JSON Variables

Friday, May 9, 2025

MNEC GHULAM AONYA WANAOICHONGANISHA CCM NA WANANCHI


Na Shushu Joel, Kisarawe 


MJUMBE wa Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa anayetokana na Umoja wa Wanawake Tanzania Bi, Nadra Ghulam amewaonya watumishi wa umma wenye tabia ya kuichonganisha ccm na wananchi.


Onyo hilo amelitoa alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mafumbi kata ya Chole Wilaya ya Kisarawe alipotembelea na kujionea jinsi wananchi walivyoungana na kujenga zahanati hiyo kwa nguvu zao.


"Watumishi wengi wa umma wamekuwa wakikisemea vibaya chama jambo ambalo wananchi wanakiona chama akifanyi kazi kumbe ni uongo mtupu hivyo niwaombe wananchi muwapuuze wote wenye nia mbaya na ccm" Alisema Mnec Nadra Ghulam. 


Aidha amewapongeza wananchi wa kijiji hicho kwa umoja wao wanaouonyesha katika ujenzi wa maendeleo ya kijiji chao.


Pia amewataka wananchi hao kuendelea kutembea kifua mbele kwani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan anawatendea haki kubwa watanzania katika sekta ya maendeleo. 


Kwa Upande wake Diwani wa kata ya Chole Moshi Mgalu amempongeza Mnec Nadra Ghulam kwa jinsi ambavyo ametatua changamoto za papo kwa papo za wananchi.


Aliongeza kuwa hakika Mnec Nadra Ghulam ameonyesha kuwa ni msaidizi mkubwa wa Rais Dkt Samia. 

0 comments:

Post a Comment