Friday, April 18, 2025
IMF YAKUNWA NA UTEKELEZAJI MIPANGO YA TANZANIA YA KUKUZA UCHUMI NA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI
BUGUMBA ATOA UJUMBE MAADHIMISHO SIKU YA MALIKALE
Mhifadhi Mkuu Mambo ya Kale na Mkuu wa Kanda ya Magharibi Makumbusho na Malikale anayesimamia uhifadhi na uendelezaji maeneo ya kusini mwa Tanzania Lindi na Mtwara Revocatus Bugumba akizungumzia siku ya Kimataifa ya Malikale ambayo hufanyika tar 18 April ya kila mwaka.
Mhifadhi Mkuu Mambo ya Kale na Mkuu wa Kanda ya Magharibi Makumbusho na Malikale anayesimamia uhifadhi na uendelezaji maeneo ya kusini mwa Tanzania Lindi na Mtwara Revocatus Bugumba akionyesha jengo la Makumbusho ya awali ambalo sasa linabaki kama malikale.
.....................
NA MUSSA KHALID
Watanzania wametakiwa kushiriki kutembelea maeneo ya Malikale zilizopo nchini ikiwemo kuzuia uharibifu wake ili waweze kujifunza historia ya nchi yao.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mhifadhi Mkuu Mambo ya Kale na Mkuu wa Kanda ya Magharibi Makumbusho na Malikale anayesimamia uhifadhi na uendelezaji maeneo ya kusini mwa Tanzania Lindi na Mtwara Revocatu Bugumba wakati akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hizi katika kuadhimisha maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Malikale ambayo hufanyika tar 18 April ya kila mwaka.
Bugumba amesema kuwa Malikale zinajumuisha maeneo na kumbukumbu za kihistoria ambayo yanahifadhiwa ikiwemo majengo ,bustani,maeneo ya kumbukumbu za kivita.
Akitolea mfano wa mji wa Dar es salaam kumesheheni maeneo ya majengo ya kale kama makanisa,mahekalu ya wahindi,majengo ya kiserikali ,maeneo ya mnazi mmoja,majengo kuanzia Ikulu na hata bustani za kale.
‘Kiujumla maeneo mengi ya Malikale huwa yanaathiriwa kwa changamoto za kiasili ambazo ni kama mabadiliko ya Tabia ya nchi,mvua kali ukame na kutokea kwa matukio makubwa yakiwemo vita” amesema Bugumba
Amesema msingi wa dhima ya Malikale imesisitiza kufanya ukusanyaji wa kumbukumbu ikiwemo kufanya tathmini ya maeneo ya malikale na kuyaweka kwenye orodha jambo ambalo litazuia uharibu.
Bungua amesema mpango mwingine ni kusisitiza jamii ishirikishwe kwa namna mbalimbali lakini pia usimamizi kuhakikisha inatumiwa mbinu za asili za uhifadhi za Malikale ili kuepukana na mtindo wa kuondoa thamani ya maeneo hayo na kuweka vitu vya kisasa.
Pia ametumia fursa hiyo kuisistiza jamii kutoa taarifa kuhusu Malikale zilizopo kwenye maeneo yao ambazo zinataka kuharibiwa ili ziweze kuhifadhiwa kwa muda mrefu.
Katika hatua nyingine ,Bugumba ametoa rai kwa Mamlaka za serikali za mitaa kuendeleza maeneo ya Malikale zilizopo kwenye miji yao ili kutopoteza uhalisia na historia ya maeneo hayo.
Mwaka huu 2025 maadhimisho hayo yanakwenda na kauli mbiu ya kuangazia madhara ya majanga na migogoro katika maeneo ya Malikale lakini pia kutafakari miaka sitini ya utekelezaji wa baraza la kimataifa la Malikale katika kutatua migogoro ya malikale na kushughulikia majanga yanayoathiri malikale hizo.
Zoezi la Uhakiki Malipo ya Mbolea za Ruzuku kwa Wakulima wa Tumbaku Tabora larizisha
Thursday, April 17, 2025
KUELEKEA MAADHIMISHO MALIKALE,MAKUMBUSHO YABAINISHA MAFANIKIO YAKE
Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga wakati akizungumza ofisini kwake jijini Dar es salaam akielezea katika kuelekea maadhimisho ya siku ya Siku ya Kimataifa ya Malikale ambayo hufanyika tar 18 April ya kila mwaka.
........................
NA MUSSA KHALID
Taasisi ya Makumbusho ya Taifa la Tanzania imeisisitiza jamii kuendelea kushiriki kikamilifu katika kuhifadhi malikale zilizopo nchini ili kuepukana na madhara yanayosababishwa na majanga na migogoro katika sekta hiyo.
Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga wakati akizungumzia kuhusu kuelekeza maadhimisho ya siku ya Siku ya Kimataifa ya Malikale ambayo hufanyika tar 18 April ya kila mwaka.
Dkt Lwoga amesema kuwa lengo la kufanyika maadhimisho hayo ni kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa malikale katika maisha yao sambamba na kushiriki katika uhifadhi wa malikale kwa faida ya jamii hiyo.
‘Kwa mwaka huu 2025 maadhimisho haya kauli mbiu kubwa ni kuangazia madhara ya majanga na migogoro katika maeneo ya Malikale lakini pia kutafakari miaka sitini ya utekelezaji wa baraza la kimataifa la Malikale katika kutatua migogoro ya malikale na kushughulikia majanga yanayoathiri malikale hizo”
Aidha Dkt Lwoga amesema mambo yanayoathiri Malikale ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa ikiwemo maeneo ya bahari yakiongezeka kina na kuleta madhara kwenye malikalie pia kuna madhara ya nayosabishwa na majanga ya asili kama vile mafuriko.
Vilevile kwa shughuli za binadamu pia zimekua zikiathiri Malikale kwa watu kuvamia baadhi ya maeneo na kubomoa jambo linalosababisha kukosa uwepo wa ushahidi wa eneo hilo la kihistoria.
Dkt Lwoga amewasisitiza watanzania kutambua na kuhifadhi vitu vya kale ili kusaidia vizazi vya sasa na vya baadae huku akihamasisha jamii kuanzisha makumbusho binafsi.
Kuhusu Mafanikio ya Makumbusho amesema kwa sasa wageni zaidi laki mbili wanazitembelea Makumbusho ya Taifa pamoja na maeneo ya Malikale ili kujifunza na kuelewa historia ya nchi yao.
WALICHOKIFANYA BODABODA MWANZA KWA MKUU WA WILAYA NYAMAGANA
Boda boda na samia mkoa wa mwanza wamefanya maandamano ya kushtukiza kuelekea kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya nyamagana kwa ajili ya kwenda kumuelezea nia yao kwa nchi ya Tanzania na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt samia Suluhu Hassan kwa namna anavyotekeleza miradi ya kimkakati .
Akizungumza mara baada yakufika kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya nyamagana mwenyekiti wa boda boda na samia Ramadhan Musabi ameeleza niya yao ya kile kilichopelekea kufanya kufanya maandamano hayo ya kwenda kwa mkuu wa wilaya ya nyamagana.
Nae mkuu wa wilaya ya nyamagana Amina makilagi baada ya kuwapokea boda boda boda hao ameeleza furaha yake na kuwashukuru kwa nia yao ya dhati huku akiwaahidi kuungananao katika harakati zao zote za kuzunguukia miradi mikubwa yote iliyopo hapa mkoani mwanza.
Mbeto: Haki ya wananchi kushiriki uchaguzi isiporwe na Vyama vya Siasa
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesifu kupevuka kwa maono ya kisiasa yalioonyeshwa na Kiongozi wa ACT Wazalendo, Dorothy Semu ,aliyeitangazia dunia chama chake kitashiriki uchaguzi Mkuu oktoba mwaka huu bila longolongo.
Pia CCM kimebaini kuwepo tofauti ya uelewa, upeo, busara na ufahamu kati ya Kiongozi wa ACT na Mwenyekiti wake Othman Masoud Othman .
Hayo yameelezwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya itikadi , Uenezi na Mafunzo ,Khamis Mbeto Khamis, aliyesema kwa chama makini ni aibu kukimbia uchaguzi wa kidemokrasia.
Mbeto alisema haki ya kushiriki uchaguzi inawahusu zaidi wananchi kupitia vyama vyao lakini si halali kwa viongozi wa Vyama vya siasa kuwazuia wananchi wasitumie haki na wajibu wa kuchagua au kuchaguliwa.
