JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumatatu, 16 Juni 2025

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA


........................

📌 Wizara ya Nishati na TAMISEMI zaendelea kushirikiana kuhakikisha  Shule mpya zinafungwa mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema gharama ya kujaza gesi kwenye mitungi (LPG) ni himilivu ikiwa ni jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ili kuwezesha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Juni 16, 2025 katika ziara ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Simiyu  wakati wa kuzindua Shule Maalum ya Sayansi ya Wasichana ya Simiyu ambayo imefungwa miundombinu ya nishati safi ya kupikia. 

“Mheshimiwa Rais ulituelekeza Taasisi ambazo zinahudumia watu zaidi ya mia moja tuzifungie miundombinu ya nishati safi ya kupikia, Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na TAMISEMI tunatekeleza agizo hilo kwa kuzifungia mifumo ya nishati safi shule mpya ambazo zinajengwa." Amesema Kapinga

Ameeleza kuwa,  uwezo wa shule hiyo ni wanafunzi 800 na mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia iliyofungwa ina uwezo wa kuhudumia wanafunzi 800.

Ameongeza kuwa, kwa idadi hiyo ya wanafunzi 800  mtungi wa gesi katika Shule ya Wasichana Simiyu utakuwa ukijazwa kila  baada ya miezi miwili.


0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio