JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Ijumaa, 23 Mei 2025

CHANGAMOTO ZA NJAA NA UMASKINI ZINAHITAJI MAJIBU YA PAMOJA YA KIMATAIFA

 

kuangaziwa katika kukabiliana na njaa na umasikini ikiwemo vita na migogoro ya kisiasa, mabadiliko ya tabianchi, ukosefu wa miundombinu muhimu kwaajili ya kilimo kama vile umwagiliaji, uhifadhi mazao pamoja na TEHAMA ambayo husaidia taarifa muhimu za mbegu, masoko na bidhaa za kilimo.



Ametaja changamoto zingine za kuangaziwa kama vile ukosefu wa ufadhili katika sekta ya kilimo, changamoto ya kuuza malighafi ambazo hazijaongezwa thamani, uwekezaji katika utafiti na maendeleo, kukosekana kwa taarifa muhimu katika sekta ya kilimo, changamoto za kiteknolojia katika nyanja zote za uzalishaji pamoja na changamoto ya sera za ushuru na biashara ambazo hazihamasishi kukua kwa kilimo na shughuli za kilimo.

Majadiliano kati ya Brazil na Nchi za Afrika ni ya pili katika mzunguko wa majadiliano ya namna hiyo, ambapo majadiliano ya kwanza yalifanyika mwaka 2010 nchini Brazil. Majadiliano hayo huandaliwa na Serikali ya Brazil kupitia Wizara ya Kilimo ya nchi hiyo kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kiufundi la Brazil (ABC) Pamoja na Shirika la Utafiti wa Kilimo la Brazil (EMBRAPA).

Majadiliano hayo huwaleta pamoja Viongozi wakuu wa Serikali, Mawaziri wa Kilimo kutoka Afrika, Mashirika ya Kimataifa kama FAO, IFAD, WFP, Benki ya Dunia pamoja na wataalamu na washirika wa kiufundi. Kadhalika majadiliano hayo yametoa fursa ya kipekee ya kuangazia maeneo ya ushirikiano chini ya Mpango wa Kimataifa dhidi ya Njaa na Umaskini (Global Alliance against Poverty and Hunger) uliozinduliwa kwenye Kikao cha G20 Novemba 2024, jijini Rio de Janeiro, pamoja na kujadili mafanikio ya moja kwa moja katika sekta za kilimo, usalama wa chakula na lishe, ushirikiano wa kiufundi na biashara ya kimataifa.

Katika Mkutano huo, Makamu wa Rais ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula Dkt. Hussein Omar Pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Brazil Mhe. Balozi Dkt. John Simbachawene.

0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio