WAZIRI MKUU AZINDUA LANGO LA UTALII HIFADHI YA MKOMAZI


.....................

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 25, 2025 amezindua lango la kuingia na kutoka watalii la Ndea kwenye Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi iliyoko Wilaya ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro.

Uzinduzi wa lango hilo ambalo limegharimu Shilingi Milioni 350 ni sehemu ya maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ili kuchochea na kuongeza vivutio vya utalii nchini.

Akitoa taarifa ya lango hilo Mhifadhi Mkuu Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, Emmanuel Mwailama amesema ujenzi wa lango hilo utaongeza idadi ya watalii katika mbuga hiyo ambao wengi wanakwenda kuona maisha ya wanyama pembezoni mwa ziwa jipe, Faru weusi pamoja na tembo.

mussa khalidi

I am ,Journalist, Presenter Radio & TV, Producer, Video editor, Graphics Designer, Layout Newspaper designer,Contact: +255 659 669 902 Email: mussakhalid70@yahoo.com or muxabhai200@gmail.com

Post a Comment

Previous Post Next Post