JSON Variables

Wednesday, April 23, 2025

MHE. KATAMBI ASISITIZA UMUHIMU WA MICHEZO KWA WAFANYAKAZI

 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi ametoa wito kwa Waajiri na Vyama vya Wafanyakazi kuweka msukumo kwa wafanyakazi kushiriki katika michezo ili kuimarisha afya zao.


Mhe. Katambi ameyasema jana Aprili 22, 2025 katika viwanja vya CCM Liti mkoani Singida wakati wa akifungua michezo ya Mei Mosi Taifa 2025 yenye kauli “Michezo kwa Afya, Ajira, Furaha, na Kazi Inaendelea. Wafanyakazi Tushiriki vyema Uchaguzi wa 2025 Tupate Viongozi Bora. Mshikamano Daima” 

"Michezo ni Afya na njia nzuri ya kujenga umoja na mahusiano mema mahali pa kazi, hivyo kuwa na afya bora kutawawezesha kutoa huduma nzuri kwa wananchi” amesema 


Aidha Mhe. Katambi amempongeza Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuwa chachu ya mafanikio makubwa katika sekta ya michezo ikiwemo kuboresha miundombinu ya viwanja vya michezo katika maeneo mbalimbali nchini.


“Jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zimeleta mafanikio katika michezo nchini tumeshuhudia hali ilivyo katika mchezo wa mpira wa miguu kupitia Goli la Mama namna lilivyowajenga wachezaji kuwa na hamasa” amesema.

Kadhalika, Naibu Waziri Katambi ametoa rai kwa waajiri kuhakikisha wanatenga muda kwa watumishi kufanya mazoezi na hivyo kujiepusha na magonjwa yanayoweza kuepukika.

HIZI HAPA HABARI KUBWA ZILIZO PEWA NAFASI KUBWA KATIKA KURASA ZA MBELE YA MAGAZETI LEO 23.04.2025

 Ikumbatie Mkisi Digital kwa Habari Moto Moto kutoka kote ulimwenguni, tunaangazia kwenye nyanja zote,  Karibu kupitia habari kubwa zilizo pewa nafasi kubwa katika kurasa za mbele ya magazeti ya leo tarehe 23.04.2025.






























Tuesday, April 22, 2025

TULINDE, TUENZI UTAMADUNI KWA MANUFAA YA VIZAZI VYETU- MAJALIWA

 

▪️Amesema tusikumbatie tamaduni zinazokwenda kinyume na maadili na ustaarabu


▪️Prof. Kabudi asema sarakasi ni mchezo unaongoza kuliingizia Taifa fedha za kigeni

 


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Watanzania wana wajibu wa pamoja wa kuhakikisha urithi wa utamaduni wa Taifa unalindwa, unaenziwa na kuendelezwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

 

Amesema hatuwezi kuwa na Taifa bila kuwa na utamaduni unaolitambulisha na kututofautisha na mataifa mengine. “Utamaduni ni utambulisho wetu halisi kama Taifa. Utamaduni wa Taifa letu ndiyo unatufanya tutambuliwe kuwa sisi ni Watanzania bila kujadili tofauti za makabila, jamii au sehemu tunazotoka.”

 

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Aprili 22, 2025) alipofungua Kikao Kazi cha 15 cha Maafisa Utamaduni na Maendeleo ya Michezo kilichofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

 

“Kamwe tusikubali kukumbatia tamaduni zinazokwenda kinyume na maadili na ustaarabu wetu. Tusikubali kuwa watumwa wa tamaduni za kigeni ambazo zinadhalilisha utu wetu. Pamoja na umuhimu wa kujifunza mambo mazuri ya tamaduni nyingine ni lazima kuchuja nini cha kuchukua na nini cha kuacha.”

 


Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwahakikishia Watanzania kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inathamini sekta za utamaduni, sanaa na michezo kutokana na umuhimu wake kwa ustawi wa Taifa, hivyo wananchi washirikiane kuwarithisha watoto na vijana misingi ya utamaduni.

 

Aidha, Waziri Mkuu amesema pamoja na utambulisho wa jamii, kupitia sekta za  utamaduni, sanaa na michezo, pia jamii inapata manufaa makubwa ikiwemo kuzalisha ajira kwa mamilioni ya Watanzania na kukuza uchumi wa Taifa.


Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa sekta hizo pamoja na kutumika kusukuma agenda mbalimbali za Kitaifa pia ni chanzo cha furaha, burudani, kuelimisha, kuonya na kuhamasisha umma katika nyanja mbalimbali.

Naye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Paramagamba Kabudi ametumia fursa hiyo kumshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuzipa kipaumbele sekta za utamaduni, Sanaa na michezo na hivyo kuziwesha kuwa na mafanikio makubwa. “Michezo ina nguvu na ushawishi mkubwa katika kuleta maendeleo na miongoni mwa michezo inayoongoza kuliletea Taifa fedha nyingi za kigeni ni riadha.”


