JSON Variables

Friday, May 9, 2025

AWAMU YA TATU YA MRADI WA MAABARA WA (EAC) WAZINDULIWA LEO, NAIBU WAZIRI WA AFYADKT. GODWIN MOLLEL AKISHIRIKI KATIKA UZINDUZI HUO.


 Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel ameshiriki katika uzinduzi wa Awamu ya Tatu ya Mradi wa Mtandao wa Maabara wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Mobile Labaratory Project Phase III) uliofanyika tarehe 9 Mei, 2025 katika Makao Makuu ya EAC jijini Arusha kando ya Mkutano wa 25 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Afya wa Jumuiya hiyo.


Mradi huo unaolenga kuimarisha uwezo wa nchi wanachama kukabiliana na milipuko ya magonjwa na dharura za afya kwa njia ya uchunguzi wa haraka wa maabara sambamba na kuwajengea uwezo wataalam wa maabara katika nchi wanachama za EAC.

Viongozi wengine waliombatana na Dkt. Mollel katika uzinduzi huo ni: Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayeshughulikia masuala ya sayansi, Prof. Daniel Mushi, Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe na maafisa waandamizi kutoka katika Wizara, Idara na taasisi za Serikali Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ya Mapinduzi Zanzibar.


Aidha, katika awamu ya kwanza na ya pili ya mradi huo Tanzania ilinufaika kwa kupata vifaa na mafunzo ya kitaalam, maabara mbili za afya zinazotembea (Mobile Laboratories) na kuimarisha mifumo ya taarifa na uhifadhi wa sampuli.

Tanzania inaendelea kushirikiana na nchi wanachama kuimarisha mifumo ya afya ya kikanda ili kuyafikia malengo yaliyowekwa ya kuwazesha wananchi kupata huduma bora za afya na zenye uhakika.

0 comments:

Post a Comment