JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumatano, 7 Mei 2025

CCM YAOMBOLEZA KIFO CHA MZEE MSUYA

......

Chama Cha Mapinduzi kimepokea Kwa huzuni na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha mmoja na viongozi waandamizi nchini,Mzee Cleopa  David Msuya kilichotokea leo



 

KERO YA MAJI KIJIJI CHA MLOKA, MBUNJU MVULENI NA NDUNDUTAWA YAPATIWA UFUMBUZI.

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI na Mbunge wa Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameshuhudia hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa miradi ya Maji itakayojengwa katika Vijiji vitatu vya Mloka, Mbunju Mvuleni pamoja na Ndundutawa ambayo itahudumia Wananchi 16, 593 hali itakayosaidia kupunguza kero ya Maji katika maeneo hayo.

Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilayani Rufiji Mhandisi Alkam Sabuni, alisema ujenzi wa Miradi ya Maji katika Vijiji hivyo utagaharimu kiiasi cha Shilingi 791,068,682.56.


"Katika Kipindi Cha Mwezi Juni 2025 hadi Oktoba 2025 Wananchi wapatao 16,593 wa Vijiji vitatu vya Mloka, Mbunju Mvuleni na Ndundutawa wanaenda kunufaika na huduma ya Maji safi na salama na yenye kutosheleza, ambapo miradi hii itakapokamilika itaongeza hali ya upatikanaji wa Maji kutoka asilimia 86.6 ya sasa hadi asilimia 97.3" alisema Sabuni

Hafla ya Utiaji Saini wa Mikataba ya ujenzi wa miradi hiyo imefanyika katika Kijiji Cha Mloka Kata ya Mwaseni Jana Mei 6, 2025.


Sabuni aliongeza kuwa RUWASA Wilayani Rufiji inatoa huduma katika Vijiji 38 vyenye Jumla ya Watu 157,412 kwa Mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa alisema uwepo wa miradi iyakapokamilika itasaidia kupunguza adha ya Wananchi kwenda kuchoma Maji katika Mto Rufiji.


"leo tumeandika historia katika changamoto ambazo tumekuwa tukizipata kwa muda mrefu leo tumezimaliza na matarajio yangu kwamba Mkandarasi sasa ataanza kazi mara Moja" alisema Mchengerwa.


Rais Mwinyi Afanya Uteuzi Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Dkt. Hussein Ally Mwinyi amefanya uteuzi leo kwa kumteua Ndugu Madina Mjaka Mwinyi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mafunzo ya Amali Zanzibar.

Ndugu Madina ni Mstaafu katika Utumishi wa Umma Zanzibar.


KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA DAR ES SALAAM YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WILAYA YA TEMEKE

 

-Kamati imeridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo na kutoa Shukrani kwa Rais Dkt Samia kwa kuwezesha utekelezaji wa miradi hiyo.  

Kamti ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam leo Mei 7, 2025 ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo Mhe Abbas Mtemvu imetembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa kwa fedha nyingi zinazotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ambapo kwa ujumla Kamati hiyo imeridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo.

Akiongea wakati wa Ukaguzi wa miradi hiyo Mhe Abbas Mtemvu amempongeza Mkuu wa Mkoa na viongozi wote waliochini yake kwa kazi nzuri wanayoifanya hususani utekelezaji wa mzuri wa miradi ya maendeleo yenye masilahi mapana kwa umma pamoja na ushirikiano mkubwa walionao kati ya Chama na Serikali.

Aidha kwa upande wa Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila amesema miradi yote katika Mkoa huo, itakamilika kwa wakati kwa viwango na kuzingatia thamani ya fedha "Value for Money " 

Vilevile amesema mkakati wa Mkoa kwa sasa kutokana na ufinyu wa Ardhi na ongezeko kubwa la idadi ya watu, majengo mengi ya umma ikiwemo shule, vituo vya Afya kwa sasa vitajengwa kwa Ghorofa ili kutumia vizuri Ardhi iliyopo.


Mwisho Kamati hiyo ikiwa katika muendelezo wa kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo imekagua ujenzi wa Jengo la Ghorofa la Shule ya Sekondari Mangaya linalojengwa Mbagala, Maradi wa Hospitali ya Wilaya ya Temeke unaojengwa Chamazi na Kituo cha Polisi cha Kisasa kinachojengwa Toangoma.

