UJENZI WA DARAJA LA JPM UMEFIKIA 99% KUKAMILIKA MWANZA

 

Mradi mkubwa wa ujenzi wa Daraja  la JPM linalounganisha wilaya ya Misungwi na wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza umefikia asilimia 99  ili kuweza kukamilika .

Hayo yamesemwa na msemaji mkuu wa Serikali Greyson Msigwa mara baada ya kufanya ziara katika Daraja hilo na kujionea hatua ya ujenzi iliyofikiwa ambapo kwasasa yamebakia marekebisho madogo ili kukamilika

Msigwa pia amesema kuwa daraja hilo litakuwa na uhai wa miaka mia moja ambapo siku nyingi litaanza kufanya kazi ili kuondoa changamoto ya wananchi kusubiri kivuko kwa muda mrefu


Aidha kwa upande wake Msimamizi wa Mradi wa ujenzi huo Mhandi Wiliam Sanga kutoka Tanroad amesema kuwa tangu kuanza kwa ujenzi   wa  mradi huo jumla ya ajira 33505 ambapo wazawa ni asilimia 91.9 ambapo mpaka sasa wamemlipa mkandarasi shilingi Bilioni 539 . 

Katika ziara hiyo ya Msemaji mkuu wa serikali ametembelea na kukagua pia mradi wa ujenzi wa vivuko 5 vinavyojengwa na Songoro Marine pamoja ujenzi wa meli ya Mv Mwanza. 

Post a Comment

Previous Post Next Post