Alisema si hivyo tu ,bali kiongozi wa ACT Wazalendo amezungumza mambo ua msingi akitumia lugha komavu ,maneno yenye hekima na busara, tofauti na matamshi holela yanayokuwa yakitolewa mara kwa mara na Mwenyekiti wake.
"Viongozi wa Vyama vya Siasa wasipore madaraka na haki za wananchi Waache kuwazuia ili wasishiriki chaguzi za kidemokrasia. Haki za vyama zisikwapue matakwa ya kisheria na kikatiba ya wananchi na kugeuza miliki ya viongozi wa vyama " Alisema Mbeto
Aidha Katibu huyo Mwenezi alisema maelezo alioyatoa kiongozi wa ACT Wazalendo, hayakuambatana kabisa na maneno ya vitisho au yenye kujenga hofu na taharuki katika jamii .
"Kiongozi wa ACT amejenga hoja zake bila kutumia lugha ya ubabe tofauti na Mwenyekiti wake .Hii ni tofauti iliopo kati ya Mwenyekiti na kiongozi wa chama. Ama kweli maarifa ya kinamama huwazidi baadhi ya kinababa ' Alieleza
Hata hivyo, katika maelezo yake, Mbeto akimtaka Semu afute ndoto za ACT kukishikda CCM kwakuwa hakijapata uwezo huo na wananchi hawajawa tayari kukiamini ACT ili kuiongoza Zanzibar.
Pia Mbeto alisema chini ya usimamizi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar na Tume huru ya Uchaguzi Tanzania, vyama vya upinzani vimekuwa vikishinda na kupata viti vingi ikiwemo kura za urais .
"Ni masikitiko kwa ACT Wazalendo kumsimamisha Othman kuwania nafasi ya urais ili ashindane na mgombea wa CCM Rais Dk Huseein Ali Mwinyi. Tunakwenda kushinda mapema asubuhi kweupe" Alisema Mbeto
Katibu huyo Mwenezi alisema kulingana na kazi kubwa ilofanywa na Serikali ya awamu ya nane, CCM kina kazi nyepesi mno ifikapo oktoba mwaka huu.
SERIKALI KUTUMIA TRILIONI 1.18 UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA ZA WILAYA
Dodoma
Katika mwaka wa fedha 2025/26, Ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini TARURA imepanga kutumia shilingi trilioni 1.18 kwa ajili ya ujenzi, matengenezo, ukarabati wa miundombinu ya barabara na usafiri na usafirishaji wa vijijini na mijini.
Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 257.03 ni za Mfuko wa Barabara, shilingi bilioni 127.50 Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali, shilingi bilioni 325.77 ni za tozo ya mafuta ya petroli na dizeli ya shilingi 100 kwa lita na shilingi bilioni 423.79 ni fedha za nje.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, OR-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 jijini Dodoma.
Amesema kupitia Mfuko wa Barabara, fedha hizo zitaenda kutekeleza matengenezo na ukarabati wa barabara za wilaya zenye urefu wa kilomita 23,105.78, box kalavati 23, mistari ya kalavati 1,647, Drift 2, na mifereji ya maji ya mvua mita 73,405, barabara za lami kilometa 17, barabara za changarawe kilometa 108.8 na madaraja 2.
Aidha, ujenzi wa kilometa 91.97 kwa kiwango cha lami, kilometa 2,621.40 za changarawe, madaraja 85, box kalavati 91, mitaro ya maji ya mvua mita 10,989 drifti tano (5), mistari ya kalavati 666 na taa za barabarani 345 zitatekelezwa kupitia Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali.
Ameongeza kuwa kupitia tozo ya mafuta ya petroli na dizeli ya shilingi 100 kwa lita, fedha hizo zitatekeleza ujenzi wa km 252.42 kwa kiwango cha lami, kilomita 6,939.41 za changarawe, madaraja 51, box kalavati 336, mistari ya kalavati 1,719, Drift 2, na mifereji ya maji ya mvua mita 63,836.
Mhe. Mchengerwa amesema ujenzi wa barabara za lami Km 147.50, ujenzi wa mifereji ya maji ya
mvua mita 24,600, ujenzi wa masoko 9, ujenzi wa stendi kuu 4
za mabasi na stendi ndogo 2 pamoja na ujenzi wa maghala 2
ya kuhifadhia mazao kwenye miji 12 ya Fungu la Kwanza la Mradi wa TACTIC unaendelea.