Mkutano wa 14 wa Baraza la Usimamizi wa Mkataba wa Lusaka kuanza Arusha kesho

 



ARUSHA


Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa 14 wa Baraza la Usimamizi wa Mkataba wa Lusaka (14TH Governing Council Meeting of Parties to the Lusaka Agreement) utakaofanyika jijini Arusha katika Hoteli ya Gran Melia kuanzia Mei 8,2025.


Hayo yamesemwa leo Mei 7,2025 jijini Arusha na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt.Pindi Chana wakati akizungumza na wanahabari.

"Tumekutana hapa hii leo kwa lengo la kuwaomba kutumia vyombo vya habari mnavyoviwakilisha kufikisha ujumbe kwa Watanzania kuhusu mkutano mkubwa na wa kipekee wa masuala ya Uhifadhi wa Wanyamapori na Misitu unaoatarajiwa kufanyika hapa nchini kwetu hususani katika Jiji hili la Utalii la Arusha."


Amesema,mkutano huu hufanyika mara moja kila baada ya miaka miwili ambapo kwa mara ya mwisho ulifanyika nchini Zambia mwezi Machi, 2022.


Balozi Dkt.Chana amesema,Baraza la Usimamizi wa Mkataba wa Lusaka, ulianzishwa mwaka 1994 kwa lengo la kuziwezesha nchi za Afrika kusaidiana katika kukabiliana na ujangili na biashara haramu ya nyara yakiwemo mazao ya misitu inayovuka mipaka ya nchi.

Tanzania ilijiunga na Mkataba huu mwaka 1999 na imekuwa ikiutekeleza kwa kushirikiana na nchi wanachama ambazo ni pamoja na Congo-Brazzaville, Kenya, Lesotho, Liberia, na Zambia.


"Kupitia Mkataba huu, Tanzania imenufaika katika nyanja mbalimbali ikiwemo kubadilishana taarifa za uhalifu wa makosa yanayohusu wanyamapori na misitu."


Mafanikio mengine amesema ni kufuatilia na kukabiliana na mitandao ya ujangili wa wanyamapori na misitu,kufanya operesheni na doria na mafunzo ya kukabiliana na vitendo vya uhalifu.

"Katika mkutano huu wa 14 ambao utafanyika hapa nchini kwetu katika Jiji hili la Arusha, pamoja na mambo mengine utapokea taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa 13 wa Baraza na utaidhinisha Mpango Mkakati wa Mkataba wa Miaka mitano (2025-20230)."


Aidha, Tanzania kupitia Waziri wa Maliasili na Utalii, itapokea nafasi ya Urais wa Baraza la Usimamizi wa Mkataba kwa kipindi cha miaka miwili ijayo kutoka kwa Waziri wa Maliaisili wa Kenya.


Waziri Chana amesema, kufanyika kwa mkutano huu katika jiji la Arusha ni fursa ya kutangaza utalii, kufanya biashara na kushiriki katika juhudi za kikanda na kimataifa za kukabiliana na ujangili na biashara haramu ya wanyamapori na mazao ya misitu.

Kwa mujibu wa Kanuni za Uendeshaji wa Mikutano ya Baraza, mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na takribani Mawaziri 19 wanaoshughulikia masuala ya Maliasili na Mazingira kutoka katika nchi 19 za Afrika.


Sambmba na wawakilishi kutoka katika Mashirika ya Umoja wa Mataifa (UNEP, UNODC, UNDP, INTERPOL WCWG) na Katibu Mkuu wa Mkataba wa Kimataifa wa Biashara ya Wanyamapori na Mimea Iliyohatarini kutoweka (CITES).


Aidha, kwa Tanzania,Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na taasisi zake zinazounda Wakala wa Utekelezaji wa Mkataba (National Bureau) zitashiriki.

NHIF SASA KUGHARAMIA MATIBABU YA AFYA YA AKILI, KUFUATA MWONGOZO

 

NA WAF, DODOMA 


Serikali imesema huduma za afya ya akili zimeshajumuishwa kwenye vifurushi vya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), na hivyo wananchi wanaonufaika na bima wanaweza kupata matibabu hayo kwa mujibu wa mwongozo wa matibabu uliopo.


Akijibu swali la Mbunge wa Iringa Mjini, Mhe. Jesca Msambatavangu, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema kuwa, huduma za afya ya akili, ushauri nasaha, pamoja na huduma za kibingwa kama vile utengamao, zote zimetajwa kama huduma muhimu kwenye Mwongozo wa Matibabu (Standard Treatment Guideline – STG) na zinagharamiwa na NHIF.


