathiri malikale hizo”

Aidha Dkt Lwoga amesema mambo yanayoathiri Malikale ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa ikiwemo maeneo ya bahari yakiongezeka kina na kuleta madhara kwenye malikalie pia kuna madhara ya nayosabishwa na majanga ya asili kama vile mafuriko.

Vilevile kwa shughuli za binadamu pia zimekua zikiathiri Malikale kwa watu kuvamia baadhi ya maeneo na kubomoa jambo linalosababisha kukosa uwepo wa ushahidi wa eneo hilo la kihistoria.

Dkt Lwoga amewasisitiza watanzania kutambua na kuhifadhi vitu vya kale ili kusaidia vizazi vya sasa na vya baadae huku akihamasisha jamii kuanzisha makumbusho binafsi.

Kuhusu Mafanikio ya Makumbusho amesema kwa sasa  wageni zaidi laki mbili wanazitembelea Makumbusho ya Taifa pamoja na maeneo ya Malikale ili kujifunza na kuelewa historia ya nchi yao.

 

WALICHOKIFANYA BODABODA MWANZA KWA MKUU WA WILAYA NYAMAGANA

 


Boda boda na samia mkoa wa mwanza wamefanya maandamano ya kushtukiza kuelekea kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya nyamagana kwa ajili ya kwenda kumuelezea nia yao kwa nchi ya Tanzania na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt samia Suluhu Hassan kwa namna anavyotekeleza miradi ya kimkakati .

Akizungumza mara baada yakufika kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya nyamagana mwenyekiti wa boda boda na samia Ramadhan Musabi ameeleza niya yao ya kile kilichopelekea kufanya kufanya maandamano hayo ya kwenda kwa mkuu wa wilaya ya nyamagana. 

Nae mkuu wa wilaya ya nyamagana Amina makilagi baada ya kuwapokea boda boda boda hao ameeleza furaha yake na kuwashukuru kwa nia yao ya dhati huku akiwaahidi kuungananao katika harakati zao zote za kuzunguukia miradi mikubwa yote iliyopo hapa mkoani mwanza.

Mbeto: Haki ya wananchi kushiriki uchaguzi isiporwe na Vyama vya Siasa


 

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar


Chama cha Mapinduzi (CCM)  kimesifu kupevuka kwa  maono ya  kisiasa  yalioonyeshwa na Kiongozi wa ACT  Wazalendo, Dorothy  Semu ,aliyeitangazia dunia  chama chake kitashiriki uchaguzi  Mkuu oktoba  mwaka huu bila  longolongo.


Pia CCM  kimebaini kuwepo  tofauti  ya uelewa, upeo, busara  na ufahamu  kati ya Kiongozi wa ACT  na Mwenyekiti  wake  Othman  Masoud Othman .


Hayo yameelezwa na Katibu wa Kamati  Maalum  ya NEC Zanzibar,  Idara  ya itikadi , Uenezi na Mafunzo ,Khamis  Mbeto  Khamis,  aliyesema kwa chama makini  ni aibu kukimbia  uchaguzi wa kidemokrasia.  


Mbeto  alisema haki ya kushiriki  uchaguzi inawahusu  zaidi  wananchi kupitia  vyama vyao  lakini  si halali kwa viongozi wa Vyama vya siasa  kuwazuia wananchi wasitumie  haki na wajibu wa kuchagua au kuchaguliwa.


Alisema si hivyo  tu ,bali kiongozi  wa ACT Wazalendo amezungumza mambo ua msingi  akitumia lugha  komavu ,maneno  yenye hekima na busara,  tofauti na matamshi holela yanayokuwa yakitolewa mara kwa mara na Mwenyekiti  wake.


"Viongozi wa Vyama vya Siasa wasipore madaraka na  haki za wananchi  Waache  kuwazuia ili wasishiriki chaguzi  za kidemokrasia. Haki za vyama zisikwapue matakwa ya  kisheria na kikatiba ya wananchi  na kugeuza  miliki ya viongozi wa vyama " Alisema Mbeto 


Aidha  Katibu  huyo Mwenezi  alisema  maelezo  alioyatoa kiongozi wa ACT Wazalendo,  hayakuambatana kabisa na maneno ya   vitisho au yenye   kujenga hofu na taharuki katika  jamii .


"Kiongozi wa ACT amejenga hoja  zake  bila kutumia  lugha  ya ubabe tofauti na Mwenyekiti wake .Hii ni tofauti iliopo kati ya Mwenyekiti na kiongozi  wa chama. Ama kweli maarifa ya  kinamama huwazidi baadhi ya kinababa ' Alieleza


Hata hivyo,  katika maelezo yake, Mbeto  akimtaka Semu afute  ndoto za ACT kukishikda CCM kwakuwa hakijapata  uwezo huo  na wananchi hawajawa tayari  kukiamini  ACT ili kuiongoza Zanzibar.


Pia  Mbeto  alisema chini ya usimamizi wa  Tume ya Uchaguzi  Zanzibar  na Tume huru ya Uchaguzi  Tanzania, vyama vya  upinzani  vimekuwa vikishinda na kupata viti vingi ikiwemo  kura za urais .


"Ni masikitiko kwa ACT  Wazalendo  kumsimamisha  Othman kuwania nafasi ya urais ili ashindane na mgombea wa CCM Rais Dk Huseein  Ali  Mwinyi. Tunakwenda kushinda mapema asubuhi kweupe" Alisema Mbeto 


Katibu   huyo Mwenezi  alisema  kulingana na kazi kubwa ilofanywa na Serikali  ya awamu ya nane, CCM kina kazi nyepesi mno ifikapo oktoba  mwaka huu.

SERIKALI KUTUMIA TRILIONI 1.18 UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA ZA WILAYA



Dodoma


Katika mwaka wa fedha 2025/26, Ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini TARURA imepanga kutumia shilingi trilioni 1.18 kwa ajili ya ujenzi, matengenezo, ukarabati wa miundombinu ya barabara na usafiri na usafirishaji wa vijijini na mijini. 


Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 257.03 ni za Mfuko wa Barabara, shilingi bilioni 127.50 Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali, shilingi bilioni 325.77 ni za tozo ya mafuta ya petroli na dizeli ya shilingi 100 kwa lita na shilingi bilioni 423.79 ni fedha za nje.


Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, OR-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa  Mwaka wa Fedha 2025/2026 jijini Dodoma.


Amesema kupitia Mfuko wa Barabara, fedha hizo zitaenda kutekeleza matengenezo na ukarabati wa barabara za wilaya zenye urefu wa  kilomita 23,105.78, box kalavati 23, mistari ya kalavati 1,647, Drift 2, na mifereji ya maji ya mvua mita 73,405, barabara za lami kilometa 17, barabara za changarawe kilometa 108.8 na madaraja 2.


Aidha, ujenzi wa kilometa 91.97 kwa kiwango cha lami, kilometa 2,621.40 za changarawe, madaraja 85, box kalavati 91, mitaro ya maji ya mvua mita 10,989 drifti tano (5), mistari ya kalavati 666 na taa za barabarani 345 zitatekelezwa kupitia Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali.


Ameongeza kuwa kupitia tozo ya mafuta ya petroli na dizeli ya shilingi 100 kwa lita, fedha hizo zitatekeleza ujenzi wa km 252.42 kwa kiwango cha lami, kilomita 6,939.41 za changarawe, madaraja 51, box kalavati 336, mistari ya kalavati 1,719, Drift 2, na mifereji ya maji ya mvua mita 63,836.


Mhe. Mchengerwa amesema ujenzi wa barabara za lami Km 147.50, ujenzi wa mifereji ya maji ya 

mvua mita 24,600, ujenzi wa masoko 9, ujenzi wa stendi kuu 4

za mabasi na stendi ndogo 2 pamoja na ujenzi wa maghala 2 

ya kuhifadhia mazao kwenye miji 12 ya Fungu la Kwanza la Mradi wa TACTIC unaendelea.


Pia kuanza kwa ujenzi kwenye Halmashauri za Miji 15 za Fungu la Pili la Mradi wa TACTIC pamoja na kukamilisha mchakato wa maandalizi ya 

Mradi wa TACTIC Fungu la Tatu katika 

Halmashauri za Miji 18.


Amesema ujenzi wa barabara Km 33 kwa kiwango cha lami katika halmashauri za Wilaya za Iringa (Wenda-

Mgama kilomita 19) na Mufindi (Mtili-Ifwagi

kilomita 14) unaendelea, pmoja na kuanza kwa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami Km 33 katika halmashauri za Wilaya za Handeni, Ruangwa na Mbogwe kupitia mradi wa RISE.


Vilevile, uboreshaji wa Bonde la Msimbazi lenye Hekta 5.7, ujenzi wa karakana ya mabasi 

ya mwendo kasi katika eneo la Ubungo 

Maziwa, ujenzi wa tuta kilomita 6.7 katika eneo la Bonde la Mto Msimbazi, ujenzi wa Bohari Mpya ya BRT eneo la Ubungo Maziwa, ujenzi wa miundombinu ya barabara awamu ya kwanza zenye jumla ya 

kilomita 132 katika Manispaa za Kinondoni,

Ubungo, Temeke, Ilala na Kigamboni.


Pia, ujenzi wa miundombinu ya 

barabara awamu ya pili ya Mradi wa DMDP 

zenye urefu wa kilomita 118 kiwango cha 

lami katika Manispaa za Kinondoni, Ubungo,

Temeke, Ilala na Kigamboni.

RAIS MWINYI:TUTANGAZE FURSA ZA UWEKEZAJI NA KUZINGATIA DIPLOMASIA YA UCHUMI.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi amewasisitiza Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika Nchi mbalimbali kuzingatia Diplomasia ya Uchumi na Kuzitangaza fursa za Uwekezaji ziliopo.


Rais Dkt, Mwinyi ameyasema hayo   alipozungumza  na Mabalozi wa  Tanzania wa Nchi za Rwanda,Zimbabwe ,Sweden na Msumbiji Waliofika Ikulu kumuaga  kabla ya kwenda katika Vituo vyao vya Kazi Baada ya kuteuliwa hivi karibuni.


Amewahimiza Mabalozi  hao kufanya Juhudi Maalum za kuitangaza Sera ya Uchumi wa Buluu na Utalii katika Mataifa hayo Ili kuvutia Wawekezaji Zaidi kuwekeza  Nchini.


Amesema Zanzibar bado inahitaji Wawekezaji wengi Hususan katika Sekta hizo Kuu za kipaumbele kutokana na kuwepo kwa fursa nyingi ikiwemo Uvuvi,Utalii na Mafuta na Gesi.


Halikadhalika Rais Dkt, Mwinyi ameeleza kuwa  Suala la Mahusiano ya Kimataifa hivi sasa limeelekezwa zaidi katika Uchumi hivyo wanapaswa kuzingatia zaidi Kuimarisha Uhusiano wa Kiuchumi.


Ameyataja Maeneo ambayo Yana fursa za kutosha kuwa ni Uwekezaji katika Sekta ya Bandari ikiwemo Bandari za Makontena ,Usafirishaji wa Mzigo, na Mafuta na Gesi.


Akizungumzia Sekta ya Biashara  amewaagiza Mabalozi hao kuzitafutia Masoko Bidhaa za Tanzania ikiwemo Bidhaa za Viungo zinazozalishwa kwa Wingi hapa Zanzibar pamoja na Utalii wa huduma na  Vivutio vya Utalii ili kuwavutia Watalii wa Mataifa hayo kutembelea Zanzibar.


Nao Mabalozi hao  wameahidi kuyatumia Maelekezo ya Rais Dkt, Mwinyi kuwa ni nyenzo na dira ya kufanya Kazi zao kwa Ufanisi pamoja na kuyazingatia Maeneo Muhimu ya Kiuchumi  kwa kuwashawishi Wawekezaji  kuwekeza.


Mabalozi walioaga ni Balozi Dkt, Habibu Kambanga- Rwanda, Balozi CP Suzane Kaganda- Zimbabwe, Balozi Mobhare Matinyi - Sweden na Balozi CP Hamad Hamad - Msumbiji.

NJE SPORTS YAICHAPA WIZARA YA UJENZI 1-0 KATIKA MCHEZO WA KIRAFIKI SINGIDA



Timu ya mpira wa miguu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje Sports) imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya Wizara ya Ujenzi katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Mwenge, mkoani Singida.