Kwa upande wake, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Mchezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Tabia Maulid Mwita amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi na mageuzi makubwa aliyoyafanya katika sekta.

 

Awali, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Hamisi Mwinjuma amesema kuwa ili kuendelea kuvutia mageuzi ya kidijitall, Wizara hiyo kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais - TAMISEMI, imefanikisha uunganishaji wa Mfumo wa Wadau wa Sanaa (AMIS) na Mfumo wa TAUSI. Ametolea mfano mapato ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) yameongezeka kwa asilimia 200 kutokana na kuunganishwa kwa mifumo hiyo ya makusanyo.

 

Amesema kuwa hatua hiyo si tu imeimarisha usimamizi wa sekta ya sanaa, bali pia imefungua ukurasa mpya wa uwazi, urahisi wa upatikanaji wa huduma, na uboreshaji wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali. “Kuanzia tarehe 26 Februari 2025, mifumo hii miwili inafanya kazi kwa pamoja, na sasa wadau katika maeneo 15 ya biashara - ikijumuisha studio za muziki, picha, video, huduma za burudani na ubunifu - wanaweza kupata vibali kwa njia moja ya haraka na ya wazi zaidi.”

 

Naye, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa amesema kuwa Kikao kazi hicho ni cha kimkakati katika kuleta mabadiliko makubwa kwa sekta za utamaduni, sanaa na michezo ikiwa ni pamoja na kurahisisha utekelezaji wa maazimio ya vikao vilivyopita.

 

Amesema kuwa kupitia vikao kazi vilivyopita, Wizara imewezesha kuanzishwa kwa Kitengo cha Utamaduni, Sanaa na Michezo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa,Kujengewa uwezo kuhusu matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa usajili wa vyama na vilabu vya michezo nchini

 

“Kupitia vikao hivi, tumeweza kuongeza idadi ya wataalamu wa utamaduni kutoka 43 mwaka 2021 mpaka 123 mwaka 2025 na Maafisa Maendeleo ya Michezo kutoka 48 mwaka 2021 hadi Maafisa Maendeleo ya Michezo 139 mwaka 2025”

WATAALAMU KUTOKA OFISI ZA UMOJA WA AFRIKA (AUC) WATEMBELEA TMA.


Dar es Salaam.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepokea timu ya wataalamu kutoka Ofisi za Umoja wa Afrika (AUC) wanaoratibu utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma za hali ya hewa wa “Intra-ACP Climate Services and related Applications Programme (ClimSA)”.

Ziara hiyo ilifanyika tarehe 17 Aprili, 2025 ikioongozwa na mmoja wa Wasimamizi wa mradi wa ClimSA kutoka AUC Bw. Freddy Falanga (ambaye ni rai wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo), ambapo timu hiyo ya wataalamu walitembelea Ofisi Kuu ya Utabiri wa Hali ya Hewa, iliyopo Ubungo Plaza, Dar es salaam kwa lengo la kukagua utendaji kazi wa mitambo ya ufuatiliaji wa mifumo ya hali ya hewa na utabiri wa hali ya hewa, inayoitwa "PUMA STATION.", iliyotolewa kwa TMA kupitia mradi ClimSA.

Mradi wa ClimSA unatekelezwa katika nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AUC), ikiwemo Tanzania kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (European Union). Mradi huu unalenga kuimarisha zaidi uwezo wa nchi wanachama wa AU katika kufuatilia mifumo ya hali ya hewa kupitia teknolojia ya satelaiti ili kuboresha zaidi utabiri wa hali ya hewa na huduma za hali ya hewa kwa ujumla.

Huduma hizi ni muhimu kwa jamii na sekta za kiuchumi katika kupanga shughuli za maendeleo na kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi.

FIRST LADY MNANGAGWA AWASILI JIJINI ARUSHA


  Mke wa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Dkt. Auxillia C. Mnangagwa amewasili jijini Arusha na kupokelewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb), Naibu Waziri, Mhe. Dunstan Kitandula, baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Sekretarieti ya Shirika la Utalii Duniani.

Mhe.Mnangagwa anatarajiwa kushiriki Jukwaa la Pili la Kimataifa la Utalii Wa Vyakula la Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism) Kanda ya Afrika kesho Aprili 23, 2025 jijini humo.

VITONGOJI 82 TARIME VIJIJINI KUPELEKEWA UMEME NA MRADI WA HEP IIB-KAPINGA

..............................

📌Taasisi 3000 zaunganishiwa umeme na fedha za Covid 19

Vitongoji 82 ambavyo bado havijafikiwa na umeme katika Wilaya ya Tarime mkoni Mara vitapelekewa umeme kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili B  (HEP IIB) ambapo tayari zabuni ya kuwapata wakandarasi wa mradi huo imeshatangazwa na inatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga, tarehe 22 Aprili, 2025 Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara aliyetaka kufahamu lini Vitongoji vyote vya Tarime, vitapata Umeme.

