JSON Variables

Sunday, May 11, 2025

NYAHOZA AKIPONGEZA CHAMA CHA CCK KWA KUMPATA MGOMBEA URAIS

Naibu Msajili wa vyama vya siasa nchini Sisty Nyahoza akizungumza na wajumbe wa Chama Cha Siasa Cha Kijamii (CCK) katika mkutano Mkuu maalum wa Chama hicho kwa ajili ya kuwachagua na kuwapitisha wagombea nafasi ya Urais wa Tanzania Bara na Zanzibar ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kijamii cha CCK David Daudi Mwaijolele ambaye pia amepitishwa kwa kupigiwa kura kugombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bara akizungumza katika mkutano Mkuu maalum wa Chama hicho ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam.

Aisha Salum Hamadi ambaye amepitishwa kugombea nafasi ya Urais kupitia Chama cha Kijamii cha CCK Zanzibar akizungumza na wajumbe wa chama hicho katika mkutano Mkuu maalum wa Chama hicho ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam.

Viongozi wa Kitaifa wa Vyama vya siasa waliohudhuria katika katika mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha siasa cha Kijamii cha CCK ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam.

Wajumbe mbalimbali waliohudhuria katika mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha siasa cha Kijamii cha CCK ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam. 

........................

NA MUSSA KHALID

Naibu Msajili wa vyama vya siasa nchini Sisty Nyahoza amekipongeza Chama Cha Siasa Cha Kijamii - CCK kwa kufanya Uchaguzi wa wazi na demokrasia wa kumchagua Mgombea Urais wa Tanzania bara na Zanzibar kupitia Chama hicho.

Katika Uchaguzi huo uliofanyia jijini Dar es salaam wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho wamepiga kura na kumchagua Mwenyekiti wa Chama hicho David Daudi Mwaijojele kuwa mgombea Urais kwa Tanzania Bara huku  Isha Salum akiteuliwa na Halmashauri kuu kuwa mgombea Pekee wa Nafasi ya Urais Kupitia Chama Cha CCK  Zanzibar.

Akizungumza kwenye mkutano huo Naibu Msajili wa vyama vya siasa Sisty Nyahoza amevisisitiza Vyama vya siasa nchini kueendelea kudumisha amani na kulinda umoja wetu wakati huu wa kuelekea uchaguzi ili nchi iweze kupita salama.

Nyahoza amesema mkutano huo umefanyika kwa sababu taifa lina amani na hivyo mtu yeyote mwenye nia ya kuvunja amani ni vyema akakemewa mapema.

‘Umoja wetu ndio unatufanya tuwe Pamoja hapa tukiwa wazanzibari na watu wa bara hivyo tulinde umoja wetu ili tfanye siasa kwa amani na utulivu’amesema Nyahoza

Kwa upande wake Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kijamii cha CCK David Daudi Mwaijolele amesema kuwa wananchi watarajie makubwa pindi atakapofanikiwa kuitangaza mikakati mbalimbali wakati wa kampeni.

Amesema kuwa malengo yao ni kutaka kuhakikisha jamii ya kitanzania inaishi maisha bora katika maeneo mbalimbali ya kilimo ,uvuvi,ujasiriamali ikiwemo makundi maalum.

‘Chama cha CCK tutakapopewa ridhaa kupitia tume Tutahakikisha vijana wanaweza kujiajiri wenyewe pindi wanapomaliza elimu,lakini pia wanawake kunufaika na uchumi wao’amesema Mwaijolele

Naye Aisha Salum Hamadi ambaye amepitishwa kugombea nafasi ya Urais kupitia chama chake cha CCK Zanzibar amesema kuwa anajivunia kuwa mwanamke wa kwanza chama chake kumuamini kuiepeperusha bendera ya chama katika visiwa hivyo.

Amesema kuwa yupo tayari kukipambania chama cha CCK kwa Zanzibar ambapo vipaumbele vyake ni kuwasaidia watui wenye uhitaji wakiwemo walemavu.

Amewasisitiza watanzania kuwaonyesha mshikamano kwa kuwaunga mkono kukichagua chama chao ili kiweze kuwasaidi kuzitatua changamoto mbalimbali kwenye maeneo yao.

   

0 comments:

Post a Comment