“Huduma hizi zinalipiwa kwa kuzingatia aina ya dawa na ngazi ya kituo cha huduma, kwa mujibu wa mwongozo wa matibabu wa Taifa,” amefafanua Naibu Waziri  Dkt. Mollel.


Serikali imeendelea kuhakikisha kuwa huduma za afya ya akili zinapewa uzito sawa na huduma nyingine za msingi, na kuimarisha upatikanaji wake kupitia mifumo ya bima ya afya kwa wote.

HOSPITALI ZA BENJAMIN MKAPA, MLOGANZILA KUENDELEA KUTUMIKA KAMA VITUO VYA MAFUNZO UDOM NA MUHAS

 

NA WAF, DODOMA


Serikali imesema Hospitali ya Benjamin Mkapa na Hospitali ya Mloganzila zitaendelea kuwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya kwa madhumuni ya kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi na kuboresha ubora wa huduma sambamba na kutumika kama vituo vya mafunzo kwa wanafunzi wa vyuo vya Vikuu vya Dodoma na Muhimbili.


Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Dkt. Thea Medard Ntara, Mei 07, 2025  kuhusu mpango wa kuzirudisha hospitali hizo chini ya vyuo husika, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, amesema vyuo hivyo bado vinaendelea kuzitumia hospitali hizo kama sehemu ya mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wa kada za afya.


“Vyuo vikuu vya Muhimbili na Dodoma vinaendelea kutumia Hospitali ya Mloganzila na Benjamin Mkapa kama hospitali za kufundishia, kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya katika kuhakikisha mazingira bora ya kitaaluma na huduma kwa wananchi,” amesema Dkt. Mollel.


Aidha, Dkt. Mollel amefafanua kuwa, usimamizi wa Wizara ya Afya umelenga kuimarisha mifumo ya huduma za afya huku ukihakikisha kuwa mahitaji ya vyuo vikuu vinavyotoa programu za afya yanaendelea kuzingatiwa.

SHULE 216 ZA SERIKALI ZATUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA-KAPINGA

 

NA MWANDISHI WETU

NAIBU Waziri Nishati,  Judith Kapinga amesema hadi kufikia mwezi Machi 2025 takribani Shule za Serikali 216 zimehamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo kati ya hizo, Sekondari 146 zinatumia gesi ya LPG.


Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 07, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Liwale, Mhe. Zuberi Mohamedi Kuachauka aliyeuliza ni lini majiko yanayotumia gesi yataanza kutumika kote nchini.


“Serikali kupitia REA inaendelea kutoa ruzuku ya ujenzi wa miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule nyingine na  tarehe 20 Aprili, 2025, REA kupitia Wizara ya Nishati imepokea kibali kutoka TAMISEMI cha kufunga miundombinu ya huduma ya nishati safi ya kupikia katika shule 115 zikiwemo shule za Mikoa za sayansi za wasichana 16; shule za kitaifa za wavulana 7, shule za bweni za kawaida 66 na shule kongwe za sekondari 26”. Amesema Mhe. Kapinga


Amesisitiza kuwa Serikali kupitia REA na wadau mbalimbali itaendelea kufunga miundombinu ya nishati ya kupikia katika shule za sekondari kulingana na upatikanaji wa fedha. 


Mhe. Kapinga ameongeza kuwa Wizara ya Nishati kupitia Wakala wa Nishati Vijijini i(REA) inatekeleza miradi ya kufunga mifumo ya nishati safi ya kupikia Jeshi la polisi na Magereza katika Mikoa 24, jeshi la Zima Moto  pamoja na huduma za Wakimbizi.


Aidha, amesisitiza kuwa upo mkakati wa kufunga mifumo ya nishati safi ya kupikia katika Taasisi zilizo chini ya Wizara ya afya ikiwemo hospitali za Mikoa, za Wilaya na za kitaifa takribani 21.


Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Tunza Malapo aliyetaka kufahamu ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha shule, Zahanati na Vituo vya afya vipya vinajengwa vikiwa na mifumo ya nishati safi ya kupikia, Mhe. Kapinga amesema kupitia mkakati wa nishati safi ya kupikia ambao utekelezaji wake umeanza kutekelezwa, Serikali inaelekea kwenye mtazamo huo wa Shule, Zahanati na Vituo vya afya kujengwa sambamba na miundombinu ya nishati safi ya kupikia.

Listen Mkisi Radio