Mchezo huo, ambao ulikuwa na ushindani mkubwa na nidhamu ya hali ya juu kutoka kwa timu zote mbili, ulikuwa sehemu ya maandalizi kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yanayotarajiwa kufanyika Mei Mosi, 2025.


Bao pekee la Nje Sports lilifungwa katika kipindi cha pili na mshambuliaji Juma Jongo, aliyepokea pasi safi kutoka kwa kiungo Mukrim, baada ya shambulizi la pamoja lililotokana na umiliki mzuri wa mpira katikati ya uwanja.


Licha ya juhudi za Wizara ya Ujenzi kusawazisha bao hilo, safu ya ulinzi ya Nje Sports ilionyesha uimara mkubwa, huku kipa wao Adam Mlele akiokoa michomo kadhaa ya hatari na kudhihirisha uwezo mkubwa langoni.


Timu hizo zipo mkoani Singida kushiriki michezo mbalimbali ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) mwaka huu.

TFS Yapewa Pongezi kwa Kusaidia Upandaji Miti Sekondari ya Nyambili–Nyambunda


Na Mwandishi Wetu, Kibiti

17 Aprili 2025


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Bungu, Mhe. Ramadhan Mpendu, ameongoza zoezi la upandaji miti katika Shule ya Sekondari Nyambili–Nyambunda jana, ikiwa ni sehemu ya kampeni endelevu ya kutunza mazingira.


Katika zoezi hilo, jumla ya miti 150 ya matunda na kivuli imepandwa shuleni hapo, ambapo Mhe. Mpendu aliipongeza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa uzalishaji na usambazaji wa miche bure kwa wananchi na taasisi mbalimbali.


“Tutunze miti, itatufaa kwa vizazi vijavyo. TFS wamefanya kazi kubwa – miche hii ni dira ya mustakabali wa mazingira bora,” alisema Mhe. Mpendu mara baada ya zoezi hilo kukamilika.


Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyambunda, Mhe. Omari Msumi, Mkuu wa shule ya Sekondari Nyambili–Nyambunda, walimu pamoja na wanafunzi wa shule hiyo ambao walishiriki kikamilifu katika upandaji miti.


Mhe. Mpendu pia aliwatia moyo walimu na wanafunzi kwa kujitoa kwao katika kutunza mazingira, akisema shule hiyo inatoa mfano bora wa kuigwa katika kulinda rasilimali za asili.

Wednesday, April 16, 2025

FEDHA ZISIZOTUMIKA HADI MWISHO WA MWAKA KURUDI MFUKO MKUU WA SERIKALI

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akijibu swali bungeni jijini Dodoma, lililoulizwa na Mbunge wa Tandahimba Mhe. Katani Ahmad Katani, aliyetaka kujua lini Serikali itarejesha fedha za miradi zilizochukuliwa na Hazina.


(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha)

...................

Na. Josephine Majura, WF, Dodoma

Serikali imesema kuwa fedha ambazo hazijatumika hadi mwisho wa mwaka hurudi Mfuko Mkuu wa Serikali ikiwa ni utaratibu wa kusimamia uwajibikaji na uwazi katika matumizi ya fedha zilizotengwa katika bajeti.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Tandahimba Mhe. Katani Ahmad Katani, aliyetaka kujua lini Serikali itarejesha fedha za miradi zilizochukuliwa na Hazina.

Mhe. Dkt. Nchemba, alifafanua kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 29 cha Sheria ya Bajeti SURA 439, fedha ambazo hazijatumika hadi mwisho wa mwaka zinakoma matumizi yake na kurudishwa Mfuko Mkuu wa Serikali. 

Aliongeza kuwa iwapo kuna miradi au shughuli ambazo hazijakamilika, Fungu husika linatakiwa kutenga bajeti na kuwasilisha maombi kwa kuambatisha hati za madai au nyaraka za utekelezaji wa miradi hiyo.

Mhe. Dkt. Nchemba alisema kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha kuwa miradi yote inatekelezwa ili kuleta maendeleo kwa wananchi.