JSON Variables

Saturday, May 10, 2025

Kongamano la Kimataifa la 18 la Elimu Mtandao kwa Afrika lafikia kilele, Mhe. Zainab Katimba (Mb) Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi (Elimu) akishiriki katika kilele hicho.

 

Mhe. Zainab Katimba (Mb) Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI (ELIMU)  tarehe 9 Mei, 2025 amehudhuria kilele cha Kongamano la Kimataifa la 18 la Elimu Mtandao kwa Afrika ‘eLearning Africa’ ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mhe. Hemed Abdulla Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akimwakilisha Mhe Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.


Mhe. Hemed Abdulla amewataka washiriki wote kuendelea kuunga jitihada za pamoja katika kukuza matumizi ya TEHAMA katika elimu kwa mustakabali wa Tanzania na nchi nyingine za Afrika. Aidha, amewaalika wafanyabiashara, wawekezaji na taasisi kuja kuwekeza na kuongeza wigo wa ushirikiano Tanzania Bara na Zanzibar katika teknolojia ya digiti hususani elimu na biashara.

0 comments:

Post a Comment