Pia kuanza kwa ujenzi kwenye Halmashauri za Miji 15 za Fungu la Pili la Mradi wa TACTIC pamoja na kukamilisha mchakato wa maandalizi ya
Mradi wa TACTIC Fungu la Tatu katika
Halmashauri za Miji 18.
Amesema ujenzi wa barabara Km 33 kwa kiwango cha lami katika halmashauri za Wilaya za Iringa (Wenda-
Mgama kilomita 19) na Mufindi (Mtili-Ifwagi
kilomita 14) unaendelea, pmoja na kuanza kwa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami Km 33 katika halmashauri za Wilaya za Handeni, Ruangwa na Mbogwe kupitia mradi wa RISE.
Vilevile, uboreshaji wa Bonde la Msimbazi lenye Hekta 5.7, ujenzi wa karakana ya mabasi
ya mwendo kasi katika eneo la Ubungo
Maziwa, ujenzi wa tuta kilomita 6.7 katika eneo la Bonde la Mto Msimbazi, ujenzi wa Bohari Mpya ya BRT eneo la Ubungo Maziwa, ujenzi wa miundombinu ya barabara awamu ya kwanza zenye jumla ya
kilomita 132 katika Manispaa za Kinondoni,
Ubungo, Temeke, Ilala na Kigamboni.
Pia, ujenzi wa miundombinu ya
barabara awamu ya pili ya Mradi wa DMDP
zenye urefu wa kilomita 118 kiwango cha
lami katika Manispaa za Kinondoni, Ubungo,
Temeke, Ilala na Kigamboni.
RAIS MWINYI:TUTANGAZE FURSA ZA UWEKEZAJI NA KUZINGATIA DIPLOMASIA YA UCHUMI.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi amewasisitiza Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika Nchi mbalimbali kuzingatia Diplomasia ya Uchumi na Kuzitangaza fursa za Uwekezaji ziliopo.
Rais Dkt, Mwinyi ameyasema hayo alipozungumza na Mabalozi wa Tanzania wa Nchi za Rwanda,Zimbabwe ,Sweden na Msumbiji Waliofika Ikulu kumuaga kabla ya kwenda katika Vituo vyao vya Kazi Baada ya kuteuliwa hivi karibuni.
Amewahimiza Mabalozi hao kufanya Juhudi Maalum za kuitangaza Sera ya Uchumi wa Buluu na Utalii katika Mataifa hayo Ili kuvutia Wawekezaji Zaidi kuwekeza Nchini.
Amesema Zanzibar bado inahitaji Wawekezaji wengi Hususan katika Sekta hizo Kuu za kipaumbele kutokana na kuwepo kwa fursa nyingi ikiwemo Uvuvi,Utalii na Mafuta na Gesi.
Halikadhalika Rais Dkt, Mwinyi ameeleza kuwa Suala la Mahusiano ya Kimataifa hivi sasa limeelekezwa zaidi katika Uchumi hivyo wanapaswa kuzingatia zaidi Kuimarisha Uhusiano wa Kiuchumi.
Ameyataja Maeneo ambayo Yana fursa za kutosha kuwa ni Uwekezaji katika Sekta ya Bandari ikiwemo Bandari za Makontena ,Usafirishaji wa Mzigo, na Mafuta na Gesi.
Akizungumzia Sekta ya Biashara amewaagiza Mabalozi hao kuzitafutia Masoko Bidhaa za Tanzania ikiwemo Bidhaa za Viungo zinazozalishwa kwa Wingi hapa Zanzibar pamoja na Utalii wa huduma na Vivutio vya Utalii ili kuwavutia Watalii wa Mataifa hayo kutembelea Zanzibar.
Nao Mabalozi hao wameahidi kuyatumia Maelekezo ya Rais Dkt, Mwinyi kuwa ni nyenzo na dira ya kufanya Kazi zao kwa Ufanisi pamoja na kuyazingatia Maeneo Muhimu ya Kiuchumi kwa kuwashawishi Wawekezaji kuwekeza.
Mabalozi walioaga ni Balozi Dkt, Habibu Kambanga- Rwanda, Balozi CP Suzane Kaganda- Zimbabwe, Balozi Mobhare Matinyi - Sweden na Balozi CP Hamad Hamad - Msumbiji.