Amefafanua kuwa  Jimbo la Tarime Vijijini lina jumla ya Vitongoji 500 ambapo vitongoji 225 tayari vina umeme, vitongoji 52 Wakandarasi wapo wanaendelea na kazi, na vitongoji 82 zabuni ya kuwapata Wakandarasi imetangazwa kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili B  (HEP IIB) na vitongoji 141 vilivyosalia vitaendelea kupelekewa umeme kupitia miradi ijayo.

Kuhusu mpango wa Serikali wa kuunganisha Umeme katika taasisi mbalimbali kupitia fedha za mradi wa Covid 19, Kapinga amesema tayari Serikali ilishaanza kutekeleza mpango huo ambapo mpaka sasa zaidi ya taasisi 3000 zimeshaunganishwa na umeme zikiwemo taasisi za Elimu, Afya, Dini, Migodi pamoja na visima vya maji.

Vilevile amesema kuwa Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imeendelea kuwapatia umeme wananchi kupitia miradi mbalimbali ya umeme.

JUKWAA LA KIMATAIFA LA UTALII WA VYAKULA KUKUTANISHA WABOBEZI WA UTALII ZAIDI YA 300

..............

Arusha

Jukwaa la Pili la Kimataifa la Utalii Wa Vyakula la Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism) Kanda ya Afrika lililoanza leo Aprili 22, 2025 jijini Arusha linatarajia kukutanisha washiriki takribani 300 wakijumuisha viongozi waandamizi katika sekta ya utalii na ukarimu, watumishi wa serikali, pamoja na wataalamu wa masuala ya upishi kutoka ndani na nje ya Afrika.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameyasema hayo leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye Hoteli ya Gran Melia jijini Arusha.

“Tukio hili linalenga kuangazia uhusiano muhimu kati ya utamaduni wa upishi na utalii, pamoja na kufanya tathmini ya mchango wa utalii wa vyakula katika kukuza maendeleo ya kiuchumi, kuhifadhi urithi wa kiutamaduni, na kuboresha maisha ya jamii linaandaliwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii, Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism), pamoja na Basque Culinary Center” amesema Mhe. Chana.

Amefafanua kuwa  hafla ya ufunguzi wa Jukwaa hilo itafanyika tarehe 23 Aprili, 2025, ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango.

Mhe. Chana ameongeza kuwa kupitia jukwaa hilo la kihistoria Tanzania itapata fursa ya kuonesha utajiri wa vyakula vya asili vinavyotokana na makabila zaidi ya 120 nchini Tanzania.

“Jukwaa hili litakuwa ni sehemu mahsusi ya kukuza utalii wa chakula, na hivyo kuongeza wigo wa mazao ya utalii nchini, kuwezesha wageni kukaa muda mrefu zaidi nchini na kuchochea mchango wa utalii katika uchumi wa taifa letu” amesisitiza Mhe. Chana.

Waziri Chana ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wadau wote wa sekta ya utalii na mapishi, pamoja na wananchi wote, kushiriki kikamilifu katika kuunga mkono na kuendeleza dhana hiyo muhimu ya utalii wa vyakula, kwa mustakabali wa maendeleo ya sekta ya utalii na utambulisho wa Taifa letu kimataifa.

Naye, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Shirika la Utalii Duniani, Elcia Grandcourt, amesema jukwaa la kimataifa la utalii wa vyakula litasaidia kukuza utalii hasa vijijini na kuhifadhi utamaduni wa asili.

"Hii ni nafasi yetu ya kuonyesha tunachoweza kutoa sio tu kutoka Tanzania bali katika Bara lenyewe la Afrika" amesema Bi. Grandcourt.

Jukwaa hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wa kimataifa wakiwemo Katibu Mkuu wa Shirika la Utalii Duniani, Bw. Zurab Pololikashvili, pamoja na Mke wa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Dkt. Auxillia C. Mnangagwa.


RAIS MWINYI ASHIRIKI SALA YA MAZISHI YA MAREHEMU SANYA

,
..............................

Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Hussein Ali Mwinyi amejumuika na Wananchi katika Mazishi ya Marehemu Muhammad Ibrahim Sanya yaliofanyika Leo .

Rais Dkt,Mwinyi aliwaongoza  Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Sala ya Maiti  katika Msikiti Jibril Mkunazini , Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 22 Aprili 2025.

Marehemu Ibrahim Sanya amefariki Jana  wakati akitibiwa  katika Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa Wa Mjini Magharibi Lumumba .

Wakati wa Uhai wake Marehemu Ibrahim  Sanya aliwahi kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Jimbo la Mkunazini  kwa tiketi ya Chama Cha Wananchi (CUF).

Marehemu Sanya amezikwa eneo la Makaburi ya Kijitoupele,Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi.