Karibu Tanzania, Karibu Nyumbani.
Ikulu jijini Dar es Salaam leo nimempokea Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mheshimiwa Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah. Kama ilivyokuwa enzi za waasisi wa mataifa yetu, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Hayati Sam Nujoma, tunaendelea kuimarisha udugu na ushirikiano ambao ulianza tangu kipindi cha kupigania uhuru, ambapo baada ya kupata uhuru wa kisiasa, sasa tunajikita katika kuimarisha uchumi na ustawi wa nchi zetu.
Katika mazungumzo yetu tumeazimia kukuza uhusiano uliopo, na kufungua fursa mpya za ushirikiano kupitia sekta mbalimbali zikiwemo biashara na uwekezaji, mifugo na uvuvi, uchumi wa buluu, utalii na lugha ya Kiswahili, kwa manufaa ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Dkt. Netumbo ni dada kwangu. Nimefarijika kumkaribisha tena nchini Tanzania, mahali alipoishi kuanzia mwaka 1980 hadi 1986 akiwa nguzo muhimu katika mapambano dhidi ya ukoloni na ubaguzi wa rangi nchini Namibia.
0 comments:
Chapisha Maoni