JSON Variables

Tuesday, May 6, 2025

ASEMA MBETO "CCM ITAHESHIMU NA KUFUATA USHAURI BILA KUVUNJA KATIBA NA SHERIA "


Mwandishi  Wetu, Zanzibar 


Chama Cha Mapinduzi  kimesema kwa miaka yote  kimepokea , kusikiliza na kutekeleza Ushauri  wa Wazee, watu  mbalimbali , Viongozi wa Dini na  Kijamii  bila kukiuka  matakwa ya Katiba na Sheria. 


CCM na serilali  zake huendesha utawala bila  kuingilia mipaka ya Sheria  huku kikiheshimu madaraka ya  Serikali,  Bunge  na Mahakama.


Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC Zanzibar,  Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis , ameeleza hayo alipotakiwa  kutoa maoni yake kufuatia ushauri uliotolewa na  Waziri Mkuu  Mstaafu  Joseph  Warioba.


Mbeto alisema  Serikali  haziwezi kuzuia Uhuru wa mawazo  ya watu na ushauri wa Wazee, lakini akawataka wanaoshauri  ,  watambue  kuna mahali  unapoishia ushauri  wao.


Alisema  kupokea ushauri  si kosa ila kosa huweza kuwa  makosa zaidi  aidha  katika utekelezaji wa Ushauri  huo    usiokiuka na kuvunja Sheria, Katiba au kuingilia  madaraka ya mihimili mingine. 


'Ushauri  wa Wazee utabaki kuwa sehemu ya utamaduni  wa Serikali  za CCM. Kama Taifa tumefika mahali  tulipo kwa  kuthamini michango  na ushauri  wa Wazee . Kila jambo lina kipimo na mipaka ya utekelezaji wake  " Alisema  Mbeto .


Katibu huyo  Mwenezi  aliongeza kusema , kupokea ushauri   wowote , lazima anaeshauri na anayeshauriwa wote  walitazame  suala husika kama lipo kisheria , lina ugumu na wepesi  upi  ,  kwakuwa  kila hatua, inahitaji kutekelezwa kwa umakini na tahadhari. 


"Mwalimu Julius  Nyerere  alitoa  msamaha kwa Wafungwa wa Kesi ya uhaini baada ya Mahakama kuhukumu  kisheria.  Rais hakuingilia kesi wakati  ikiwa   Mahakamani. Alifanya hivyo kwa kuheshimu dhana ya  mgawanyo wa Madaraka "Alieleza  


Mbeto  alisema katika Kesi  ya kina Michael  Kamaliza na wenzake    , alikuwemo  Mpigania Uhuru  Mstari  wa mbele wa TANU , Titi Mohamed lakini Rais kwanza  aliheshimu Sheria na Mhimili wa Mahakama.


Aliongeza kusema    ikiwa leo Viongozi  aidha wa CCM, ACT , Chadema ,  Chauma na vingine, ikitokea kuvunja sheria,  kisha  yaanze  mazungumzo ya  usuluhishi, itakuwa kila anayevunja sheria lazima iwepo meza ya mazungumzo , huko si katika kuheshimu dhana ya  Utawala wa  Sheria.


"Meli, Jahazi au Ngarawa zinapita majini .Ukiona vyombo hivyo vinasafiri Nchi Kavu au Angani  huo ni uchuro. Sheria lazima  ifuate mkondo   wake. Iwe kwa Wazee  , Wanasiasa au Viongozi  wote tutumie hekima kila  tunaposhauri" Alieleza.


Kadhalika Mbeto  alisema katika Awamu ya Tano ya Utawala kulikuwa na  baadhi ya mambo kadhaa yalioonekana kuwa magumu lakini hawakutokea

Wazee waliokuwa na ujasiri  na  kushauri lolote .

0 comments:

Post a Comment