Macho na akili za mashabiki wa mpira wa miguu nchini tanzania na duniani kote waliokuwa wakiisubilia siku ya leo tarehe 27.04.2025 kuushuhudia mtanange wa maamuzi makubwa sana , Baadhi ya mashabiki wa club ya Simba wamesema wapotayari kufanya chochote na popote imradi timu yao iweze kushinda
Juma hamis ni mkazi wa Temeke Mwembeyanga anasema yeye ni mnazi wa club ya Simba na leo hii simba anaibuka na ubingwa na kusonga kwenye fainali kisha kurudi na kombe nyumbani baada ya ushindi katika fainali itakayo fanyika baada ya Simba kushinda mechi ya leo ninafuraha sana kwa sababu hii siku niliisubilia kwa hamu sana nimeamini kwamba SIKU HAZIGANDI HATA UKIZIWEKA KWENYE FRIJI
Kwa upande wake Rose Anthony mkazi wa Dodoma ambaye yeye ni shabiki kindaki ndaki wa club ya Young Africans, Amesema watani wetu wameweza kupiga hatua kubwa sana kufikia hii leo kiasi kwamba ninawivu sana kwaajili yao, japokua mimi ni shabiki wa yanga sina kinyongo na watani wetu wa jadi kwa sababu wanacho kifanya wanaiwakilisha Taifa kiujumla kwa hiyo sina budi kuwa shabikia katika michuano hii ya kimataifa, wamalize salama waje na kombe nyumbani lakini wajue kwamba kwenye ligi yetu ya NBC sisi ndiyo mabingwa licha ya viporo walivyo bakisha
BIG SCREEN ya kumuangalia Mnyama akitinga fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika inakusubiri pale viwanja vya Mbagala Zakhiem. Mo Cola wamesimamia mpango mzima kufanikisha hili.