Joe Biden amekuwa akikabiliwa na kibarua kigumu baada ya utendakazi wake duni katika mdahalo wa kwanza wa urais 2024 dhidi ya Donald Trump.
Huku uchaguzi wa Novemba ukikaribia, idadi ya wafuasi wa chama cha Democratic wanaomnamtaka rais ajiondoe kwenye kinyang'anyiro hicho kutokana na wasiwasi kuhusu afya yake inaongezeka.
Makumi ya Wademocrats wametoa wito hadharani kumtaka Bw. Biden kutogombea urais na kumpisha mtu mwinye umri mdogo kwenye chama chake.
Bw. Biden ameapa kugombea muhula wa pili, amesisitiza hilo katika mikutano ya hadhara na mahojiano katika vituo vya habari vya ABC News na MSNBC.
0 Comments