JSON Variables

Tuesday, May 13, 2025

TRC YATOA TAARIFA JUU YA AJALI YA TRENI YA ABIRIA KUTOKA PUGU KWENDA KAMATA

 


Jumla ya watu 10 wamejeruhiwa baada ya treni ya abiria maarufu kama treni ya Mwakyembe inayofanya safari zake kati ya Kariakoo na Pugu jijini Dar es Salaam, kupata ajali baada ya mabehewa yake matatu kuacha njia.


Ajali hiyo imetokea leo Mei 13, 2025, majira ya saa 11:00 jioni eneo la Kamata ikielekea Machinga Complex uelekeo wa Pugu.


Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Amana, amekiri kupokea majeruhi 10 waliotokana na ajali hiyo kati yao nane ni wanawake na wawili ni wanaume.

0 comments:

Post a Comment