JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumapili, 18 Mei 2025

Rais Mwinyi ajivunia utendaji wa Serikali yake Zanzibar



Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 


Chama  Cha Mapinduzi  kimesema kina matumaini makubwa ya kushinda Uchaguzi Mkuu wa Oktoba  Mwaka  huu, baada ya  kutekeleza ahadi  zake za kisera zilizoleta maendeleo na kuwatumikia wananchi kwa Haki na Usawa.


Kimesisitiza kitashinda tena na kuongoza Serikali  ya zanzibar  kwa ridhaa na matakwa ya wananchi ili kukata ngebe za upinzani  Visiwani humu.


Makamu Mwenyekiti  wa CCM  Zanzibar  na Rais wa SMZ  , Dk Hussein Ali Mwinyi , ameeleza hayo katika mkutano  wa hadhara akifungua  Tawi la CCM  la kisasa huko Mpendae Juu ,Mkoa wa Mjini Magharibi Kisiwani Unguja. 


Rais Dkt  Mwinyi  alisema CCM kitashinda kwa kishindo na kupata kura nyingi   bada ya kutekeleza wajibu wake wa kuwatumikia wananchi kwa  vitendo ,hali ilioleta mabadiliko ya kimaendekeo ,.


Alisema kutokana na  CCM kutimiza ahadi zake zilizoleta mageuzi  katika  sekta muhimu za maendeleo ,hatua hizo zimekuza ustawi kwa wananchi kupitia  ilani ya uchaguzi ya CCM Mwaka 2020/2025.


"Wananchi  na wana CCM  wa Mkoa wa Mjini Magharibi nina furaha kuona  mmejiandikisha kwa wingi katika  Daftari la Kudumu la Mpiga Kura. Kazi iliobaki na jukumu  lenu ni kupiga  kura ifikapo oktoba mwaka huu"Alisema Rais Dk Mwinyi 


Aidha Makamu  huyo Mwenyekiti wa CCM  Zanzibar ,alisema kujitokeza kwenu na kupiga kura kwa mgombea  urais wa zanzibar kupitia  CCM , Wabunge ,  Wawakilishi na Madiwani wa chama chenu  kutaka ngebe za wapinzani  wetu .


Aliwasisitiza wananchi na wana CCM,Rais huyo  wa Zanzibar alisema kazi kubwa iliobaki iko mikononi mwa wananchi ya kujitokeza mapema na kupiga  kura.


"Kazi imebaki kwenu ya kukirudisha chama chenu madarakani. Tutahakikisha Zanzibar  inazidi kupaa  kimaendeleo kuliko ya miaka mitano ya kwanza. Hiyo ni ahadi yangu  kwenu na kwa wazanzibari  wote "Alisisitiza Rais Dk Mwinyi

0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio