JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Gospel. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Gospel. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 23 Mei 2025

SERIKALI IMETOA RUZUKU YA ASILIMIA 20 HADI 50 KWENYE MITUNGI YA GESI LAKI 4.4 – KAPINGA


📌 *Asema lengo ni kupunguza gharama na kuhamasisha Nishati Safi ya Kupikia*


*📌  REA kusambaza majiko banifu 200,000 kwa punguzo la hadi asilimia 75*


📌 *Baada ya umeme kufika kwenye vijiji vyote; Serikali kuendelea kuhamasisha matumizi ya majiko ya umeme*



Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali imetoa ruzuku ya asilimia 20 hadi 50 kwenye mitungi ya gesi ya LPG takribani 452,445 kwa watumiaji wa mwisho ikiwa ni jjtihada za kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.


Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 23, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Grace Tendega aliyetaka kufahamu Serikali ina mkakati gani wa muda mfupi wa kuhakikisha Wananchi wa Vijijini wanatumia Nishati Safi ya kupikia badala ya Kuni na Mkaa.

 

"Mheshimiwa Mwenyekiti Serikali kupitia REA pia  itasambaza majiko banifu 200,000 yenye bei ya punguzo la hadi asilimia 75 pamoja na kuwezesha ufungaji wa mifumo ya nishati safi ya kupikia katika Taasisi za Umma zinazohudumia watu zaidi ya 100."  Amesema  Kapinga


Aidha, amesema Serikali imekamilisha kazi ya usambazaji umeme katika vijiji vyote hivyo kwa sasa inaendelea kuhimiza matumizi ya majiko ya kupikia yanayotumia umeme ikiwa ni njia mojawapo ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi wa vijijini badala ya kutumia kuni na mkaa.


Mhe. Kapinga ametanabaisha  kuwa, Mkakati wa Taifa wa  Nishati Safi ya Kupikia ni wa miaka kumi lakini Serikali inao mkakati wa matumizi bora ya nishati ambao unahusisha pia sekta binafsi kwa ajili ya kusaidia kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.


Akijibu swali la Mbunge wa Mbulu, Mhe. Zacharia Isaay aliyeuliza Serikali imejipangaje kuhakikisha Vitongoji vyote vilivyokusudiwa katika mwaka huu wa bajeti kufikiwa  na umeme katika kipindi cha mwezi mmoja uliobaki, Mhe. Kapinga amesema Serikali inayo mikakati na miradi mbalimbali ya kupeleka umeme katika Vitongoji. 


Amesema kuwa, moja ya mikakati hiyo ni kupeleka umeme katika Vitongoji 15 kwa kila Jimbo, na pia  Serikali imekuja na mkakati wa kupeleka umeme katika Vitongoji 20,000 ambapo   awamu ya kwanza inaanza kupeleka umeme katika Vitongoji 9000 na hatua iliyopo ni utafutajj wa wakandarasi.


Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Anatropia Theonest aliyeuliza bei ya Serikali ya ruzuku imeanza kutumika lini kutokana na mitungi ya gesi kuendelea kuuzwa kati ya 22,000/- na 25,000 na kwa mitungi mikubwa ya kilo 15 shilingi 50,000/- na 60,000/-,  Mhe. Kapinga ameeleza kuwa kwa maeneo ya mjini Serikali imepeleka ruzuku hadi asilimia 25 na maeneo ya Vijijini ni kati ya asilimia 50 hadi 75 na kutolea mfano iwapo mtungi ulikuwa unauzwa shilingi 45,000/- kwa bei ya ruzuku inapatikana kwa shilingi 17,000/- hadi 21,000/- na kusema ni zaidi ya nusu ya bei yake.


Ameongeza kuwa, katika kila Wilaya kuna takribani mitungi 3,255 inayopatikana kwa ruzuku na kuongeza kuwa ndio kwanza mkakati umeanza.


Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Yustina Rahhi alieuliza mpango wa Serikali kuwapelekea jamii ya wafugaji teknolojia ya biogas au kuwajengea majiko yanayotumia samadi ya gesi ambayo ni rahisi, Mhe. Kapinga amesema Serikali inatekeleza mradi huo kupitia umoja wa Ulaya (mfuko wa UNCDF) ambao unateknolojia alizozitaja Mhe. Mbunge.


Akijibu swali la Mbunge wa Nyang’wale, Mhe. Hussein Amar aliyeuliza kuhusu mpango wa Serikali kuzipelekea nishati safi ya kupikia  Shule za Sekondari 19 na Sekondari 12 za bweni zilizo Wilaya ya Nyang’wale ili kulinda mazingira,  Mhe. Kapinga amesema Wizara ya Nishati inaompango wa kuzipelekea nishati safi ya kupikia Taasisi za umma kwa kushirikiana na TAMISEMI.


Katika hatua nyingine Mhe. Kapinga amezishauri Halmashauri  kufunga mifumo ya nishati safi ya kupikia  katika Taasisi zilizopo katika Halmashauri wanazoziongoza kwa kutumia mapato ya ndani.

Jumanne, 13 Mei 2025

KIJANA KABLA YA KUOA SOMA HII

 

Kijana wangu njoo  usikie maneno yangu

 Usioe mwanamke ambaye kwa kumtazama tu unajua ana matunzo ,anaweza kuwa anajitunza mwenyewe anapendeza ,au ana matunzo nyuma usiyoyajua ..endapo unajua maisha Yako ni ya kuungaunga usisogee Kaa pembeni. 


Chukuaaliye pauka au wa kawaida ili angalau wewe unatakapokuwa unampa mafuta ya 3000 anafurahi na kuona anathaminiwa ,, lakini ukichukua mtu anapaka mafuta ya 140000, sabuni ya 40000

Wakati wewe laki na40 unaipigia hesabu za mwezi mzima 😃😃 utaenda pasuka kichwa huko ....


Mwanamke anapiga pamba za 700k 

Wewe unawaza kumzawadia kitenge cha morogo utaenda kuumia

OA mwanamke anayefanana na kiwango chako Cha maisha utaishi kwa furaha ..OA mwanamke anayezidi kiwango chako Cha maisha ukapate presha ...


Usije sema sikusiki ..umesikia Leo


#PASTORLEAH 

.

Ijumaa, 9 Mei 2025

Robert Prevost ni nani? Mfahamu kwa undani Papa mpya Leo XIV

 

Hata kabla jina lake halijatangazwa kutoka kwenye roshani ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, umati wa watu uliokuwa chini ulikuwa ukiimba "Viva il Papa" kwa maana ya Ishi milele Papa.

Robert Prevost, mwenye umri wa miaka 69, atakuwa kiongozi wa 267 kwenye kiti cha enzi cha Mtakatifu Petro na atajulikana kama Leo XIV.

Atakuwa Mmarekani wa kwanza kushika wadhifa wa Papa, ingawa anachukuliwa kuwa Kardinali kutoka Amerika ya Kusini kwa sababu ya miaka mingi aliyotumikia kama mmisionari nchini Peru, kabla ya kuwa askofu mkuu huko.

Ana uraia wa Peru na anakumbukwa kwa upendo kama mtu aliyefanya kazi na jamii zilizotengwa na kusaidia kuungfanisha jamii katika Kanisa la eneo hilo.

Alizaliwa Chicago mwaka 1955, Prevost alihudumu kama kijana wa altare na aliwekwa wakfu kuwa padri mwaka 1982.

Katika maneno yake ya kwanza kama Papa, Leo XIV alizungumza kwa upendo kuhusu mtangulizi wake Francis.

"Bado tunasikia masikioni mwetu sauti dhaifu lakini daima yenye ujasiri ya Papa Francis ambaye alitubariki," alisema.

"Tukiungana na kushikana mikono na Mungu, tusonge mbele pamoja," aliwaambia umati wa watu waliokuwa wakishangilia.

Aliwaambia umati uliokuwa ukisikiliza katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kwamba alikuwa mwanachama wa Shirika la Augustino. Alikuwa na umri wa miaka 30 alipohamia Peru kama sehemu ya misheni ya Augustino.

Francis alimteua kuwa Askofu wa Chiclayo nchini Peru mwaka mmoja baada ya kuwa Papa.

Anawajua vizuri Makadinali kote ulimwenguni kwa sababu ya nafasi yake muhimu kama mkuu wa Baraza la Maaskofu.

Kwa kuwa asilimia 80 ya makadinali walioshiriki mkutano mkuu waliteuliwa na Francis, haishangazi sana kwamba mtu kama Prevost alichaguliwa.

Ataonekana kama mtu aliyeunga mkono kuendelea kwa mageuzi ya Francis katika Kanisa Katoliki.

Ingawa ni Mmarekani, na atakuwa anafahamu kikamilifu mgawanyiko ndani ya Kanisa Katoliki, historia yake ya Amerika ya Kusini pia inawakilisha mwendelezo baada ya Papa aliyetoka Argentina.

Ingawa wakati wake kama askofu mkuu nchini Peru hakuepuka kashfa za unyanyasaji wa kijinsia ambazo zimegubika Kanisa, jimbo lake lilikanusha vikali kwamba alihusika na jaribio lolote la kuficha ukweli.

Kabla ya mkutano mkuu, msemaji wa Vatican Matteo Bruni alisema kuwa wakati wa mikutano ya Baraza la Makadinali katika siku zilizotangulia mkutano mkuu walisisitiza umuhimu wa kuwa na Papa mwenye "roho ya kinabii inayoweza kuliongoza Kanisa ambalo halijifungi ndani bali linajua jinsi ya kwenda nje na kuleta mwanga kwa ulimwengu uliojaa kukata tamaa".

Kutoka BBC Swahili.

2004, Papa Leo XIV alifika nchini Tanzania

Mwaka 2004, Papa Leo XIV alifika nchini Tanzania na kufanya ziara kama Mkuu wa Shirika la Waagustiniani Ulimwenguni. 

Katika.ziara hiyo Papa Leo anayetoka katika Shirika la Order of Saint Augustine (OSA), alifika jijini Dar es Salaam kisha akaenda mkoani Njombe.

Ziara hiyo pia ilihusisha maeneo ya Mahanje hadi mkoani Songea.

 

Alhamisi, 8 Mei 2025

MRITHI WA PAPA FRANCISCO APATIKANA LEO MEI 8 2025

HUYU HAPA PAPA MPYA, KIONGOZI MKUU WA DHEHEDU LA KANISA KATORIKI DUNIANI.

Robert Francis Prevost, aliyezaliwa tarehe 14 Septemba 1955 mjini Chicago, Marekani, ni Papa mpya wa Kanisa Katoliki, akichukua jina la Papa Leo wa XIV.  Kuchaguliwa kwake mnamo Mei 8, 2025, kunamfanya kuwa Mmarekani wa kwanza kushika wadhifa huu katika historia ya miaka 2,000 ya Kanisa Katoliki.

ELIMU NA MAISHA YAKE YA AWALI

Prevost alihitimu Shahada ya Sayansi katika Hisabati kutoka Chuo Kikuu cha Villanova mwaka 1977.  Baadaye, alijiunga na Shirika la Mtakatifu Augustino (OSA) mwaka huo huo, na akaweka nadhiri zake za milele mnamo Agosti 1981.  Alipata Shahada ya Uzamili katika Theolojia kutoka Catholic Theological Union mjini Chicago, na kisha Shahada ya Uzamili na Shahada ya Uzamivu katika Sheria ya Kanisa kutoka Chuo Kikuu cha Kipapa cha Mtakatifu Thomas Aquinas (Angelicum) mjini Roma  .


HUDUMA YA KICHUNGAJI NA UONGOZI 

Baada ya kupewa daraja la upadre mwaka 1982, Prevost alitumwa Peru mwaka 1985 kama mmisionari.  Alitumikia katika maeneo mbalimbali ya Peru, ikiwa ni pamoja

Listen Mkisi Radio