JSON Variables

Friday, May 9, 2025

MUENDELEZO WA ZIARA YA KAMATI YA SIASA CCM MKOA DAR ES SALAAM KUKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KWA MIRADI YA KIJAMII NA MIRADI YA MAENDELEO

 

📍Ubungo

🗓08 May 2025


Abasi Mtemvu Mwenyekiti wa CCM Mkoa ameongozana na wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa katika Ukaguzi utekelezaji wa ilani ya CCM Wilaya ya Ubungo.  Mwenyekiti *Mtemvu* amewapongeza watendaji wa serikali katika kutekeleza miradi hiyo na amewasisitiza wananchi kutunza miradi hiyo ambayo imetumia gharama kubwa kwa ajili ya maendeleo ya wana Ubungo. Miradi iliyokaguliwa ni:- 


🎤 ~*Mradi wa maji wa booster* (DAWASA)- KIBAMBA ambao unagharimu *Tsh Bilioni 36.9* ambapo mradi huo unatarajia kunufaisha zaidi ya wananchi takribani *77000* wa wilaya ya ubungo, Temeke na Ilala kwani maji yatakuwa yanatoka mara mbili kwa wiki

🎤~*Mradi wa ujenzi wa vyumba 4 vya madarasa na matundu 8 ya vyoo* katika shule ya sekondari ya Mbezi Inn, ambapo mradi huo umegharimu *Tsh milioni 114* mpaka kukamilika kwake

 


🎤~*Mradi wa ujenzi wa uboreshaji wa kituo cha afya makulumla* ambao unatekelezwa kwa pesa za ndani kwa gharama ya *Tsh milioni 380* ambao ulianza 2022 na unatarajiwa kukamilika mapema tarehe 1/6/2025 ambapo mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar Es salaam ndugu *Abasi Mtemvu* amewasihi mafundi katika mradi huu kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha haraka mradi huu.

🎤~ *Mradi wa ufungaji wa Ufungaji wa Transforma 4* kubwa kituo cha umeme cha NIT ambao unafadhiliwa na pesa za ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa gharama ya *Tsh Bilioni 125* ambapo unatarajiwa kukamilika tarehe 3/11/2025 kwani vifaa vimekamilika kwa 95%


Kadhalika; Mkuu wa mkoa wa Dar Es salaam ndugu *Albert Chalamila* ameijulisha kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Dar Es salaam kuwa ameziagiza Halmashauri zote zinazounda mkoa wa Dar Es salaam kuhakikisha *zinatenga Fedha ili kujenga vituo vya polisi kwa kushirikiana na jeshi la polisi* ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuendelea kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao ndani ya jiji la Dar Es salaam.

Pongezi kwa serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi  wa Rais *Dkt Samia Suluhu Hassan* kwa kuendelea kusogeza huduma za kijamii kwa wananchi wa Ubungo


*Imetolewa na Idara ya siasa na uenezi mkoa wa Dar Es saalam*


#Ccm Imara

#Kaziiendelee

# DktSamiaMitanoTena🖐🏿


©️Kazi na Utu Tunasonga mbele 2025

0 comments:

Post a Comment