Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amempongeza Profesa Mohamed Yakoub Janabi kwa kuchaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika.
Uteuzi huu ni uthibitisho wa mchango mkubwa alioutoa Profesa Janabi katika sekta ya afya, pamoja na dhamira yake ya kuimarisha mifumo ya afya barani Afrika.
Zanzibar itaendelea kuunga mkono ajenda ya afya ya kikanda na kimataifa, pamoja na kushirikiana kwa karibu na Profesa Janabi katika juhudi za pamoja za kuboresha huduma za afya.
0 comments:
Chapisha Maoni